Sure: AL-QALAM 

Vers : 31

قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tumekuwa warukao mipaka



Sure: AL-QALAM 

Vers : 32

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Sure: AL-QALAM 

Vers : 33

كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Kama hivyo ndivyo inakuwa adhabu (ya hapa duniani), bila shaka adhabu ya akhera ni kubwa zaidi, laiti wangalijua!



Sure: AL-QALAM 

Vers : 34

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema



Sure: AL-QALAM 

Vers : 35

أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ

Je, Tuwafanye Waislamu (watiifu) sawa Kama wahalifu?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 36

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ

Mmekuwaaje Nyinyi, Vipi mnahukumu?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 37

أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 38

إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ

Kwamba hakika Yatakuwamo Kwa ajili yenu mnayo yachagua (mnachopendelea)?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 39

أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ

Au je, mnavyo viapo juu yetu vinavyofika mpaka siku ya Kiyama ya kuwa ninyi mtapata mnayo yahukumu?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 40

سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ

Waulize Hao: Ni nani miongoni mwao mdhamini wa hayo?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 41

أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli



Sure: AL-QALAM 

Vers : 42

يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ

Siku ambayo yatakapokuwa mateso makali, na wataitwa kusujudu lakini hawataweza



Sure: AL-QALAM 

Vers : 43

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ

Macho Yao yatainama chini, udhalilifu utawafunika. Na hali walikuwa wakiitwa wasujudu (kuswali duniani) walipokuwa wazima wa afya



Sure: AL-QALAM 

Vers : 44

فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ

Basi Niache na anayekadhibisha Maneno haya (Qurani hii) Tutawavuta pole pole adhabuni kwa namna wasiyoijua



Sure: AL-QALAM 

Vers : 45

وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ

Na Ninawapa muda, hakika mpango Wangu ni Madhubuti



Sure: AL-QALAM 

Vers : 46

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au unawaomba ujira, na wao wanaelemewa na gharama hiyo?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 47

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanayo (elimu) ya ghaibu, basi wao wanaandika?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 48

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ

Basi subiri hukumu ya mola wako, wala usiwe kama sahibu wa nyangumi, alipomwita (Mola wake) na hali yeye alikuwa mwenye huzuni nyingi (Amebanwa na Dhiki)



Sure: AL-QALAM 

Vers : 49

لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa



Sure: AL-QALAM 

Vers : 50

فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Lakini mola wake alimchagua na akamfanya kuwa ni miongoni mwa watu wema



Sure: AL-QALAM 

Vers : 51

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ

Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni



Sure: AL-QALAM 

Vers : 52

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote