السورة: ANNAJMI 

الآية : 42

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Na hakika kwa bwana wako ndio marejeo



السورة: ANNAJMI 

الآية : 43

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Anayesababisha kwa Mtu kicheko (furaha) na kilio



السورة: ANNAJMI 

الآية : 44

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا

Na hakika yeye ndiye anafisha na ndiye anayehuisha



السورة: ANNAJMI 

الآية : 45

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ

Na hakika yeye ameumba aina mbili ya viumbe Dume Na Jike



السورة: ANNAJMI 

الآية : 46

مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ

Kutokana na tone la manii linapomiminwa



السورة: ANNAJMI 

الآية : 47

وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ

Na kwamba ni juu Yake uanzishaji mwengine (kufufua)



السورة: ANNAJMI 

الآية : 48

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Atoshelezaye na Akinaishaye



السورة: ANNAJMI 

الآية : 49

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye Mola wa nyota ya Ash-Shi’-raa (inayoabudiwa).[1]


1- - Ash-Shi’-raa:- Hii ni Nyota maarufu, na Allah ameihusisha kuitaja hapa, ijapokuwa yeye ni Mola wa kila kitu kwasababu hii Nyota ni katika zilizokuwa zikiabudiwa katika zama za Kijaahiliyya, kwahiyo Allah akabainisha kila chochote wanacho kiabudu Washirikina basi hicho kimeumbwa na Allah, na hakistahiki kuabudiwa.


السورة: ANNAJMI 

الآية : 50

وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Aliyeangamiza kina ‘Aad Mwanzo



السورة: ANNAJMI 

الآية : 51

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Watu wa Thamuwd kisha Hakuwabakisha



السورة: ANNAJMI 

الآية : 52

وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ

Na Watu wa Nuwh hapo kabla, hakika wao walikuwa madhalimu zaidi na wapindukaji mipaka zaidi wa kuasi



السورة: ANNAJMI 

الآية : 53

وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ

Na miji iliyopinduliwa ni yeye Allah aliyeipindulia mbali



السورة: ANNAJMI 

الآية : 54

فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Na ikawafunika ambacho kimewafunika



السورة: ANNAJMI 

الآية : 55

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Basi neema gani za Bwana wako unazitilia shaka?



السورة: ANNAJMI 

الآية : 56

هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ

Huyu (Mtume þ) ni muonyaji miongoni mwa waonyaji wa awali



السورة: ANNAJMI 

الآية : 57

أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ

Kimekaribia kinachokaribia



السورة: ANNAJMI 

الآية : 58

لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Hakuna asiyekuwa Allah mwenye uwezo wa kukibainisha



السورة: ANNAJMI 

الآية : 59

أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ

Je, mnastaajabu kwa Mazungumzo haya (ya Qur-aan)?



السورة: ANNAJMI 

الآية : 60

وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ

Na mnacheka na wala hamlii?



السورة: ANNAJMI 

الآية : 61

وَأَنتُمۡ سَٰمِدُونَ

Na hali nyinyi mnaghafilika, mnadharau na kushughulika na anasa?



السورة: ANNAJMI 

الآية : 62

فَٱسۡجُدُواْۤ لِلَّهِۤ وَٱعۡبُدُواْ۩

Basi msujudieni Allah na mwabuduni Yeye tu



السورة: AL-QAMAR

الآية : 1

ٱقۡتَرَبَتِ ٱلسَّاعَةُ وَٱنشَقَّ ٱلۡقَمَرُ

Kimekaribia Kiyama na mwezi umepasuka



السورة: AL-QAMAR

الآية : 2

وَإِن يَرَوۡاْ ءَايَةٗ يُعۡرِضُواْ وَيَقُولُواْ سِحۡرٞ مُّسۡتَمِرّٞ

Na (Makafiri kila) wanapoona Aya yoyote (ishara/muujiza) wanakengeuka na kusema: (Huu) Ni uchawi endelevu



السورة: AL-QAMAR

الآية : 3

وَكَذَّبُواْ وَٱتَّبَعُوٓاْ أَهۡوَآءَهُمۡۚ وَكُلُّ أَمۡرٖ مُّسۡتَقِرّٞ

Na wamekadhibisha (haki) na wamefuata utashi wa nafsi zao. Na kila jambo (la kheri au la shari) litatulia (mahali pake. Watu wema watalipwa wema na watu wabaya watalipwa ubaya)



السورة: AL-QAMAR

الآية : 4

وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّنَ ٱلۡأَنۢبَآءِ مَا فِيهِ مُزۡدَجَرٌ

Na kwa yakini kabisa, katika habari muhimu, imekwishawajia habari ambayo ndani yake mna makemeo makali



السورة: AL-QAMAR

الآية : 5

حِكۡمَةُۢ بَٰلِغَةٞۖ فَمَا تُغۡنِ ٱلنُّذُرُ

Ni hekima ya kiwango cha juu kabisa, lakini maonyo (wanayopewa) hayasaidii kitu



السورة: AL-QAMAR

الآية : 6

فَتَوَلَّ عَنۡهُمۡۘ يَوۡمَ يَدۡعُ ٱلدَّاعِ إِلَىٰ شَيۡءٖ نُّكُرٍ

Basi wapuuze (na waache waingoje) siku (ya Kiyama ambapo) mnadi (mtangazaji) atanadi (atatangaza ili watu waende) kwenye jambo la kutisha sana



السورة: AL-QAMAR

الآية : 7

خُشَّعًا أَبۡصَٰرُهُمۡ يَخۡرُجُونَ مِنَ ٱلۡأَجۡدَاثِ كَأَنَّهُمۡ جَرَادٞ مُّنتَشِرٞ

Macho yao yakiwa dhalili, watatoka katika makaburi kama kwamba wao ni nzige waliosambaa



السورة: AL-QAMAR

الآية : 8

مُّهۡطِعِينَ إِلَى ٱلدَّاعِۖ يَقُولُ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا يَوۡمٌ عَسِرٞ

Wenye kukimbia mbio huku wakibinua shingo zao wakielekea kwa muitaji; makafiri watasema: Hii ni siku ngumu!



السورة: AL-QAMAR

الآية : 9

۞كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ فَكَذَّبُواْ عَبۡدَنَا وَقَالُواْ مَجۡنُونٞ وَٱزۡدُجِرَ

Walikadhibisha kabla yao watu wa nuhu na wakamkadhibisha mja wetu wakasema mwendawazimu na akafanyiwa maudhi