السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo