ٱلَّذِيٓ أَنقَضَ ظَهۡرَكَ
Ulio vunja mgongo wako?
وَرَفَعۡنَا لَكَ ذِكۡرَكَ
Na tukakunyanyulia utajo wako?
فَإِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرًا
Basi kwa hakika pamoja na uzito upo wepesi,
إِنَّ مَعَ ٱلۡعُسۡرِ يُسۡرٗا
Hakika pamoja na uzito upo wepesi
فَإِذَا فَرَغۡتَ فَٱنصَبۡ
Na ukipata faragha, fanya juhudi
وَإِلَىٰ رَبِّكَ فَٱرۡغَب
Na kwa (ajili ya) Mola wako Mlezi ushughulike
وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ
Naapa kwa tini na zaituni
وَطُورِ سِينِينَ
Na Mlima wa Sinai
وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ
Na mji huu (wa Makka) wenye amani
لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ
Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa
ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ
Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ
Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha
فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ
Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?
أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ
Kwani Allah si muadilifu kuliko mahakimu wote?
ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi ambaye ameumba
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu
ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Mkarimu kushinda wote!
ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ
Ambaye amefundisha kwa kalamu
عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ
Kamfundisha mtu aliyokuwa hayajui
كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ
Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri
أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ
Akijiona katajirika
إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ
Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ
Umemwona yule anaye mkataza
عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ
Mja anapo sali?
أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ
Waonaje kama yeye yuko juu ya uwongofu?
أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ
Au anaamrisha ucha Mungu?
أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ
Waonaje kama yeye akikanusha na akarudi nyuma?
أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ
Hajui ya kwamba Allah anaona?
كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ
Si hivyo! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele (nywele za mbele)!
نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ
Shungi la uwongo, lenye makosa!