السورة: AL-KAAFIRUUN 

الآية : 6

لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ

Nyinyi mna dini yenu, nami nina dini yangu



السورة: ANASRI 

الآية : 1

إِذَا جَآءَ نَصۡرُ ٱللَّهِ وَٱلۡفَتۡحُ

Itakapokuja nusra ya Allah na ushindi (ukombozi wa mji wa Makka)



السورة: ANASRI 

الآية : 2

وَرَأَيۡتَ ٱلنَّاسَ يَدۡخُلُونَ فِي دِينِ ٱللَّهِ أَفۡوَاجٗا

Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Allah kwa makundi



السورة: ANASRI 

الآية : 3

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا

Basi zitakase sifa za Mola wako Mlezi na muombe msamaha. Hakika, Yeye (Allah) amekuwa Mwenye kukubali sana toba. Sura imetoa utabiri wa kifo cha Mtume rehma na amani ziwe juu yake



السورة: AL-MASAD

الآية : 1

تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ

Imeangamia mikono ya Abulahab na yeye (kwa maana hiyo) ameangamia



السورة: AL-MASAD

الآية : 2

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ

Haitamfaa mali yake na (vitendo) alivyovichuma (alivyovifanya)



السورة: AL-MASAD

الآية : 3

سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ

Atauingia moto wenye muwako



السورة: AL-MASAD

الآية : 4

وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ

(Ataingia Motoni yeye) Na mkewe, mchukuzi mkubwa wa kuni



السورة: AL-MASAD

الآية : 5

فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ

Shingoni mwake iko kamba ya kusokotwa



السورة: AL-IKHLAAS 

الآية : 1

قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ

Sema: Yeye Allah ni wa pekee



السورة: AL-IKHLAAS 

الآية : 2

ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ

Allah ndiye tu Mkusudiwa (katika kuabudiwa, kutegemewa na kutatua shida za watu)



السورة: AL-IKHLAAS 

الآية : 3

لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ

Hakuzaa[1] na hakuzaliwa.[2]


1- - Kwa maana hiyo hana mtoto.


2- - Kwa maana hiyo hana baba wala mama.

---------------

------------------------------------------------------------

---------------

------------------------------------------------------------


السورة: AL-IKHLAAS 

الآية : 4

وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ

Na hakuna yeyote anaye fanana naye



السورة: AL-FALAQ

الآية : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ

Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko



السورة: AL-FALAQ

الآية : 2

مِن شَرِّ مَا خَلَقَ

(Najikinga) Dhidi ya shari ya alivyoviumba



السورة: AL-FALAQ

الآية : 3

وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya giza la usiku liingiapo



السورة: AL-FALAQ

الآية : 4

وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya (wanawake) wanaopulizia mafundoni



السورة: AL-FALAQ

الآية : 5

وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ

Na (najikinga) dhidi ya shari ya hasidi anapo husudu



السورة: ANNAAS

الآية : 1

قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ

Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu



السورة: ANNAAS

الآية : 2

مَلِكِ ٱلنَّاسِ

Mfalme wa watu



السورة: ANNAAS

الآية : 3

إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ

Muabudiwa wa haki wa watu (Mwenye haki ya kuabudiwa na watu)



السورة: ANNAAS

الآية : 4

مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ

(Najilinda dhidi ya shari ya (shetani) mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma



السورة: ANNAAS

الآية : 5

ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ

Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu



السورة: ANNAAS

الآية : 6

مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ

(Shetani) Anayetokana na majini na watu