السورة: AN-FAL 

الآية : 25

وَٱتَّقُواْ فِتۡنَةٗ لَّا تُصِيبَنَّ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنكُمۡ خَآصَّةٗۖ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Na (enyi waumini) jihadharini na fitina (kujiingiza kwenye majanga) ambayo hayatowasibu waliodhulumu (waliofanya uovu) tu miongoni mwenu. Na jueni kuwa Allah ni Mkali wa kuadhibu



السورة: AN-FAL 

الآية : 26

وَٱذۡكُرُوٓاْ إِذۡ أَنتُمۡ قَلِيلٞ مُّسۡتَضۡعَفُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ تَخَافُونَ أَن يَتَخَطَّفَكُمُ ٱلنَّاسُ فَـَٔاوَىٰكُمۡ وَأَيَّدَكُم بِنَصۡرِهِۦ وَرَزَقَكُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Na kumbukeni (Enyi Muhajirina) mlipokuwa wachache mnaonyanyaswa katika ardhi (ya Makkah), mnaogopa watu wasikunyakueni (na kukuteseni), basi (Allah) akakupeni hifadhi (mahali pazuri pa kuishi ambapo ni mji wa Madina), na akakutieni nguvu kwa nusra yake, na akakupeni riziki nzuri ili mpate kushukuru



السورة: AN-FAL 

الآية : 27

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَخُونُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ وَتَخُونُوٓاْ أَمَٰنَٰتِكُمۡ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Enyi mlioamini, msimfanyie hiana Allah na Mtume (kwa kuvunja ahadi na makubaliano ya imani zenu), wala msifanyie khiyana amana zenu (mnazoaminiana), na ilhali mnajua



السورة: AN-FAL 

الآية : 28

وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَآ أَمۡوَٰلُكُمۡ وَأَوۡلَٰدُكُمۡ فِتۡنَةٞ وَأَنَّ ٱللَّهَ عِندَهُۥٓ أَجۡرٌ عَظِيمٞ

Na jueni ya kwamba, hakika mali zenu na watoto ni mtihani[1], na kwamba kwa Allah kuna ujira mkubwa mno


1- - Mali na watoto ni mtihani unaoweza kumuingiza mtu katika mitihani kwa kuwa na kiburi au kufanya mambo ya haramu kwa sababu ya mali au watoto.


السورة: AN-FAL 

الآية : 29

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِن تَتَّقُواْ ٱللَّهَ يَجۡعَل لَّكُمۡ فُرۡقَانٗا وَيُكَفِّرۡ عَنكُمۡ سَيِّـَٔاتِكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡۗ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Enyi mlioamini, mkimcha Allah atakufanyieni kipambanuzi (kinachokuwezesheni kupambanua kati ya haki na batili), na atakusameheni na kukufutieni makosa yenu. Na Allah ni Mwenye fadhila kubwa mno



السورة: AN-FAL 

الآية : 30

وَإِذۡ يَمۡكُرُ بِكَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لِيُثۡبِتُوكَ أَوۡ يَقۡتُلُوكَ أَوۡ يُخۡرِجُوكَۚ وَيَمۡكُرُونَ وَيَمۡكُرُ ٱللَّهُۖ وَٱللَّهُ خَيۡرُ ٱلۡمَٰكِرِينَ

Na (kumbuka) wakati waliokufuru wanakupangia njama (pale Makkah kwenye Darun Nad’wa ima) wakufunge (wakuweke kizuizini) au wakuue au wakutoe (wakufukuze). Na wanapanga njama (hiyo kwa siri) na Allah anapanga njama (zake). Na Allah ndiye Mbora wa wanaopindua njama



السورة: AN-FAL 

الآية : 31

وَإِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُنَا قَالُواْ قَدۡ سَمِعۡنَا لَوۡ نَشَآءُ لَقُلۡنَا مِثۡلَ هَٰذَآ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na (Washirikina) wanaposomewa Aya zetu, husema: “Tumesikia; laiti tungetaka (nasi) tungesema kama hii (Qur’ani). Hii (Qur’an) si chochote ila ni ngano za watu wa kale tu”



السورة: AN-FAL 

الآية : 32

وَإِذۡ قَالُواْ ٱللَّهُمَّ إِن كَانَ هَٰذَا هُوَ ٱلۡحَقَّ مِنۡ عِندِكَ فَأَمۡطِرۡ عَلَيۡنَا حِجَارَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ أَوِ ٱئۡتِنَا بِعَذَابٍ أَلِيمٖ

Na (kumbuka) wakati (washirikina) waliposema: Ewe Allah, ikiwa ni kweli hii (Qur’an) inatoka kwako, basi tushushie (mvua ya) mawe kutoka mbinguni (kama ulivyowafanyia watu wa Nabii Luti) au tuletee adhabu (yoyote) inayoumiza sana



السورة: AN-FAL 

الآية : 33

وَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيُعَذِّبَهُمۡ وَأَنتَ فِيهِمۡۚ وَمَا كَانَ ٱللَّهُ مُعَذِّبَهُمۡ وَهُمۡ يَسۡتَغۡفِرُونَ

Na Allah hakuwa Mwenye kuwaadhibu (kuwaangamiza washirikina kama walivyoomba) ilhali nawe upo nao, na Allah si mwenye kuwaadhibu na ilhali wanaomba msamaha



السورة: AN-FAL 

الآية : 34

وَمَا لَهُمۡ أَلَّا يُعَذِّبَهُمُ ٱللَّهُ وَهُمۡ يَصُدُّونَ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَمَا كَانُوٓاْ أَوۡلِيَآءَهُۥٓۚ إِنۡ أَوۡلِيَآؤُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُتَّقُونَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na (Washirikina) wana jambo gani (jema) hata Allah asiwaadhibu (asiwaangamize), na ilhali wanauwekea vikwazo Msikiti Mtukufu (kwa kuwazuia watu kwenda kutekeleza ibada) na wala wao hawakuwa waangalizi wake? Hawakuwa waangalizi wake ila wachaMungu tu, lakini wengi wao hawajui (kuwa hawana haki hiyo ya uangalizi wa Msikiti Mtukufu)



السورة: AN-FAL 

الآية : 35

وَمَا كَانَ صَلَاتُهُمۡ عِندَ ٱلۡبَيۡتِ إِلَّا مُكَآءٗ وَتَصۡدِيَةٗۚ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ

Na haikuwa (Swala) ibada yao kwenye Nyumba (Al Kaaba) ila ni kupiga miruzi na makofi tu. Basi (enyi Washirikina) onjeni adhabu (ya duniani kwa kupigwa kwenye vita vya Badri) (na adhabu ya huko Akhera inawangojeni) kwa vile mlivyokuwa mnakufuru



السورة: AN-FAL 

الآية : 36

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُنفِقُونَ أَمۡوَٰلَهُمۡ لِيَصُدُّواْ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَسَيُنفِقُونَهَا ثُمَّ تَكُونُ عَلَيۡهِمۡ حَسۡرَةٗ ثُمَّ يُغۡلَبُونَۗ وَٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِلَىٰ جَهَنَّمَ يُحۡشَرُونَ

Hakika wale waliokufuru hutoa mali zao ili kuzuia (kuiwekea vikwazo) njia ya Allah (Uislamu usimakinike na watu wasiufuate). Basi watazitoa (mali zao hizo), kisha zitakuwa majuto kwao, kisha watashindwa. Na waliokufuru watakusanywa katika Jahanamu tu



السورة: AN-FAL 

الآية : 37

لِيَمِيزَ ٱللَّهُ ٱلۡخَبِيثَ مِنَ ٱلطَّيِّبِ وَيَجۡعَلَ ٱلۡخَبِيثَ بَعۡضَهُۥ عَلَىٰ بَعۡضٖ فَيَرۡكُمَهُۥ جَمِيعٗا فَيَجۡعَلَهُۥ فِي جَهَنَّمَۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Allah (aliyafanya hayo) ili awapambanue waovu dhidi ya wema, na kuwaweka waovu juu ya waovu wengine warundikane wote pamoja, na kisha awatumbukize katika Jahanamu. Hao ndio waliohasirika (duniani na Akhera)



السورة: AN-FAL 

الآية : 38

قُل لِّلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِن يَنتَهُواْ يُغۡفَرۡ لَهُم مَّا قَدۡ سَلَفَ وَإِن يَعُودُواْ فَقَدۡ مَضَتۡ سُنَّتُ ٱلۡأَوَّلِينَ

(Ewe Nabii Muhammad) Waambie waliokufuru kwamba: Iwapo watakoma (Washirikina, kuwafanyia uadui Waislamu na kuwapiga vita) watasamehewa yaliyokwishapita. Na wakirudi (kwenye maovu yao hayo) basi imekwishapita mifano (kama hii ya kuangamiza) kwa watu wa kale (nao wangoje kuangamizwa kama wenzao waliopita)



السورة: AN-FAL 

الآية : 39

وَقَٰتِلُوهُمۡ حَتَّىٰ لَا تَكُونَ فِتۡنَةٞ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ كُلُّهُۥ لِلَّهِۚ فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِمَا يَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Na piganeni nao (Washirikina) mpaka fitina (mateso dhidi ya Waislamu) yasiwepo, na Dini yote iwe ya Allah. Basi wakiacha, hakika Allah anayaona wanayoyatenda



السورة: AN-FAL 

الآية : 40

وَإِن تَوَلَّوۡاْ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَوۡلَىٰكُمۡۚ نِعۡمَ ٱلۡمَوۡلَىٰ وَنِعۡمَ ٱلنَّصِيرُ

Na kama wakigeuka (na kuamua kuendelea na uadui wao) basi jueni kwamba, Allah ndiye Mtetezi wenu. Mtetezi bora kabisa na Msaidizi bora kabisa ni yeye