السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 25

كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 26

وَزُرُوعٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na mimea na vyeo vitukufu!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 27

وَنَعۡمَةٖ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ

Na neema walizokuwa wakiji-stareheshea!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 28

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ

Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 29

فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ

Hazikuwalilia mbingu wala ardhi, wala hawakupewa muhula



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 30

وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ

Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 31

مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 32

وَلَقَدِ ٱخۡتَرۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ عِلۡمٍ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 33

وَءَاتَيۡنَٰهُم مِّنَ ٱلۡأٓيَٰتِ مَا فِيهِ بَلَـٰٓؤٞاْ مُّبِينٌ

Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 34

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ لَيَقُولُونَ

Hakika hawa wanasema:



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 35

إِنۡ هِيَ إِلَّا مَوۡتَتُنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُنشَرِينَ

Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 36

فَأۡتُواْ بِـَٔابَآئِنَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 37

أَهُمۡ خَيۡرٌ أَمۡ قَوۡمُ تُبَّعٖ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ أَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa’ na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 38

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَا لَٰعِبِينَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 39

مَا خَلَقۡنَٰهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 40

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ مِيقَٰتُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 41

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي مَوۡلًى عَن مَّوۡلٗى شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 42

إِلَّا مَن رَّحِمَ ٱللَّهُۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Isipo kuwa atakaye mrehemu Allah. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 43

إِنَّ شَجَرَتَ ٱلزَّقُّومِ

Hakika Mti wa Zaqqum



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 44

طَعَامُ ٱلۡأَثِيمِ

Ni chakula cha mwenye dhambi



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 45

كَٱلۡمُهۡلِ يَغۡلِي فِي ٱلۡبُطُونِ

Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 46

كَغَلۡيِ ٱلۡحَمِيمِ

Kama kutokota kwa maji ya moto



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 47

خُذُوهُ فَٱعۡتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 48

ثُمَّ صُبُّواْ فَوۡقَ رَأۡسِهِۦ مِنۡ عَذَابِ ٱلۡحَمِيمِ

Kisha mwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 49

ذُقۡ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡكَرِيمُ

Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 50

إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِۦ تَمۡتَرُونَ

Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 51

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 52

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani na chemchem



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 53

يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 54

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurulaini