السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 73

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi Tumeufanya kuwa ni ukumbusho na manufaa kwa wasafiri



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 74

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliyetukuka



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 75

۞فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 76

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Hakika hicho ni kiapo kikubwa lau mnaelewa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 77

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika ya hiyo ni Kurani tukufu



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 78

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa (Walio twahara)



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 80

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 81

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Hivi kwa maneno haya nyinyi mnapuuza na kuikanusha?



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 82

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na mnafanya (badala ya kushu-kuru) kwa riziki mnayopata, nyinyi ndio mnakad hibisha



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 83

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Itakuaje basi pale roho itaka-pofika kwenye koo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 84

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama tu



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 85

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Nasi Tuko karibu naye zaidi kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuoni



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 86

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hammo katika mamlaka yangu.[1]


1- - Basi kama lau kusingekua na kufufuliwa.


السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 87

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho (mwilini mwake), mkiwa ni wakweli?



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 88

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa (mwenye roho hiyo) ni miongoni mwa waliokurubishwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 89

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na mabustani zenye kila aina ya neema



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 90

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa watu wa kuliani



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 91

فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Basi itaambiwa amani iwe juu yako uliye katika watu kuliani



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 92

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa wakadhibisha waliyopotea



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 93

فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ

Basi mapokezi na mafikio yake ni maji ya moto yachemkayo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 94

وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ

Na kuingizwa kwenye Moto wa jahimu, (uwakao vikali mno)



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 95

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Hakika hii bila shaka ni haki yenye yakini.[1]


1- - Hakika haya yaliotajwa katika Sura hii tukufu bila shaka ni kiini cha yakini ilio thabiti, isiyo ingiliwa na shaka hata kidogo.


السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 96

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliye Mtukufu



السورة: AL-HADIID

الآية : 1

سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Vimemsabihi (vimemtakasa) Allah na kumtukuza vyote vilivyomo katika mbingu na ardhi na yeye tu ndiye Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



السورة: AL-HADIID

الآية : 2

لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Ni Wake pekee ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na yeye Muweza wa kila kitu



السورة: AL-HADIID

الآية : 3

هُوَ ٱلۡأَوَّلُ وَٱلۡأٓخِرُ وَٱلظَّـٰهِرُ وَٱلۡبَاطِنُۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Yeye ndiye wa mwanzo na ndiye wa mwisho na mjuzi wa mambo ya dhahiri na ya siri na yeye ni Mjuzi sana wa kila kitu



السورة: AL-HADIID

الآية : 4

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يَعۡلَمُ مَا يَلِجُ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا يَخۡرُجُ مِنۡهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا يَعۡرُجُ فِيهَاۖ وَهُوَ مَعَكُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha Akawa juu (Istawaa)[1] ya ‘Arsh, Anajua yale yanayoingia ardhini, na yale yatokayo humo, na yale yanayoteremka kutoka mbinguni, na yale yanayopanda humo, Naye Yu Pamoja nanyi popote mlipo. Na Allah ni Mwenye kuona yote myatendayo


1- - Faida: Maana ya Istawaa: Yuko juu kabisa kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah. {Rejea Tanbihi (2: 29)}.


السورة: AL-HADIID

الآية : 5

لَّهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ

Ni Wake Pekee ufalme wa mbingu na ardhi, kwa Allah Pekee yanarejeshwa mambo yote



السورة: AL-HADIID

الآية : 6

يُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَيُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِۚ وَهُوَ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Anauingiza usiku katika mchana, na Anaingiza mchana katika usiku, Naye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani