فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا
Basi pigana katika njia ya Allah. Hukalifishwi isipokuwa nafsi yako tu, na wahamasishe waumini, huenda Allah akayazuia mashambulizi ya waliokufuru. Na Allah ni Mkali sana wa kushambulia na Mkali wa kuadhibu
مَّن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةً حَسَنَةٗ يَكُن لَّهُۥ نَصِيبٞ مِّنۡهَاۖ وَمَن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةٗ سَيِّئَةٗ يَكُن لَّهُۥ كِفۡلٞ مِّنۡهَاۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقِيتٗا
Yeyote atakayeombea maombezi mazuri (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo jema) atapata fungu katika jambo zuri hilo, na yeyote atakayeombea maombezi maovu (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo ovu) atapata fungu katika jambo ovu hilo. Na Allahni Mwenye uweza na ujuzi juu ya kila kitu
وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٖ فَحَيُّواْ بِأَحۡسَنَ مِنۡهَآ أَوۡ رُدُّوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَسِيبًا
Na mnapoamkiwa maamkizi yoyote yale, basi nanyi itikieni kwa maamkizi mazuri zaidi kuliko hayo au rejesheni hayo hayo. Hakika, Allah ni Mwenye kuhesabu kila kitu
ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۗ وَمَنۡ أَصۡدَقُ مِنَ ٱللَّهِ حَدِيثٗا
Allah, hakuna mwenye haki ya kuabudiwa ispokuwa yeye tu. Kwa yakini kabisa, atakukusanyeni katika Siku ya Kiyama isiyokuwa na shaka yoyote. Na ni nani mkweli sana wa maneno kuliko Allah?
۞فَمَا لَكُمۡ فِي ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِئَتَيۡنِ وَٱللَّهُ أَرۡكَسَهُم بِمَا كَسَبُوٓاْۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهۡدُواْ مَنۡ أَضَلَّ ٱللَّهُۖ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا
Basi mna nini nyinyi mmegawanyika makundi mawili kuhusu wanafiki, na ilhali Allah amewageuza (na kurudi kwenye ukafiri) kwasababu ya yale waliyo-yachuma? Hivi mnataka kuwaongoa ambao Allah amewapoteza? Na yeyote ambaye Allah amempoteza hutapata njia (ya kumuongoza)
وَدُّواْ لَوۡ تَكۡفُرُونَ كَمَا كَفَرُواْ فَتَكُونُونَ سَوَآءٗۖ فَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ أَوۡلِيَآءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ وَجَدتُّمُوهُمۡۖ وَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرًا
Wametamani lau mngekufuru kama walivyokufuru wao ili muwe sawa. Basi msiwafanye marafiki wa karibu miongoni mwao mpaka wahame kwa ajili ya dini ya Allah. Basi kama wakikengeuka washikeni (mateka) na waueni popote mtakapowakuta, na msifanye miongoni mwao rafiki wa karibu wala msaidizi
إِلَّا ٱلَّذِينَ يَصِلُونَ إِلَىٰ قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٌ أَوۡ جَآءُوكُمۡ حَصِرَتۡ صُدُورُهُمۡ أَن يُقَٰتِلُوكُمۡ أَوۡ يُقَٰتِلُواْ قَوۡمَهُمۡۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَسَلَّطَهُمۡ عَلَيۡكُمۡ فَلَقَٰتَلُوكُمۡۚ فَإِنِ ٱعۡتَزَلُوكُمۡ فَلَمۡ يُقَٰتِلُوكُمۡ وَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ فَمَا جَعَلَ ٱللَّهُ لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سَبِيلٗا
Isipokuwa wale ambao wana-husiana na watu ambao kati yenu na wao kuna mkataba au wamekujieni huku nyoyo zao zikiona tabu kupigana nanyi au kupigana na watu wao. Na Allah angetaka angeliwapa nguvu dhidi yenu wakakupigeni. Basi wakiachana nanyi na wasipigane nanyi na wakakuleteeni amani (wakakutangazieni amani), basi Allah hakukupeni njia (ruhusa ya kupiganana nao)
سَتَجِدُونَ ءَاخَرِينَ يُرِيدُونَ أَن يَأۡمَنُوكُمۡ وَيَأۡمَنُواْ قَوۡمَهُمۡ كُلَّ مَا رُدُّوٓاْ إِلَى ٱلۡفِتۡنَةِ أُرۡكِسُواْ فِيهَاۚ فَإِن لَّمۡ يَعۡتَزِلُوكُمۡ وَيُلۡقُوٓاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ وَيَكُفُّوٓاْ أَيۡدِيَهُمۡ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ ثَقِفۡتُمُوهُمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكُمۡ جَعَلۡنَا لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٗا مُّبِينٗا
Mtawakuta wengine wanataka kukaa nanyi kwa amani (kwa kuonesha kuwa nao wameamini) na kukaa kwa amani na watu wao (kwa kuwaonesha kuwa bado wao ni makafiri). Kila wanaporudishwa kwenye fitina (ukafiri) wanaporomoshwa (wanaburuzwa na kurudi kwa kasi kubwa) kwenye ukafiri huo. Basi kama hawakukuacheni na hawakukutangazieni amani na hawakuizuia mikono yao (wakaacha kukupigeni), basi wakamateni na waueni popote mtakapowakuta, na hao tumekupeni hoja ya wazi (ya kuwashambulia, kuwapiga, kuwaua na kuwakamata mateka)
وَمَا كَانَ لِمُؤۡمِنٍ أَن يَقۡتُلَ مُؤۡمِنًا إِلَّا خَطَـٔٗاۚ وَمَن قَتَلَ مُؤۡمِنًا خَطَـٔٗا فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖ وَدِيَةٞ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَصَّدَّقُواْۚ فَإِن كَانَ مِن قَوۡمٍ عَدُوّٖ لَّكُمۡ وَهُوَ مُؤۡمِنٞ فَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖۖ وَإِن كَانَ مِن قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٞ فَدِيَةٞ مُّسَلَّمَةٌ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ وَتَحۡرِيرُ رَقَبَةٖ مُّؤۡمِنَةٖۖ فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ شَهۡرَيۡنِ مُتَتَابِعَيۡنِ تَوۡبَةٗ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Na haiwi kwa Muumini (Muis-lamu) yeyote kumuua Muumini (mwingine) isipokuwa tu kwa kukosea. Na yeyote aliyemuua Muumini kwa kukosea, basi (adhabu yake) ni kuacha huru mtumwa Muumini (Muislamu) na Dia (fidia)[1] itakayokabidhiwa kwa ndugu zake (warithi wake), isipokuwa tu kama (ndugu hao) watafanya Dia hiyo sadaka (kwa kusamehe). Na kama (aliyeuliwa) ni kutoka kwa watu maadui wenu (makafiri), na yeye (marehemu) ni Mumini (Muislamu), basi (adhabu ya muuaji) ni kuacha huru mtumwa Muislamu tu.[2] Na kama (aliyeuliwa) ni kutoka kwa watu (makafiri) ambao kuna mkataba kati yenu na wao (wa kuishi kwa amani) basi (adhabu ya muuaji) ni Dia (fidia) itakayokabidhiwa kwa ndugu zake na kuacha huru mtumwa Muislamu[3]. Basi ambaye hakupata (mtumwa wa kumuacha huru adhabu yake) ni kufunga miezi miwili mfululizo. (Hii) Ndio toba kutoka kwa Allah, na Allah ni Mjuzi sana, Mwenye hekima nyingi
1- - Dia au fidia ya kuua ni ngamia mia moja (100) kama alivyoainisha Mtume, Allah amshushie rehema na amani, katika waraka alioutuma kwa watu wa Yemen. Ameyanukuu haya Imamu Malik katika kitabu chake cha Muwattwai.
2- - Hapa aya inamaanisha kuwa aliyeuliwa ni Muislamu lakini ndugu zake ni makafiri. Hivyo hakuna fidia itakayotolewa isipokuwa tu kuacha huru Mtumwa Muislamu. Kwa nini fidia hapa haipo? Ni kwa sababu fidia kama itatolewa itakwenda kwa makafiri wenye uadui na Uislamu. Kuwapa fidia makafiri maadui ni kuwapa nguvu dhidi ya Waislamu.
3- - Pamoja na kwamba ndugu wa Muislamu aliyeuliwa ni makafiri lakini hapa Uislamu unawapa fidia kwa sababu fidia hiyo haitarajiwi kutumika katika kuwadhuru Waislamu kwa sababu makafiri hawa wamo katika mkataba wa kuishi kwa amani. Hapa tunajifunza namna Uislamu unavyothamini amani na utulivu katika jamii. Ndugu wa marehemu kama ni makafiri wasioingia mkataba wa amani na Waislamu hawapewi Dia. Ama kama ni makafiri walioingia mkataba wa amani na Waislamu wanapewa Dia kwa kuzingatia amani.
وَمَن يَقۡتُلۡ مُؤۡمِنٗا مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآؤُهُۥ جَهَنَّمُ خَٰلِدٗا فِيهَا وَغَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَلَعَنَهُۥ وَأَعَدَّ لَهُۥ عَذَابًا عَظِيمٗا
Na yeyote anayemuua Muumini (Muislamu) kwa kukusudia basi malipo yake ni Jahanamu, ataishi humo milele na Allah amemghadhibikia na amemlaani na amemuandalia adhabu kubwa kabisa
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا ضَرَبۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَتَبَيَّنُواْ وَلَا تَقُولُواْ لِمَنۡ أَلۡقَىٰٓ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَٰمَ لَسۡتَ مُؤۡمِنٗا تَبۡتَغُونَ عَرَضَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا فَعِندَ ٱللَّهِ مَغَانِمُ كَثِيرَةٞۚ كَذَٰلِكَ كُنتُم مِّن قَبۡلُ فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمۡ فَتَبَيَّنُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا
Enyi mlioamini, mnaposafiri katika njia ya Allah (Jihadi), basi kuweni waangalifu. Na msimwambie yeyote aliyekusalimieni (kwa maamkizi ya Kiislamu[1]) kwamba: “Wewe sio Muumini”, kwa kutaka manufaa ya maisha ya dunia hii. Basi kwa Allah ziko ngawira (kheri) nyingi. Hivyo ndivyo mlivyo kuwa nyinyi zamani (kwa kutamka tu na Uislamu wenu ukakubalika), na Allah akakuneemesheni, basi zindukeni. Hakika Allah ni Mjuzi wa yote mnayoyatenda
1- - Waislamu, wanapokuwa vitani, wanakatazwa kumdhuru mtu ambaye ameonesha alama za kwamba ameukubali Uislamu, ikiwa ni pamoja na kutumia maamkizi ya Kiislamu yenye kuashiria amani.
لَّا يَسۡتَوِي ٱلۡقَٰعِدُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ غَيۡرُ أُوْلِي ٱلضَّرَرِ وَٱلۡمُجَٰهِدُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ فَضَّلَ ٱللَّهُ ٱلۡمُجَٰهِدِينَ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ عَلَى ٱلۡقَٰعِدِينَ دَرَجَةٗۚ وَكُلّٗا وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡحُسۡنَىٰۚ وَفَضَّلَ ٱللَّهُ ٱلۡمُجَٰهِدِينَ عَلَى ٱلۡقَٰعِدِينَ أَجۡرًا عَظِيمٗا
Waumini wasiokuwa na udhuru wowote waliokaa (kwa kuacha kwenda vitani) hawawi sawa na wale wanaopigana Jihadi katika njia ya Allah kwa mali zao na nafsi zao. Allah amewafanya bora zaidi kwa daraja wanaopigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao kuliko wanaokaa. Na wote Allah amewaahidi mazuri (Pepo)[1]. Na Allah amewafanya bora zaidi wanaopigana Jihadi kuliko wanaokaa kwa ujira mkubwa kabisa
1- - Kwa mujibu wa Aya hii ni kwamba, waumini walioshiriki Jihadi na ambao hawakushiriki wote Allah amewaahidi Pepo. Huu ni ushahidi kwamba, wale wanaodai kuwa Swahaba wengi waliritadi na kukufuru kwa kutoshiriki Jihadi isipokuwa wachache tu madai hayo ni ya uongo na itikadi yao hii sio sahihi.
دَرَجَٰتٖ مِّنۡهُ وَمَغۡفِرَةٗ وَرَحۡمَةٗۚ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمًا
Ni daraja nyingi kutoka kwake na msamaha na rehema. Na Allah amekuwa Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu
إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَفَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ ظَالِمِيٓ أَنفُسِهِمۡ قَالُواْ فِيمَ كُنتُمۡۖ قَالُواْ كُنَّا مُسۡتَضۡعَفِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ قَالُوٓاْ أَلَمۡ تَكُنۡ أَرۡضُ ٱللَّهِ وَٰسِعَةٗ فَتُهَاجِرُواْ فِيهَاۚ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرًا
Hakika, wale ambao Malaika wamewafisha (wamewatoa roho) ilhali wamezidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawauliza: Je, mlikuwa na nini nyinyi? Watasema: Tulikuwa wayonge katika ardhi (duniani). (Malaika) Watawaambia: Hivi Ardhi ya Allah haikuwa yenye wasaa mkahama humo? Basi hao makazi yao ni Jahanamu, na marejeo mabaya mno ni hayo.[1]
1- - Aya hii inawataka Waislamu kutoridhika na mazingira ambayo sio rafiki katika kutekeleza majukumu ya dini yao na pia mambo yao ya kimaendeleo. Wanatakiwa kupambana na ikishindikana wahame na kwenda eneo jingine lenye mazingira rafiki.
إِلَّا ٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلرِّجَالِ وَٱلنِّسَآءِ وَٱلۡوِلۡدَٰنِ لَا يَسۡتَطِيعُونَ حِيلَةٗ وَلَا يَهۡتَدُونَ سَبِيلٗا
Isipokuwa (wanaosameheka na dhambi hii ni) wale wanyonge ikiwa ni pamoja na wanaume na wanawake na watoto ambao hawawezi (kufanya) mbinu yoyote (ya kujihami) na hawajui njia (ya kukimbilia)[1]
1- - Kusameheka kwa mwanaume ni kwa sababu ya uzee, ugonjwa n.k. Kwa mwanamke ni kwa sababu ya jinsia yake, na kwa mtoto ni kwa sababu ya umri.
فَأُوْلَـٰٓئِكَ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَعۡفُوَ عَنۡهُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَفُوًّا غَفُورٗا
Basi hao huenda Allah akawasamehe, na Allah ni Msamehevu sana, Mwingi wa kufuta dhambi
۞وَمَن يُهَاجِرۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ يَجِدۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُرَٰغَمٗا كَثِيرٗا وَسَعَةٗۚ وَمَن يَخۡرُجۡ مِنۢ بَيۡتِهِۦ مُهَاجِرًا إِلَى ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ ثُمَّ يُدۡرِكۡهُ ٱلۡمَوۡتُ فَقَدۡ وَقَعَ أَجۡرُهُۥ عَلَى ٱللَّهِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na yeyote anayehama katika njia ya Allah atapata faida nyingi ardhini na ukunjufu. Na yeyote anayetoka nyumbani kwake akahama kwa ajili ya Allah na Mtume wake, kisha kifo kikamfika, hakika ujira wake umeshathibiti kwa Allah. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu
وَإِذَا ضَرَبۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَن تَقۡصُرُواْ مِنَ ٱلصَّلَوٰةِ إِنۡ خِفۡتُمۡ أَن يَفۡتِنَكُمُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْۚ إِنَّ ٱلۡكَٰفِرِينَ كَانُواْ لَكُمۡ عَدُوّٗا مُّبِينٗا
Na mnaposafiri ardhini[1], basi hakuna ubaya wowote kwenu kupunguza Swala[2] ikiwa mtahofia kupata mitihani ya makafiri (kwa kukudhuruni). Hakika makafiri wamekuwa maadui wa dhahiri kwenu
1- - Hapa imetajwa kusafiri ardhini kwa sababu sehemu kubwa ya usafiri kwa wakati Qur’ani inashuka ilikuwa kwa njia ya ardhini na majini. Ama ruhusa hii inahusu pia usafiri wa anga abao umeshamiri hivi sasa.
2- - Swala zinazokusudiwa kupunguzwa hapa ni zile zenye rakaa nne. Zinapunguzwa na kuswaliwa rakaa mbili. Swala hizo ni Adhuhuri, Alasiri na Isha.
وَإِذَا كُنتَ فِيهِمۡ فَأَقَمۡتَ لَهُمُ ٱلصَّلَوٰةَ فَلۡتَقُمۡ طَآئِفَةٞ مِّنۡهُم مَّعَكَ وَلۡيَأۡخُذُوٓاْ أَسۡلِحَتَهُمۡۖ فَإِذَا سَجَدُواْ فَلۡيَكُونُواْ مِن وَرَآئِكُمۡ وَلۡتَأۡتِ طَآئِفَةٌ أُخۡرَىٰ لَمۡ يُصَلُّواْ فَلۡيُصَلُّواْ مَعَكَ وَلۡيَأۡخُذُواْ حِذۡرَهُمۡ وَأَسۡلِحَتَهُمۡۗ وَدَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ تَغۡفُلُونَ عَنۡ أَسۡلِحَتِكُمۡ وَأَمۡتِعَتِكُمۡ فَيَمِيلُونَ عَلَيۡكُم مَّيۡلَةٗ وَٰحِدَةٗۚ وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ إِن كَانَ بِكُمۡ أَذٗى مِّن مَّطَرٍ أَوۡ كُنتُم مَّرۡضَىٰٓ أَن تَضَعُوٓاْ أَسۡلِحَتَكُمۡۖ وَخُذُواْ حِذۡرَكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ أَعَدَّ لِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٗا مُّهِينٗا
Na unapokuwa nao ukawa-simamishia Swala, basi lisimame kundi miongoni mwao pamoja nawe, na washike silaha zao. Wanaposujudu, (walioshika silaha) wawe nyuma yenu. Na (likimaliza kundi hili) lije kundi jingine ambalo halijaswali liswali pamoja na wewe na wachukue tahadhari zao na silaha zao. Waliokufuru wanapenda lau mngesahau silaha zenu na mizigo yenu ili wakushukieni (wakushambulieni kwa) shambulio moja tu (na kukumalizeni). Na hakuna ubaya wowote kwenu, kama mtakuwa katika hali ya udhia utokanao na mvua au mkiwa wagonjwa kutochukua silaha zenu. Na chukueni tahadhari zenu. Hakika Allah amewaandalia makafiri adhabu yenye kudhalilisha
فَإِذَا قَضَيۡتُمُ ٱلصَّلَوٰةَ فَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ قِيَٰمٗا وَقُعُودٗا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمۡۚ فَإِذَا ٱطۡمَأۡنَنتُمۡ فَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَۚ إِنَّ ٱلصَّلَوٰةَ كَانَتۡ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ كِتَٰبٗا مَّوۡقُوتٗا
Mmalizapo kuswali basi mtajeni Allah mkiwa mmesimama na mkiwa mmekaa na mkiwa mmejilaza ubavu. Mnapokuwa katika utulivu (amani), basi simamisheni Swala (kwa ukamilifu na bila ya kupunguza). Kwa hakika, Swala kwa Waislamu ni jambo liliofaradhishwa, lililowekewa wakati maaulumu
وَلَا تَهِنُواْ فِي ٱبۡتِغَآءِ ٱلۡقَوۡمِۖ إِن تَكُونُواْ تَأۡلَمُونَ فَإِنَّهُمۡ يَأۡلَمُونَ كَمَا تَأۡلَمُونَۖ وَتَرۡجُونَ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا يَرۡجُونَۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمًا
Na msiwe dhaifu katika kuwasaka jamaa (ambao ni maadui wenu). Ikiwa nyinyi mnaumia (katika mapambano) kwa hakika wao pia wanaumia kama mnavyoumia nyinyi, na nyinyi mnataraji kwa Allah kitu ambacho wao hawakitaraji, na Allah ni Mjuzi sana, Mwenye hekima nyingi
إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِتَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ بِمَآ أَرَىٰكَ ٱللَّهُۚ وَلَا تَكُن لِّلۡخَآئِنِينَ خَصِيمٗا
Hakika, sisi tumekuteremshia kitabu kwa haki ili uhukumu baina ya watu kwa kile ambacho Allah amekuonyesha (amekuelimisha). Na usiwe mtetezi wa wanaofanya khiana
وَٱسۡتَغۡفِرِ ٱللَّهَۖ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na muombe msamaha Allah. Hakika Allah ni Msamehevu sana, Mwenye kurehem
وَلَا تُجَٰدِلۡ عَنِ ٱلَّذِينَ يَخۡتَانُونَ أَنفُسَهُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ مَن كَانَ خَوَّانًا أَثِيمٗا
Na usiwatetee wale wanaozi-fanyia khiana nafsi zao (kwa kutenda dhambi na makosa mbali mbali). Hakika Allah hampendi (mtu) mwenye khiana, mwenye dhambi
يَسۡتَخۡفُونَ مِنَ ٱلنَّاسِ وَلَا يَسۡتَخۡفُونَ مِنَ ٱللَّهِ وَهُوَ مَعَهُمۡ إِذۡ يُبَيِّتُونَ مَا لَا يَرۡضَىٰ مِنَ ٱلۡقَوۡلِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ بِمَا يَعۡمَلُونَ مُحِيطًا
Wanajificha wasionekane na watu na wala hawamstahi Allah kuwaona (wanapofanya dhambi) ilhali yeye yuko pamoja nao wakati wanapopanga njama usiku za (kusema) kauli zisizoridhiwa (na Allah). Na Allah anayajua vilivyo yote wayafanyayo
هَـٰٓأَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ جَٰدَلۡتُمۡ عَنۡهُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا فَمَن يُجَٰدِلُ ٱللَّهَ عَنۡهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ أَم مَّن يَكُونُ عَلَيۡهِمۡ وَكِيلٗا
Ee! Nyinyi hawa mmewatetea katika maisha ya kidunia. Basi ni nani atakayejadiliana na Allah Siku ya Kiama akiwatetea au ni nani atakayekuwa wakili wao?
وَمَن يَعۡمَلۡ سُوٓءًا أَوۡ يَظۡلِمۡ نَفۡسَهُۥ ثُمَّ يَسۡتَغۡفِرِ ٱللَّهَ يَجِدِ ٱللَّهَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na yeyote mwenye kutenda baya au kudhulumu nafsi yake, kisha akamuomba msamaha Allah, atamkuta Allah ni Msamehevu sana, Mwenye kurehem
وَمَن يَكۡسِبۡ إِثۡمٗا فَإِنَّمَا يَكۡسِبُهُۥ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Na yeyote anayechuma dhambi, basi hakika anazichuma kwa (kuidhuru) nafsi yake. Na Allah ni Mjuzi mno, Mwenye hekima nyingi
وَمَن يَكۡسِبۡ خَطِيٓـَٔةً أَوۡ إِثۡمٗا ثُمَّ يَرۡمِ بِهِۦ بَرِيٓـٔٗا فَقَدِ ٱحۡتَمَلَ بُهۡتَٰنٗا وَإِثۡمٗا مُّبِينٗا
Na yeyote anayetenda kosa au dhambi kisha akamsingizia asiyekuwa na hatia, basi hakika amebeba uzushi na dhambi inayobainisha (uovu wake)
وَلَوۡلَا فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكَ وَرَحۡمَتُهُۥ لَهَمَّت طَّآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ أَن يُضِلُّوكَ وَمَا يُضِلُّونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡۖ وَمَا يَضُرُّونَكَ مِن شَيۡءٖۚ وَأَنزَلَ ٱللَّهُ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَعَلَّمَكَ مَا لَمۡ تَكُن تَعۡلَمُۚ وَكَانَ فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكَ عَظِيمٗا
Na lau kama si hisani ya Allah na rehema zake kwako basi kwa yakini kabisa kundi miongoni mwao lilikusudia kukupotosha. Na hawapotoshi ispokuwa nafsi zao tu na hawatakudhuru chochote. Na Allah amekuteremshia kitabu (Qur’an) na hekima, na amekufundisha uliyokuwa huyajui. Na hisani ya Allah kwako ni kubwa sana