السورة: AL-BURUJI 

الآية : 4

قُتِلَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأُخۡدُودِ

Wameangamizwa watu wa mahandaki



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 5

ٱلنَّارِ ذَاتِ ٱلۡوَقُودِ

Yenye moto wenye kuni nyingi,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 6

إِذۡ هُمۡ عَلَيۡهَا قُعُودٞ

Walipo kuwa wamekaa hapo,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 7

وَهُمۡ عَلَىٰ مَا يَفۡعَلُونَ بِٱلۡمُؤۡمِنِينَ شُهُودٞ

Na wao ni mashahidi wa yale waliyo kuwa wakiwafanyia Waumini



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 8

وَمَا نَقَمُواْ مِنۡهُمۡ إِلَّآ أَن يُؤۡمِنُواْ بِٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَمِيدِ

Nao hawakuona baya lolote kwao ila kuwa wakimuamini Allah, Mwenye nguvu, Msifiwa,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 9

ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Ambaye anao ufalme wa mbingu na ardhi; na Allah ni shaahidi wa kila kitu



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 12

إِنَّ بَطۡشَ رَبِّكَ لَشَدِيدٌ

Hakika kutesa kwa Mola wako Mlezi ni kukali



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 13

إِنَّهُۥ هُوَ يُبۡدِئُ وَيُعِيدُ

Yeye ndiye anaye anzisha na ndiye anaye rejesha tena,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 14

وَهُوَ ٱلۡغَفُورُ ٱلۡوَدُودُ

Naye ni Mwenye kusamehe, Mwenye mapenzi,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 15

ذُو ٱلۡعَرۡشِ ٱلۡمَجِيدُ

Mwenye Kiti cha Enzi,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 16

فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Atendaye ayatakayo



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 17

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡجُنُودِ

Je! Zimekufikia khabari za majeshi?



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 18

فِرۡعَوۡنَ وَثَمُودَ

Ya Firauni na Thamudi?



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 19

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي تَكۡذِيبٖ

Lakini walio kufuru wamo katika kukadhibisha



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 20

وَٱللَّهُ مِن وَرَآئِهِم مُّحِيطُۢ

Na Allah nyuma yao amewazunguka



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 21

بَلۡ هُوَ قُرۡءَانٞ مَّجِيدٞ

Bali hii ni Qur’ani tukufu



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 22

فِي لَوۡحٖ مَّحۡفُوظِۭ

Katika Ubao Ulio Hifadhiwa



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 1

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 2

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinachokuja usiku?



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 3

ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ

Ni Nyota yenye mwanga mkali



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 4

إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 5

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ

Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 6

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 7

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 8

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ

Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 9

يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ

Siku zitakapo dhihirishwa siri



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 10

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi



السورة: ATTAARIQ 

الآية : 11

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!