Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 45

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ

Hakika walikua kabla ya hapo kwenye maisha ya neema na anasa



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 46

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ

Na walikuwa wakishikilia kufanya dhambi kubwa mno



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 47

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Na walikuwa wakisema: Je, hivi tutakapo kufa na tukawa udongo na mifupa, je hivi sisi hakika tutafufuliwa?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 48

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Au na wazee wetu wa mwanzo?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 49

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ

Sema; Hakika wa mwanzo na wa mwisho,



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 50

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Hakika watakusanywa kwenye wakati na siku maalumu



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 57

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ

Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 58

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ

Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 59

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?



Sure: AL-WAAQIA’H 

Vers : 60

نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ

Sisi tumekadiria kati yenu umauti na haikua sisi wenye kukimbiwa