فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا
Basi pigana katika njia ya Allah. Hukalifishwi isipokuwa nafsi yako tu, na wahamasishe waumini, huenda Allah akayazuia mashambulizi ya waliokufuru. Na Allah ni Mkali sana wa kushambulia na Mkali wa kuadhibu
مَّن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةً حَسَنَةٗ يَكُن لَّهُۥ نَصِيبٞ مِّنۡهَاۖ وَمَن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةٗ سَيِّئَةٗ يَكُن لَّهُۥ كِفۡلٞ مِّنۡهَاۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقِيتٗا
Yeyote atakayeombea maombezi mazuri (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo jema) atapata fungu katika jambo zuri hilo, na yeyote atakayeombea maombezi maovu (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo ovu) atapata fungu katika jambo ovu hilo. Na Allahni Mwenye uweza na ujuzi juu ya kila kitu
وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٖ فَحَيُّواْ بِأَحۡسَنَ مِنۡهَآ أَوۡ رُدُّوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَسِيبًا
Na mnapoamkiwa maamkizi yoyote yale, basi nanyi itikieni kwa maamkizi mazuri zaidi kuliko hayo au rejesheni hayo hayo. Hakika, Allah ni Mwenye kuhesabu kila kitu
ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۗ وَمَنۡ أَصۡدَقُ مِنَ ٱللَّهِ حَدِيثٗا
Allah, hakuna mwenye haki ya kuabudiwa ispokuwa yeye tu. Kwa yakini kabisa, atakukusanyeni katika Siku ya Kiyama isiyokuwa na shaka yoyote. Na ni nani mkweli sana wa maneno kuliko Allah?