السورة: AL-FAJRI 

الآية : 10

وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi??



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 11

ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 12

فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi?



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 13

فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 15

فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 16

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 17

كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 18

وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 19

وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 20

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا

Na mnapenda mali mapenzi ya kupita kiasi



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 21

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 22

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 23

وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 24

يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia (mema) katika uhai wangu!



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 25

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote kama kuadhibu kwake



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 28

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 29

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 30

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu



السورة: AL-BALAD 

الآية : 1

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!



السورة: AL-BALAD 

الآية : 2

وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Nawe unakaa Mji huu



السورة: AL-BALAD 

الآية : 3

وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa



السورة: AL-BALAD 

الآية : 4

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu



السورة: AL-BALAD 

الآية : 5

أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ

Ati anadhani hapana yeyote atakaye muweza?



السورة: AL-BALAD 

الآية : 6

يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا

Anasema: Nimeteketeza mali chungu nzima



السورة: AL-BALAD 

الآية : 7

أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?



السورة: AL-BALAD 

الآية : 8

أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?



السورة: AL-BALAD 

الآية : 9

وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ

Na ulimi, na midomo miwili?