وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ
Na tukambainishia njia zote mbili?
فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ
Lakini hakujitoma (hakuingia) kwenye njia ya vikwazo vya milimani
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ
Na nini kitakujulisha ni nini njia ya vikwazo vya milimani?
فَكُّ رَقَبَةٍ
Kumkomboa mtumwa;
أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ
Au kumlisha siku ya njaa
يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ
Yatima aliye katika jamaa wa karibu (ndugu)
أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ
Au masikini aliye vumbini
ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ
Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana
أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ
Hao ndio watu wa kheri wa kuliani
وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ
Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni
عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ
Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande
وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا
Na hakika amepata hasara aliye iviza (ichafua)
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ
Kina Thamudi walikadhibisha kwasababu ya upotofu wao,
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا
Alipo simama mwovu wao mkubwa
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا
Hapo Mtume wa Allah alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Allah, mwacheni anywe maji fungu lake
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwahivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwasababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا
Wala Yeye haogopi matokeo yake
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ
Naapa kwa usiku unapo funika!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ
Na mchana unapo dhihiri!
وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Na kwa Aliye umba dume na jike!
إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ
Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni tofauti