السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 22

وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَيۡنَ شُرَكَآؤُكُمُ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ

Na (kumbuka) siku tutakapowa-kusanya wote kisha tuwaambie wale washirikina (kwamba): Wako wapi washirika wenu ambao mlikuwa mnadai (kuwa ni washirika wa Allah)?



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 23

ثُمَّ لَمۡ تَكُن فِتۡنَتُهُمۡ إِلَّآ أَن قَالُواْ وَٱللَّهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشۡرِكِينَ

Kisha haukuwa mtihani wao isipokuwa kwamba walisema tu: Ewe Mola wetu tunaapa; sisi hatukuwa Washirikina



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 24

ٱنظُرۡ كَيۡفَ كَذَبُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡۚ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Ona namna walivyozidanganya nafsi zao na yakawapotea yote waliyokuwa wanayazua



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 25

وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُ إِلَيۡكَۖ وَجَعَلۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ أَكِنَّةً أَن يَفۡقَهُوهُ وَفِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٗاۚ وَإِن يَرَوۡاْ كُلَّ ءَايَةٖ لَّا يُؤۡمِنُواْ بِهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُوكَ يُجَٰدِلُونَكَ يَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na miongni mwao wapo wanaokusikiliza na tumeweka juu ya nyoyo zao vifuniko wasiyafahamu (hayo wanayoyasikia) na katika masikio yao (tumeweka) uziwi. Na wanapoona kila Aya (inayoteremka kusadikisha Utume wako) hawaiamini mpaka wanapokujia wanakufanyia mjadala wakisema wale waliokufuru kwamba: (Haya anayoyasema) sio chochote isipokuwa tu ni hadithi za kale



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 26

وَهُمۡ يَنۡهَوۡنَ عَنۡهُ وَيَنۡـَٔوۡنَ عَنۡهُۖ وَإِن يُهۡلِكُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Na wanakataza (watu kuiamini Qur’ani) na (wao wenyewe) wanajitenga nayo. Na hawaangamizi isipokuwa nafsi zao tu, na hawatambui



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 27

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَى ٱلنَّارِ فَقَالُواْ يَٰلَيۡتَنَا نُرَدُّ وَلَا نُكَذِّبَ بِـَٔايَٰتِ رَبِّنَا وَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na lau ungeona wakati watakaposimamishwa motoni na kusema (kwa majuto): Eee! Laiti tungerudishwa (duniani) na tusizikanushe Aya za Mola wetu Mlezi na tuwe miongoni mwa Waumini



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 28

بَلۡ بَدَا لَهُم مَّا كَانُواْ يُخۡفُونَ مِن قَبۡلُۖ وَلَوۡ رُدُّواْ لَعَادُواْ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Bali yamewadhihirikia yale waliyokuwa wanayaficha kabla ya hapo. Na lau kama wangerudishwa, kwa yakini kabisa wangerudia yale waliyokatazwa. Na kwa hakika kabisa wao ni waongo



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 29

وَقَالُوٓاْ إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ

Na walisema: Hayakuwa haya (maisha) isipokuwa tu ni maisha yetu ya duniani, na sisi si wenye kufufuliwa



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 30

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَىٰ رَبِّهِمۡۚ قَالَ أَلَيۡسَ هَٰذَا بِٱلۡحَقِّۚ قَالُواْ بَلَىٰ وَرَبِّنَاۚ قَالَ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ

Na lau kama utawaona wakati watakaposimamishwa kwa Mola wao atasema Allah na kuwaambia): Hivi hili (la kufufuliwa) sio kweli? Watasema: Tunaapa kwa Mola wetu (kwamba ni kweli). (Allah) Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mnayapinga



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 31

قَدۡ خَسِرَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱللَّهِۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَتۡهُمُ ٱلسَّاعَةُ بَغۡتَةٗ قَالُواْ يَٰحَسۡرَتَنَا عَلَىٰ مَا فَرَّطۡنَا فِيهَا وَهُمۡ يَحۡمِلُونَ أَوۡزَارَهُمۡ عَلَىٰ ظُهُورِهِمۡۚ أَلَا سَآءَ مَا يَزِرُونَ

Hakika, wamepata hasara wale waliopinga kukutana na Allah, hadi kitakapowajia Kiyama ghafla watasema: Eee! Majuto ni yetu kwa (sababu ya) yale tuliyoyafanyia uzembe humo (duniani), na huku wanabeba mizigo (makosa) yao migongoni mwao. Elewa kwamba, ni mabaya mno hayo (madhambi) wanayoyabeba



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 32

وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا لَعِبٞ وَلَهۡوٞۖ وَلَلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na maisha ya duniani si chochote isipokuwa tu ni mchezo na pumbao. Na kwa yakini kabisa, nyumba ya Akhera ndio bora zaidi kwa wanaomcha Allah. Je, hamtumii akili?



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 33

قَدۡ نَعۡلَمُ إِنَّهُۥ لَيَحۡزُنُكَ ٱلَّذِي يَقُولُونَۖ فَإِنَّهُمۡ لَا يُكَذِّبُونَكَ وَلَٰكِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ يَجۡحَدُونَ

Hakika, tunajua kuwa kwa yakini kabisa, yanakuhuzunisha mno yale wanayosema. Kwa hakika hawakupingi wewe, lakini madhalimu wanazipinga Aya za Allah



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 34

وَلَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَ فَصَبَرُواْ عَلَىٰ مَا كُذِّبُواْ وَأُوذُواْ حَتَّىٰٓ أَتَىٰهُمۡ نَصۡرُنَاۚ وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِ ٱللَّهِۚ وَلَقَدۡ جَآءَكَ مِن نَّبَإِيْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na kwa hakika kabisa, walipingwa Mitume wengi kabla yako, wakasubiri juu ya yale waliopingwa, na walifanyiwa maudhi hadi ulipowajia msaada wetu. Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Allah. Na kwa hakika kabisa, zimekujia baadhi ya habari za Mitume



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 35

وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيۡكَ إِعۡرَاضُهُمۡ فَإِنِ ٱسۡتَطَعۡتَ أَن تَبۡتَغِيَ نَفَقٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ سُلَّمٗا فِي ٱلسَّمَآءِ فَتَأۡتِيَهُم بِـَٔايَةٖۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَمَعَهُمۡ عَلَى ٱلۡهُدَىٰۚ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

Na kama umekwazwa sana na upinzani wao, basi kama utaweza kupata njia ya chini ya ardhi au ngazi upande mbinguni ili uwaletee Aya (zisizo kuwa hizi basi fanya). Na lau kama Allah angetaka, basi kwa hakika kabisa angewakusanya wote (wakawa) katika uongofu. Basi (acha kabisa) usiwe miongoni mwa wajinga