سَيَصۡلَىٰ نَارٗا ذَاتَ لَهَبٖ
Atauingia moto wenye muwako
وَٱمۡرَأَتُهُۥ حَمَّالَةَ ٱلۡحَطَبِ
(Ataingia Motoni yeye) Na mkewe, mchukuzi mkubwa wa kuni
فِي جِيدِهَا حَبۡلٞ مِّن مَّسَدِۭ
Shingoni mwake iko kamba ya kusokotwa
قُلۡ هُوَ ٱللَّهُ أَحَدٌ
Sema: Yeye Allah ni wa pekee
ٱللَّهُ ٱلصَّمَدُ
Allah ndiye tu Mkusudiwa (katika kuabudiwa, kutegemewa na kutatua shida za watu)
لَمۡ يَلِدۡ وَلَمۡ يُولَدۡ
Hakuzaa[1] na hakuzaliwa.[2]
1- - Kwa maana hiyo hana mtoto.
2- - Kwa maana hiyo hana baba wala mama.
---------------
------------------------------------------------------------
---------------
------------------------------------------------------------
وَلَمۡ يَكُن لَّهُۥ كُفُوًا أَحَدُۢ
Na hakuna yeyote anaye fanana naye
قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلۡفَلَقِ
Sema: Najikinga kwa Mola Mlezi wa mapambazuko
مِن شَرِّ مَا خَلَقَ
(Najikinga) Dhidi ya shari ya alivyoviumba
وَمِن شَرِّ غَاسِقٍ إِذَا وَقَبَ
Na (najikinga) dhidi ya shari ya giza la usiku liingiapo
وَمِن شَرِّ ٱلنَّفَّـٰثَٰتِ فِي ٱلۡعُقَدِ
Na (najikinga) dhidi ya shari ya (wanawake) wanaopulizia mafundoni
وَمِن شَرِّ حَاسِدٍ إِذَا حَسَدَ
Na (najikinga) dhidi ya shari ya hasidi anapo husudu
قُلۡ أَعُوذُ بِرَبِّ ٱلنَّاسِ
Sema: Ninajikinga kwa Mola Mlezi wa watu
مَلِكِ ٱلنَّاسِ
Mfalme wa watu
إِلَٰهِ ٱلنَّاسِ
Muabudiwa wa haki wa watu (Mwenye haki ya kuabudiwa na watu)
مِن شَرِّ ٱلۡوَسۡوَاسِ ٱلۡخَنَّاسِ
(Najilinda dhidi ya shari ya (shetani) mwenye kutia wasiwasi, mwenye kurejea nyuma
ٱلَّذِي يُوَسۡوِسُ فِي صُدُورِ ٱلنَّاسِ
Anayetia wasiwasi katika vifua vya watu
مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ
(Shetani) Anayetokana na majini na watu