أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِأَصۡحَٰبِ ٱلۡفِيلِ
Je, hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo watenda wale wenye tembo?
أَلَمۡ يَجۡعَلۡ كَيۡدَهُمۡ فِي تَضۡلِيلٖ
Je, hakujaalia vitimbi vyao kuharibika?
وَأَرۡسَلَ عَلَيۡهِمۡ طَيۡرًا أَبَابِيلَ
Na akawapelekea ndege makundi kwa makundi?
تَرۡمِيهِم بِحِجَارَةٖ مِّن سِجِّيلٖ
(Ndege) Wanaowatupia mawe ya Motoni?
فَجَعَلَهُمۡ كَعَصۡفٖ مَّأۡكُولِۭ
(Mawe hayo) Yakawafanya kama majani yaliyoliwa (yaliyotafunwa)!
لِإِيلَٰفِ قُرَيۡشٍ
Kwasababu ya kuzoea kwa Waqureshi
إِۦلَٰفِهِمۡ رِحۡلَةَ ٱلشِّتَآءِ وَٱلصَّيۡفِ
Kuzoea kwao safari za Kusi na Kaskazi
فَلۡيَعۡبُدُواْ رَبَّ هَٰذَا ٱلۡبَيۡتِ
Kwasababu ya hayo, wamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii (Tukufu ya Makka)
ٱلَّذِيٓ أَطۡعَمَهُم مِّن جُوعٖ وَءَامَنَهُم مِّنۡ خَوۡفِۭ
Ambaye amewalisha wasipate njaa, na amewasalimisha wasipate hofu
أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يُكَذِّبُ بِٱلدِّينِ
Je, umemuona anayekadhibisha (anayekataa) dini?
فَذَٰلِكَ ٱلَّذِي يَدُعُّ ٱلۡيَتِيمَ
Basi huyo ni anayemsukuma (na kumtelekeza) yatima
وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ
Wala hahimizi kumlisha (kumpa chakula) maskini
فَوَيۡلٞ لِّلۡمُصَلِّينَ
Basi, ole wao wanaoswali
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَن صَلَاتِهِمۡ سَاهُونَ
Ambao wanapuuza Swala zao
ٱلَّذِينَ هُمۡ يُرَآءُونَ
Ambao wanaonyesha (matendo yao kwa watu ili wasifiwe)
وَيَمۡنَعُونَ ٱلۡمَاعُونَ
Na wanazuia msaada
إِنَّآ أَعۡطَيۡنَٰكَ ٱلۡكَوۡثَرَ
Hakika tumekupa Kauthar (kheri nyingi ikiwemo mto wa Peponi)
فَصَلِّ لِرَبِّكَ وَٱنۡحَرۡ
Basi Swali na uchinje kwa ajili ya Mola wako Mlezi
إِنَّ شَانِئَكَ هُوَ ٱلۡأَبۡتَرُ
Hakika anayekuchukia (wewe Muhammad) ndiye hasa aliyepungukiwa (na kheri zote)
قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡكَٰفِرُونَ
Sema: Enyi makafiri
لَآ أَعۡبُدُ مَا تَعۡبُدُونَ
Siabudu mnacho kiabudu
وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ
Na nyinyi hamuabudu ninaye muabudu
وَلَآ أَنَا۠ عَابِدٞ مَّا عَبَدتُّمۡ
Na mimi si mwenye kuviabudu mlivyo viabudu
وَلَآ أَنتُمۡ عَٰبِدُونَ مَآ أَعۡبُدُ
Na nyinyi si wenye kuabudu ninayemuabudu
لَكُمۡ دِينُكُمۡ وَلِيَ دِينِ
Nyinyi mna dini yenu, nami nina dini yangu
إِذَا جَآءَ نَصۡرُ ٱللَّهِ وَٱلۡفَتۡحُ
Itakapokuja nusra ya Allah na ushindi (ukombozi wa mji wa Makka)
وَرَأَيۡتَ ٱلنَّاسَ يَدۡخُلُونَ فِي دِينِ ٱللَّهِ أَفۡوَاجٗا
Na ukaona watu wanaingia katika Dini ya Allah kwa makundi
فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَٱسۡتَغۡفِرۡهُۚ إِنَّهُۥ كَانَ تَوَّابَۢا
Basi zitakase sifa za Mola wako Mlezi na muombe msamaha. Hakika, Yeye (Allah) amekuwa Mwenye kukubali sana toba. Sura imetoa utabiri wa kifo cha Mtume rehma na amani ziwe juu yake
تَبَّتۡ يَدَآ أَبِي لَهَبٖ وَتَبَّ
Imeangamia mikono ya Abulahab na yeye (kwa maana hiyo) ameangamia
مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُ مَالُهُۥ وَمَا كَسَبَ
Haitamfaa mali yake na (vitendo) alivyovichuma (alivyovifanya)