السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 175

وَأَبۡصِرۡهُمۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na watazame, nao wataona



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 176

أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ

Je! Wanaihimiza adhabu yetu?



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 177

فَإِذَا نَزَلَ بِسَاحَتِهِمۡ فَسَآءَ صَبَاحُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Basi itakapo shuka uwanjani kwao, itakuwa asubuhi mbaya kwa walio onywa



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 178

وَتَوَلَّ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ حِينٖ

Na waache kwa muda



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 179

وَأَبۡصِرۡ فَسَوۡفَ يُبۡصِرُونَ

Na tazama, na wao wataona



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 180

سُبۡحَٰنَ رَبِّكَ رَبِّ ٱلۡعِزَّةِ عَمَّا يَصِفُونَ

Subhana Rabbi’l’Izzat Ametakasika Mola Mlezi Mwenye enzi na yale wanayo mzulia



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 181

وَسَلَٰمٌ عَلَى ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na Salamu juu ya Mitume



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 182

وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sifa njema zote ni za Allah Mola Mlezi wa walimwengu wote



السورة: SWAAD 

الآية : 1

صٓۚ وَٱلۡقُرۡءَانِ ذِي ٱلذِّكۡرِ

Swaad. Nina apa kwa Qur’ani yenye mawaidha



السورة: SWAAD 

الآية : 2

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فِي عِزَّةٖ وَشِقَاقٖ

(Kwamba) Lakini waliokufuru wamo katika majivuno na upingaji



السورة: SWAAD 

الآية : 3

كَمۡ أَهۡلَكۡنَا مِن قَبۡلِهِم مِّن قَرۡنٖ فَنَادَواْ وَّلَاتَ حِينَ مَنَاصٖ

Ni (watu wa) karne yangapi tumewaangamiza kabla yao, na wakapiga kelele, lakini wakati wa kuokoka ulikwisha pita?



السورة: SWAAD 

الآية : 4

وَعَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٞ مِّنۡهُمۡۖ وَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا سَٰحِرٞ كَذَّابٌ

Na walistaajabu kuwajia muonyaji anayetokana nao wenyewe, na makafiri wakasema: Huyu ni mchawi, muongo sana



السورة: SWAAD 

الآية : 5

أَجَعَلَ ٱلۡأٓلِهَةَ إِلَٰهٗا وَٰحِدًاۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيۡءٌ عُجَابٞ

Hivi amewafanya Miungu wote kuwa Mungu Mmoja tu? Hakika hili ni jambo la ajabu sana!



السورة: SWAAD 

الآية : 6

وَٱنطَلَقَ ٱلۡمَلَأُ مِنۡهُمۡ أَنِ ٱمۡشُواْ وَٱصۡبِرُواْ عَلَىٰٓ ءَالِهَتِكُمۡۖ إِنَّ هَٰذَا لَشَيۡءٞ يُرَادُ

Na wakaondoka wakubwa wao wakiwaambia: Nendeni zenu na dumuni na miungu yenu, kwani hili ni jambo lililo pangwa



السورة: SWAAD 

الآية : 7

مَا سَمِعۡنَا بِهَٰذَا فِي ٱلۡمِلَّةِ ٱلۡأٓخِرَةِ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا ٱخۡتِلَٰقٌ

Sisi hatukusikia haya katika mila hii ya mwisho. Haya si chochote ila ni uzushi tu



السورة: SWAAD 

الآية : 8

أَءُنزِلَ عَلَيۡهِ ٱلذِّكۡرُ مِنۢ بَيۡنِنَاۚ بَلۡ هُمۡ فِي شَكّٖ مِّن ذِكۡرِيۚ بَل لَّمَّا يَذُوقُواْ عَذَابِ

Ati yeye tu ndiye aliye teremshiwa mawaidha peke yake katika sisi? Lakini hao wana shaka na mawaidha yangu, bali hawajaionja adhabu yangu



السورة: SWAAD 

الآية : 9

أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَحۡمَةِ رَبِّكَ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡوَهَّابِ

Au wanazo wao hazina za rehema za Mola wako Mlezi, Mwenye nguvu, Mpaji?



السورة: SWAAD 

الآية : 10

أَمۡ لَهُم مُّلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَاۖ فَلۡيَرۡتَقُواْ فِي ٱلۡأَسۡبَٰبِ

Au wao wana ufalme wa mbingu na ardhi na viliomo kati yao? Basi nawazipande njia za kwendea huko!



السورة: SWAAD 

الآية : 11

جُندٞ مَّا هُنَالِكَ مَهۡزُومٞ مِّنَ ٱلۡأَحۡزَابِ

Hao ni askari watakao shindwa miongoni mwa makundi yatakayo shindwa



السورة: SWAAD 

الآية : 12

كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ وَعَادٞ وَفِرۡعَوۡنُ ذُو ٱلۡأَوۡتَادِ

Walikanusha kabla yao watu wa Nuhu, na kina A’adi na Firauni mwenye majengo



السورة: SWAAD 

الآية : 13

وَثَمُودُ وَقَوۡمُ لُوطٖ وَأَصۡحَٰبُ لۡـَٔيۡكَةِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡأَحۡزَابُ

Na Thamud na watu wa Lutwi na watu wa Machakani. Hayo ndiyo makundi



السورة: SWAAD 

الآية : 14

إِن كُلٌّ إِلَّا كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ عِقَابِ

Hao wote waliwakadhibisha Mitume; basi wakastahiki adhabu yangu



السورة: SWAAD 

الآية : 15

وَمَا يَنظُرُ هَـٰٓؤُلَآءِ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ مَّا لَهَا مِن فَوَاقٖ

Na hawa hawangojei ila ukelele mmoja tu usio na muda



السورة: SWAAD 

الآية : 16

وَقَالُواْ رَبَّنَا عَجِّل لَّنَا قِطَّنَا قَبۡلَ يَوۡمِ ٱلۡحِسَابِ

Na wao husema: Mola wetu Mlezi! Tuletee upesi sehemu yetu ya adhabu kabla ya Siku ya Hesabu



السورة: SWAAD 

الآية : 17

ٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَٱذۡكُرۡ عَبۡدَنَا دَاوُۥدَ ذَا ٱلۡأَيۡدِۖ إِنَّهُۥٓ أَوَّابٌ

Subiri kwa hayo wayasemayo, na umkumbuke mja wetu Daudi, mwenye nguvu. Hakika yeye alikuwa mwingi wa kutubia



السورة: SWAAD 

الآية : 18

إِنَّا سَخَّرۡنَا ٱلۡجِبَالَ مَعَهُۥ يُسَبِّحۡنَ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِشۡرَاقِ

Hakika tuliidhalilisha milima pamoja naye ikisabihi (ikamtakasa Allah) jioni na asubuhi pamoja naye



السورة: SWAAD 

الآية : 19

وَٱلطَّيۡرَ مَحۡشُورَةٗۖ كُلّٞ لَّهُۥٓ أَوَّابٞ

Na pia ndege walio kusanywa makundi kwa makundi; wote walikuwa wanyenyekevu kwake



السورة: SWAAD 

الآية : 20

وَشَدَدۡنَا مُلۡكَهُۥ وَءَاتَيۡنَٰهُ ٱلۡحِكۡمَةَ وَفَصۡلَ ٱلۡخِطَابِ

Na tukautia nguvu ufalme wake, na tukampa hekima, na kukata hukumu



السورة: SWAAD 

الآية : 21

۞وَهَلۡ أَتَىٰكَ نَبَؤُاْ ٱلۡخَصۡمِ إِذۡ تَسَوَّرُواْ ٱلۡمِحۡرَابَ

Na je! Imekufikia habari ya wagombanao walipo pindukia ukuta kuingia chumbani?



السورة: SWAAD 

الآية : 22

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَىٰ دَاوُۥدَ فَفَزِعَ مِنۡهُمۡۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ خَصۡمَانِ بَغَىٰ بَعۡضُنَا عَلَىٰ بَعۡضٖ فَٱحۡكُم بَيۡنَنَا بِٱلۡحَقِّ وَلَا تُشۡطِطۡ وَٱهۡدِنَآ إِلَىٰ سَوَآءِ ٱلصِّرَٰطِ

Walipoingia kwa Daudi, naye akawaogopa. Wakasema: Usiogope! Sisi ni wagombanao wawili, mmoja wetu amemdhulumu mwenziwe. Basi tuhukumu kwa haki, wala usipendelee. Na utuongoe kwenye njia iliyo sawa