Sure: HUUD 

Vers : 31

وَلَآ أَقُولُ لَكُمۡ عِندِي خَزَآئِنُ ٱللَّهِ وَلَآ أَعۡلَمُ ٱلۡغَيۡبَ وَلَآ أَقُولُ إِنِّي مَلَكٞ وَلَآ أَقُولُ لِلَّذِينَ تَزۡدَرِيٓ أَعۡيُنُكُمۡ لَن يُؤۡتِيَهُمُ ٱللَّهُ خَيۡرًاۖ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا فِيٓ أَنفُسِهِمۡ إِنِّيٓ إِذٗا لَّمِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na sisemi kuwa nina hazina za Allah na siwaambii kuwa mimi ninajua ghaibu na siwaambii (katika daawa yangu) kwamba mimi ni Malaika, na sisemi kuhusu wale yanawadharau macho yenu kuwa Allah hatawapa kheri yeyote. Allah ni Mjuzi zaidi wa yaliyo katika nafsi zao, (ikiwa nitayafanya hayo) kwa hakika kabisa nitakuwa miongoni mwa madhalimu



Sure: HUUD 

Vers : 32

قَالُواْ يَٰنُوحُ قَدۡ جَٰدَلۡتَنَا فَأَكۡثَرۡتَ جِدَٰلَنَا فَأۡتِنَا بِمَا تَعِدُنَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Walisema ewe Nuhu kwa hakika umejadiliana nasisi na umezidisha mijadala yako kwetu, basi tuletee kile unachotukamia nacho kama kweli ni katika wasemao kweli



Sure: HUUD 

Vers : 33

قَالَ إِنَّمَا يَأۡتِيكُم بِهِ ٱللَّهُ إِن شَآءَ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ

(Nuhu) akasema: Hakika sivingine Allah ndiye atawaleteeni akitaka wala nyinyi si wenye kumshinda



Sure: HUUD 

Vers : 34

وَلَا يَنفَعُكُمۡ نُصۡحِيٓ إِنۡ أَرَدتُّ أَنۡ أَنصَحَ لَكُمۡ إِن كَانَ ٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يُغۡوِيَكُمۡۚ هُوَ رَبُّكُمۡ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Nasaha zangu hazitawafaa (chochote) iwapo Allah akitaka awaache mpotee, yeye tu ndiye Mola wenu mlezi na kwake tu mtarejeshwa



Sure: HUUD 

Vers : 35

أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ إِنِ ٱفۡتَرَيۡتُهُۥ فَعَلَيَّ إِجۡرَامِي وَأَنَا۠ بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُجۡرِمُونَ

Au wanasema kuwa (kauli hii Nuhu) ameizusha tu, sema kama itakuwa nimeizusha basi kosa la uzushi ni langu peke yangu, na mimi niko mbali na yote mnayoyafanya



Sure: HUUD 

Vers : 36

وَأُوحِيَ إِلَىٰ نُوحٍ أَنَّهُۥ لَن يُؤۡمِنَ مِن قَوۡمِكَ إِلَّا مَن قَدۡ ءَامَنَ فَلَا تَبۡتَئِسۡ بِمَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ

Na akapewa wah-yi Nuhu ya kwamba hataamini katika watu wako yeyote ispokuwa tu yule aliyekwisha amini, hivyo basi usihuzunike kutokana na yale waliyokuwa wakiyatenda



Sure: HUUD 

Vers : 37

وَٱصۡنَعِ ٱلۡفُلۡكَ بِأَعۡيُنِنَا وَوَحۡيِنَا وَلَا تُخَٰطِبۡنِي فِي ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ إِنَّهُم مُّغۡرَقُونَ

Na unda jahazi mbele ya macho yetu na na wah-yi wetu. Na usiniambie lolote kuhusu wale waliodhulumu (nafsi zao), kwa yakini wao watazamishwa



Sure: HUUD 

Vers : 38

وَيَصۡنَعُ ٱلۡفُلۡكَ وَكُلَّمَا مَرَّ عَلَيۡهِ مَلَأٞ مِّن قَوۡمِهِۦ سَخِرُواْ مِنۡهُۚ قَالَ إِن تَسۡخَرُواْ مِنَّا فَإِنَّا نَسۡخَرُ مِنكُمۡ كَمَا تَسۡخَرُونَ

Na (Nuhu alianza) kuuunda jahazi; Na wakubwa wa watu wake kila walipopita pale walimdhihaki, (Nuhu) akasema: Ijapokuwa mnatudhihaki, hakika na sisi tutawadhihaki kama mnavyo-tudhihaki



Sure: HUUD 

Vers : 39

فَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ مَن يَأۡتِيهِ عَذَابٞ يُخۡزِيهِ وَيَحِلُّ عَلَيۡهِ عَذَابٞ مُّقِيمٌ

Basi mtajua ni nani itakayemfika adhabu ya kumfedhehesha na itamteremkia adhabu yenye kudumu



Sure: HUUD 

Vers : 40

حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَمۡرُنَا وَفَارَ ٱلتَّنُّورُ قُلۡنَا ٱحۡمِلۡ فِيهَا مِن كُلّٖ زَوۡجَيۡنِ ٱثۡنَيۡنِ وَأَهۡلَكَ إِلَّا مَن سَبَقَ عَلَيۡهِ ٱلۡقَوۡلُ وَمَنۡ ءَامَنَۚ وَمَآ ءَامَنَ مَعَهُۥٓ إِلَّا قَلِيلٞ

Hadi ilipofika amri yetu (ya kuwaangamiza) na chemchem ya maji ikabubujika, tukamwambia (Nuhu): pakia humo (katika jahazi) kila mnyama pea moja jike na dume, na (pakia) ahali zako ispokuwa yule ambaye imepita hukumu na walioamini. Na hawakuamini pamoja na Nuhu ispokuwa wachache tu



Sure: HUUD 

Vers : 41

۞وَقَالَ ٱرۡكَبُواْ فِيهَا بِسۡمِ ٱللَّهِ مَجۡرٜىٰهَا وَمُرۡسَىٰهَآۚ إِنَّ رَبِّي لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na akasema: Pandeni humo, kwa jina la Allah (Bismillah arrahmani arrahim) iwe kwenda kwake na kusimama kwake. Hakika Mola wangu mlezi ni msamehevu sana mwenye kurehemu



Sure: HUUD 

Vers : 42

وَهِيَ تَجۡرِي بِهِمۡ فِي مَوۡجٖ كَٱلۡجِبَالِ وَنَادَىٰ نُوحٌ ٱبۡنَهُۥ وَكَانَ فِي مَعۡزِلٖ يَٰبُنَيَّ ٱرۡكَب مَّعَنَا وَلَا تَكُن مَّعَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Nayo ili kwenda nao katika mawimbi mfano wa milima. Na Nuhu alimwita mwanawe aliyekuwa mbali: ewe mwanangu panda pamoja na sisi na usiwe pamoja na makafiri



Sure: HUUD 

Vers : 43

قَالَ سَـَٔاوِيٓ إِلَىٰ جَبَلٖ يَعۡصِمُنِي مِنَ ٱلۡمَآءِۚ قَالَ لَا عَاصِمَ ٱلۡيَوۡمَ مِنۡ أَمۡرِ ٱللَّهِ إِلَّا مَن رَّحِمَۚ وَحَالَ بَيۡنَهُمَا ٱلۡمَوۡجُ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُغۡرَقِينَ

(Mtoto yule alimjibu baba yake): Nitakimbilia katika Jabali litanikinga na maji, (Nuhu) akasema: Leo hakuna wa kuikinga amri ya Allah ispokuwa yule tu (Allah) atamrehemu, na wimbi likaingia kati yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa



Sure: HUUD 

Vers : 44

وَقِيلَ يَـٰٓأَرۡضُ ٱبۡلَعِي مَآءَكِ وَيَٰسَمَآءُ أَقۡلِعِي وَغِيضَ ٱلۡمَآءُ وَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ وَٱسۡتَوَتۡ عَلَى ٱلۡجُودِيِّۖ وَقِيلَ بُعۡدٗا لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na pakasemwa: Ewe ardhi! Meza maji yako, na ewe mbingu jizuie, na maji yakazama, na jambo likamalizwa (kwa kuangamizwa watu wa Nuhu), na jahazi likasimama juu ya mlima judy. Na pakasemwa: Kuangamia kuwe kwa watu madhalimu



Sure: HUUD 

Vers : 45

وَنَادَىٰ نُوحٞ رَّبَّهُۥ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ٱبۡنِي مِنۡ أَهۡلِي وَإِنَّ وَعۡدَكَ ٱلۡحَقُّ وَأَنتَ أَحۡكَمُ ٱلۡحَٰكِمِينَ

Na (hapo) Nuhu akamwita Mola wake mlezi akasema: Ee Mola wangu mlezi!(umeniahidi utaniokoa mimi na watu wangu), Hakika mwanangu ni katika watu wangu, na hakika ahadi yako ni haki (huendi kinyume na uliloahidi), nawe ni Hakimu uliye zaidi ya Mahakimu (Muadilifu wao)



Sure: HUUD 

Vers : 46

قَالَ يَٰنُوحُ إِنَّهُۥ لَيۡسَ مِنۡ أَهۡلِكَۖ إِنَّهُۥ عَمَلٌ غَيۡرُ صَٰلِحٖۖ فَلَا تَسۡـَٔلۡنِ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۖ إِنِّيٓ أَعِظُكَ أَن تَكُونَ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

(Allah) akasema: Ewe Nuhu, hakika huyo si miongoni mwa watu wako (niliokuahidi kuwaokoa kwa sababu ya ukafiri wake); hakika ana matendo yasio mazuri. Basi usiniombe mambo usiyoyajua undani wake. Hakika mimi nakuwaidhi usije ukawa miongoni mwa wajinga



Sure: HUUD 

Vers : 47

قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَعُوذُ بِكَ أَنۡ أَسۡـَٔلَكَ مَا لَيۡسَ لِي بِهِۦ عِلۡمٞۖ وَإِلَّا تَغۡفِرۡ لِي وَتَرۡحَمۡنِيٓ أَكُن مِّنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

(Nuhu) akasema: Ee Mola wangu, mlezi hakika ninajikinga kwako kukuomba jambo nisilolijua undani wake; Na endapo hutanisamehe na kunirehemu, nitakuwa miongoni mwa waliopata hasara



Sure: HUUD 

Vers : 48

قِيلَ يَٰنُوحُ ٱهۡبِطۡ بِسَلَٰمٖ مِّنَّا وَبَرَكَٰتٍ عَلَيۡكَ وَعَلَىٰٓ أُمَمٖ مِّمَّن مَّعَكَۚ وَأُمَمٞ سَنُمَتِّعُهُمۡ ثُمَّ يَمَسُّهُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Pakasemwa: ewe Nuhu, teremka kwa salama (amani) itokayo kwetu, na baraka nyingi ziwe kwako na kwa watu walio pamoja nawe. Na hivi punde zitakuwepo kaumu nyingi za watu waovu tutawapa starehe, kisha itawashika kutoka kwetu adhabu iumizayo mno



Sure: HUUD 

Vers : 49

تِلۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهَآ إِلَيۡكَۖ مَا كُنتَ تَعۡلَمُهَآ أَنتَ وَلَا قَوۡمُكَ مِن قَبۡلِ هَٰذَاۖ فَٱصۡبِرۡۖ إِنَّ ٱلۡعَٰقِبَةَ لِلۡمُتَّقِينَ

Hizo ni sehemu tu ya habari za ghaibu tunakufunulia. Hukuwa unazijua kabla ya hapa, sio wewe wala watu wako, Basi subiri, hakika mwisho (mwema) ni kwa wamchao Allah



Sure: HUUD 

Vers : 50

وَإِلَىٰ عَادٍ أَخَاهُمۡ هُودٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۖ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا مُفۡتَرُونَ

Na (tulimpeleka kwa kabila la) Aadi ndugu yao Hudi. Akawaambia: Enyi watu wangu! Mwabuduni Allah; Hamna nyinyi Mungu mwingine zaidi yake. Na nyinyi hakuna mnachoabudu ispokuwa wazushi (waongo) tu



Sure: HUUD 

Vers : 51

يَٰقَوۡمِ لَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ أَجۡرًاۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱلَّذِي فَطَرَنِيٓۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Enyi watu wangu, siwaombeni ujira wowote (katika daawa yangu kwenu) hakika sivingine ujira wangu unatoka kwa yule tu aliyeniumba: hivi basi hamfahamu?



Sure: HUUD 

Vers : 52

وَيَٰقَوۡمِ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِ يُرۡسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡكُم مِّدۡرَارٗا وَيَزِدۡكُمۡ قُوَّةً إِلَىٰ قُوَّتِكُمۡ وَلَا تَتَوَلَّوۡاْ مُجۡرِمِينَ

Na enyi watu wangu! Ombeni msamaha kwa Mola wenu, kisha rudini kwake, atayatuma mawingu yatakayotiririsha kwenu mvua, na atawazidishieni nguvu kuongezea nguvu zenu. Wala msigeuke mkawa Waovu



Sure: HUUD 

Vers : 53

قَالُواْ يَٰهُودُ مَا جِئۡتَنَا بِبَيِّنَةٖ وَمَا نَحۡنُ بِتَارِكِيٓ ءَالِهَتِنَا عَن قَوۡلِكَ وَمَا نَحۡنُ لَكَ بِمُؤۡمِنِينَ

Wakasema: Ewe Hudi! Hujatujia na dalili yoyote (itakayotubainishia ukweli wa madai yako), na sisi hatuwezi kuiacha Miungu yetu kwa kauli yako tu, na sisi kwako si wenye kukuamini



Sure: HUUD 

Vers : 54

إِن نَّقُولُ إِلَّا ٱعۡتَرَىٰكَ بَعۡضُ ءَالِهَتِنَا بِسُوٓءٖۗ قَالَ إِنِّيٓ أُشۡهِدُ ٱللَّهَ وَٱشۡهَدُوٓاْ أَنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ

Hatuna cha kusema ispokuwa baadhi ya Miungu yetu imekutia balaa (uwendawazimu). (Hudi) akasema: Hakika mimi namshuhudisha Allah, na shuhudieni kwamba mimi niko mbali na vyote mnavyovishirikisha na (Allah)



Sure: HUUD 

Vers : 55

مِن دُونِهِۦۖ فَكِيدُونِي جَمِيعٗا ثُمَّ لَا تُنظِرُونِ

Kinyume chake. Basi nyote nifanyieni vitimbi kisha msinipe muhula (muda wowote wakunisubiria)



Sure: HUUD 

Vers : 56

إِنِّي تَوَكَّلۡتُ عَلَى ٱللَّهِ رَبِّي وَرَبِّكُمۚ مَّا مِن دَآبَّةٍ إِلَّا هُوَ ءَاخِذُۢ بِنَاصِيَتِهَآۚ إِنَّ رَبِّي عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Hakika mimi nimemtegemea Allah, Mola wangu mlezi na Mola wenu mlezi. Hakuna mnyama (kiumbe) yeyote ispokuwa yeye (Allah) amezishika nywele zake za utosi. Bila shaka Mola wangu mlezi yupo katika njia iliyonyooka



Sure: HUUD 

Vers : 57

فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقَدۡ أَبۡلَغۡتُكُم مَّآ أُرۡسِلۡتُ بِهِۦٓ إِلَيۡكُمۡۚ وَيَسۡتَخۡلِفُ رَبِّي قَوۡمًا غَيۡرَكُمۡ وَلَا تَضُرُّونَهُۥ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ رَبِّي عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَفِيظٞ

Na kama mtakengeuka, basi kwa hakika nimeshawafikishia kile nilichotumwa kwenu, na Mola wangu mlezi atawaleta watu wengine baada yenu, na nyinyi hamtamdhuru Yeye chochote. Hakika Mola wangu mlezi ni mwenye kukihifadhi kila kitu



Sure: HUUD 

Vers : 58

وَلَمَّا جَآءَ أَمۡرُنَا نَجَّيۡنَا هُودٗا وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ بِرَحۡمَةٖ مِّنَّا وَنَجَّيۡنَٰهُم مِّنۡ عَذَابٍ غَلِيظٖ

Na ilipofika amri yetu, tulimuokoa Hudi na wale walioamini pamoja naye kwa rehema kutoka kwetu. Na tukawaokoa katika adhabu ngumu



Sure: HUUD 

Vers : 59

وَتِلۡكَ عَادٞۖ جَحَدُواْ بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ وَعَصَوۡاْ رُسُلَهُۥ وَٱتَّبَعُوٓاْ أَمۡرَ كُلِّ جَبَّارٍ عَنِيدٖ

Na (zile ni athari za kabila la) Aaadi. Walikanusha Aya za Mola wao mlezi, na wakamuasi Mtume wake (Huud), na wakafuata amri za kila aliye hodari sana mkaidi



Sure: HUUD 

Vers : 60

وَأُتۡبِعُواْ فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا لَعۡنَةٗ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ أَلَآ إِنَّ عَادٗا كَفَرُواْ رَبَّهُمۡۗ أَلَا بُعۡدٗا لِّعَادٖ قَوۡمِ هُودٖ

Na wakafuatiliziwa laana hapa duniani na Siku ya Kiyama. Eleweni! Hakika (watu) Aadi wamemkufuru Mola wao mlezi. Eleweni! Maangamizi yawafike (kabila la) Aadi, watu wa Huud