السورة: AL-IMRAN 

الآية : 15

۞قُلۡ أَؤُنَبِّئُكُم بِخَيۡرٖ مِّن ذَٰلِكُمۡۖ لِلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَا وَأَزۡوَٰجٞ مُّطَهَّرَةٞ وَرِضۡوَٰنٞ مِّنَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Sema: Je, nikupeni habari ya vilivyo bora zaidi kuliko hivyo? Wenye ucha Mungu tu watapata kwa Mola wao bustani zipitazo mito chini yake, watakaa humo milele na (pia watapata) wake waliotakaswa na radhi za Allah, na Allah ni Mwenye kuwaona sana waja



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 16

ٱلَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَآ إِنَّنَآ ءَامَنَّا فَٱغۡفِرۡ لَنَا ذُنُوبَنَا وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ

Ambao wanasema: Ewe Mola wetu, hakika sisi tumeamini, hivyo tusamehe dhambi zetu na tukinge na adhabu ya Moto



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 17

ٱلصَّـٰبِرِينَ وَٱلصَّـٰدِقِينَ وَٱلۡقَٰنِتِينَ وَٱلۡمُنفِقِينَ وَٱلۡمُسۡتَغۡفِرِينَ بِٱلۡأَسۡحَارِ

Na wafanyao subira na wasemao kweli na wanaotii na wanaotoa (walivyojaaliwa na kuwapa wengine) na wanaoomba msamaha usiku wa manane



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 18

شَهِدَ ٱللَّهُ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَأُوْلُواْ ٱلۡعِلۡمِ قَآئِمَۢا بِٱلۡقِسۡطِۚ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Allah Ameshuhudia kwamba, hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu, na Malaika (pia wameshudia hivyo) na wenye elimu, akisimamia uadilifu. Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima nyingi



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 19

إِنَّ ٱلدِّينَ عِندَ ٱللَّهِ ٱلۡإِسۡلَٰمُۗ وَمَا ٱخۡتَلَفَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَهُمُ ٱلۡعِلۡمُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۗ وَمَن يَكۡفُرۡ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَإِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Hakika, dini (inayokubalika) kwa Allah ni Uislamu tu. Na wale waliopewa Kitabu hawakutofautiana isipokuwa tu baada ya kuwa elimu imewafikia kwa sababu ya uovu uliokuwepo kati yao. Na yeyote anayezikataa Aya za Allah, basi hakika Allah ni Mwepesi mno wa kuhesabu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 20

فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Na kama watakuletea hoja (yoyote), basi sema: Nimeukabidhi uso wangu (nimejisalimisha) kwa Allah; mimi na wale walionifuata. Na waambie waliopewa kitabu na wasio na elimu kwamba: Je, mmesilimu (Mmejisalimisha kwa Allah)? Kama wamesilimu basi hakika wameongoka, na kama wakikataa, basi wajibu wako ni kufikisha tu. Na Allah anawaona mno waja



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 21

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَيَقۡتُلُونَ ٱلَّذِينَ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡقِسۡطِ مِنَ ٱلنَّاسِ فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Hakika, wanaozikataa Aya za Allah na wanaua Mitume bila ya hakina (pia wanaua) watu ambao wanaamrisha uadilifu, wape habari njema[1] ya adhabu iumizayo sana


1- - “…wape habari njema ya adhabu iumizayo sana”. Hapa Kurani imetumia muundo wa fasihi ya lugha ya
Kiarabu unaoitwa “Muundo wa Kudhihaki”. Kumuahidi mtu kuwa utamuadhibu si habari njema na ya
kumfurahisha. Lakini kurani inasema “…wape habari njema ya adhabu iumizayo sana”. Ni aina fulani tu
ya kuwakebehi makafiri na kuwadhihaki. Muundo huu umetumika katika maeneo mengi ya Kurani
ikiwemo Aya ya 49 ya Sura Addukhaan (44) ambapo kafiri wakati atakapoadhibiwa motoni ataambiwa:
“… Onja (adhabu, kwa sababu) wewe ndiye hasa mwenye ukubwa, mheshimiwa! ”Vipi tena mheshimiwa
anaadhibiwa? Huku ni kumdhihaki tu!


السورة: AL-IMRAN 

الآية : 22

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ حَبِطَتۡ أَعۡمَٰلُهُمۡ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Hao ndio ambao amali zao zimepomoka (zimepotea bure) duniani na Akhera na hawana yeyote wa kuwanusuru”



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 23

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ أُوتُواْ نَصِيبٗا مِّنَ ٱلۡكِتَٰبِ يُدۡعَوۡنَ إِلَىٰ كِتَٰبِ ٱللَّهِ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَهُمۡ ثُمَّ يَتَوَلَّىٰ فَرِيقٞ مِّنۡهُمۡ وَهُم مُّعۡرِضُونَ

Hivi hukuwaona ambao wamepewa sehemu ya kitabu; wanaitwa kukiendea kitabu cha Allah ili kihukumu baina yao, kisha kundi miongoni mwao linakengeuka na wao wakipuuza?



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 24

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ قَالُواْ لَن تَمَسَّنَا ٱلنَّارُ إِلَّآ أَيَّامٗا مَّعۡدُودَٰتٖۖ وَغَرَّهُمۡ فِي دِينِهِم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Hiyo ni kwa sababu walisema: Moto (wa Jahanamu) hautatugusa[1] isipokuwa kwa siku chache tu, na yaliwadanganya katika dini yao yale waliyokuwa wakiyazua


1- - Hautatuunguza


السورة: AL-IMRAN 

الآية : 25

فَكَيۡفَ إِذَا جَمَعۡنَٰهُمۡ لِيَوۡمٖ لَّا رَيۡبَ فِيهِ وَوُفِّيَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Basi itakuwaje tutakapo-wakusanya kwa ajili ya siku ambayo haina shaka, na kila nafsi italipwa kwa ukamilifu kutokana na ilichokichuma na wao hawatadhulumiwa?



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 26

قُلِ ٱللَّهُمَّ مَٰلِكَ ٱلۡمُلۡكِ تُؤۡتِي ٱلۡمُلۡكَ مَن تَشَآءُ وَتَنزِعُ ٱلۡمُلۡكَ مِمَّن تَشَآءُ وَتُعِزُّ مَن تَشَآءُ وَتُذِلُّ مَن تَشَآءُۖ بِيَدِكَ ٱلۡخَيۡرُۖ إِنَّكَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Sema: Ewe Mola wangu, Mmiliki wa ufalme, unampa ufalme umtakaye, na unamuondolea ufalme umtakaye, na unamtukuza umtakaye, na unamfanya dhalili umtakaye. Kheri zote zipo mkononi mwako tu. Hakika, wewe ni Muweza sana wa kila kitu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 27

تُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَتُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِۖ وَتُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَتُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتَ مِنَ ٱلۡحَيِّۖ وَتَرۡزُقُ مَن تَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٖ

Unauingiza usiku ndani ya mchana[1], na unauingiza mchana ndani ya usiku, na unatoa (kiumbe) hai kutoka katika (kiumbe) mfu, na unatoa (kiumbe) mfu kutoka katika (kiumbe) hai. Na unampa riziki umtakaye bila ya hesabu


1- - Allah anauingiza usiku katika mchana na unakuwa mrefu katika kipindi fulani na pia anauingiza mchana
katika usiku na unakuwa mrefu katika kipindi kingine. Allah anaelezea uweza wake mkubwa unaotoa
kiumbe hai kutoka katika kinachoonekana kama kiumbe mfu, na anatoa kiumbe mfu katika kiumbe hai!
Hapa Allah anelezea uwezo wake mkubwa katika kinachoitwa “Mfuatano na muendelezo wa maisha ya
viumbe hai”.


السورة: AL-IMRAN 

الآية : 28

لَّا يَتَّخِذِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ فَلَيۡسَ مِنَ ٱللَّهِ فِي شَيۡءٍ إِلَّآ أَن تَتَّقُواْ مِنۡهُمۡ تُقَىٰةٗۗ وَيُحَذِّرُكُمُ ٱللَّهُ نَفۡسَهُۥۗ وَإِلَى ٱللَّهِ ٱلۡمَصِيرُ

Waumini wasiwafanye makafiri kuwa vipenzi vyao badala ya Waumini (wenzao). Na atakayefanya hilo, basi hana chochote mbele ya Allah, isipokuwa kwa kujikinga dhidi ya shari zao. Na Allah anakutahadharisheni nafsi yake. Na kwa Allah tu ndio marejeo



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 29

قُلۡ إِن تُخۡفُواْ مَا فِي صُدُورِكُمۡ أَوۡ تُبۡدُوهُ يَعۡلَمۡهُ ٱللَّهُۗ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Sema: Mkiyaficha yaliyomo vifuani mwenu au mkiyadhihirisha Allah anayajua, na anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini, na Allah ni Mwenye uweza mkubwa wa kila kitu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 30

يَوۡمَ تَجِدُ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا عَمِلَتۡ مِنۡ خَيۡرٖ مُّحۡضَرٗا وَمَا عَمِلَتۡ مِن سُوٓءٖ تَوَدُّ لَوۡ أَنَّ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَهُۥٓ أَمَدَۢا بَعِيدٗاۗ وَيُحَذِّرُكُمُ ٱللَّهُ نَفۡسَهُۥۗ وَٱللَّهُ رَءُوفُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Siku ambayo kila nafsi itakuta kheri iliyoitenda ikiwa imehudhurishwa, na pia ubaya iliyoutenda. Itapenda lau kungekuwepo masafa marefu kati yake na ubaya huo. Na Allah anakutahadharisheni nafsi yake. Na Allah ni Mpole mno kwa waja (wake)



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 31

قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allah, basi nifuateni, Allah atakupendeni na atakusameheni madhambi yenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 32

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Sema: Mtiini Allah na Mtume. Kama mkikengeuka, basi kwa hakika Allah hawapendi makafiri



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 33

۞إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰٓ ءَادَمَ وَنُوحٗا وَءَالَ إِبۡرَٰهِيمَ وَءَالَ عِمۡرَٰنَ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Hakika, Allah amemteua Adamu na Nuhu na familia ya Ibrahimu na familia ya Imrani kati ya walimwengu (wengine wa wakati wao)



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 34

ذُرِّيَّةَۢ بَعۡضُهَا مِنۢ بَعۡضٖۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Ni kizazi kinachotokana na wao kwa wao, na Allah ni Msikivu sana, Mjuzi mno



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 35

إِذۡ قَالَتِ ٱمۡرَأَتُ عِمۡرَٰنَ رَبِّ إِنِّي نَذَرۡتُ لَكَ مَا فِي بَطۡنِي مُحَرَّرٗا فَتَقَبَّلۡ مِنِّيٓۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

(Kumbuka) Aliposema mke wa Imrani (kwamba): Ewe Mola wangu, hakika mimi nimeweka nadhiri kwa aliyemo tumboni mwangu kwa ajili yako akiwa Wakfu, basi nikubalie. Hakika, wewe ni Msikiaji mno, Mjuzi sana



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 36

فَلَمَّا وَضَعَتۡهَا قَالَتۡ رَبِّ إِنِّي وَضَعۡتُهَآ أُنثَىٰ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا وَضَعَتۡ وَلَيۡسَ ٱلذَّكَرُ كَٱلۡأُنثَىٰۖ وَإِنِّي سَمَّيۡتُهَا مَرۡيَمَ وَإِنِّيٓ أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّيَّتَهَا مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

Alipomzaa alisema: Ewe Mola wangu, hakika nimezaa (mtoto) mwanamke, na Allah anamjua zaidi (mtoto) aliyemzaa. Na (mtoto) mwanaume sio sawa na (mtoto) mwanamke. Na kwa hakika, mimi nimempa jina la Mariamu, na kwa hakika mimi nakuomba umkinge yeye na kizazi chake dhidi ya shetani aliyelaaniwa



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 37

فَتَقَبَّلَهَا رَبُّهَا بِقَبُولٍ حَسَنٖ وَأَنۢبَتَهَا نَبَاتًا حَسَنٗا وَكَفَّلَهَا زَكَرِيَّاۖ كُلَّمَا دَخَلَ عَلَيۡهَا زَكَرِيَّا ٱلۡمِحۡرَابَ وَجَدَ عِندَهَا رِزۡقٗاۖ قَالَ يَٰمَرۡيَمُ أَنَّىٰ لَكِ هَٰذَاۖ قَالَتۡ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ إِنَّ ٱللَّهَ يَرۡزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٍ

Basi Mola wake akampokea kwa mapokezi mazuri na akamkuza makuzi mazuri na akampa Zakaria jukumu la kumlea. Zakaria kila alipoingia kwa Mariamu katika Mihirabu[1] alikuta ana riziki (ya vyakula). Akasema: Ewe Mariamu, unavipata wapi (vyakula) hivi? Akasema: Vinatoka kwa Allah. Hakika Allah anampa riziki amtakaye bila ya hesabu


1- - Mihirabu ni chumba kinachokuwepo ndani ya msikiti kwa madhumuni ya kukaa faragha ili kumuabudu
Allah. Pia mihirabu ni sehemu anayosimama imamu katika kuongoza Swala msikitini.


السورة: AL-IMRAN 

الآية : 38

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُۥۖ قَالَ رَبِّ هَبۡ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةٗ طَيِّبَةًۖ إِنَّكَ سَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Hapo, Zakaria alimuomba Mola wake. Alisema: “Ewe Mola wangu, nakuomba kizazi chema kutoka kwako, hakika wewe ni Mwingi wa kusikia maombi



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 39

فَنَادَتۡهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَهُوَ قَآئِمٞ يُصَلِّي فِي ٱلۡمِحۡرَابِ أَنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكَ بِيَحۡيَىٰ مُصَدِّقَۢا بِكَلِمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَسَيِّدٗا وَحَصُورٗا وَنَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Malaika walimuita akiwa amesimama Mihirabuni akiswali (na kumwambia) kwamba: Allah anakupabishara (ya mtoto atakayeitwa) Yahya, Mwenye kusadikisha neno kutoka kwa Allah, na ni Bwana na ni Mtawa na Nabii atokanaye na watu wema



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 40

قَالَ رَبِّ أَنَّىٰ يَكُونُ لِي غُلَٰمٞ وَقَدۡ بَلَغَنِيَ ٱلۡكِبَرُ وَٱمۡرَأَتِي عَاقِرٞۖ قَالَ كَذَٰلِكَ ٱللَّهُ يَفۡعَلُ مَا يَشَآءُ

Akasema: Ewe Mola wangu, vipi nitapata mtoto ilhali ukongwe umenifikia na mke wangu ni tasa?Allah akasema: Hivyo ndivyo Allah hufanya apendavyo



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 41

قَالَ رَبِّ ٱجۡعَل لِّيٓ ءَايَةٗۖ قَالَ ءَايَتُكَ أَلَّا تُكَلِّمَ ٱلنَّاسَ ثَلَٰثَةَ أَيَّامٍ إِلَّا رَمۡزٗاۗ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ كَثِيرٗا وَسَبِّحۡ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِبۡكَٰرِ

Akasema: Ewe Mola wangu, nakuomba nipe alama (dalili). Akasema: Alama yako ni kwamba hutazungumza na watu kwa siku tatu isipokuwa kwa ishara tu, na mtaje Mola wako kwa wingi, na umtakase katika nyakati za jioni na asubuhi



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 42

وَإِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰكِ وَطَهَّرَكِ وَٱصۡطَفَىٰكِ عَلَىٰ نِسَآءِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na (kumbuka) Malaika walipo-sema: Ewe Mariamu, hakika Allah amekuteua na amekutakasa, na amekuteua kuliko wanawake wa walimwengu wote



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 43

يَٰمَرۡيَمُ ٱقۡنُتِي لِرَبِّكِ وَٱسۡجُدِي وَٱرۡكَعِي مَعَ ٱلرَّـٰكِعِينَ

Ewe Mariamu, mnyenyekee Mola wako na sujudu na rukuu pamoja na wenye kurukuu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 44

ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهِ إِلَيۡكَۚ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يُلۡقُونَ أَقۡلَٰمَهُمۡ أَيُّهُمۡ يَكۡفُلُ مَرۡيَمَ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Hizo ni baadhi tu ya habari za Ghaibu tunazokufunulia, na hukuwa nao wakati wakitupa kalamu zao (kwa kupiga kura); ni nani kati yao atamlea Mariamu. Na hukuwa nao walipokuwa wakigombana