السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 1

الٓمٓ

Alif Laam Miim[1]


1- - Allah ndiye ajuwaye zaidi madhumuni ya herufi hizi.


السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 2

ذَٰلِكَ ٱلۡكِتَٰبُ لَا رَيۡبَۛ فِيهِۛ هُدٗى لِّلۡمُتَّقِينَ

Kitabu hiki hakina shaka. Ni muongozo kwa Wacha Mungu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 3

ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡغَيۡبِ وَيُقِيمُونَ ٱلصَّلَوٰةَ وَمِمَّا رَزَقۡنَٰهُمۡ يُنفِقُونَ

Ambao wanaamini Ghaibu na wanasimamisha swala na baadhi ya tulivyowapa wanatoa



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 4

وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَ وَمَآ أُنزِلَ مِن قَبۡلِكَ وَبِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ يُوقِنُونَ

Na ambao wanaamini yale tuliyoyateremsha kwako na yale tuliyoyateremsha kabla yako, na ambao wanaamini Akhera



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 5

أُوْلَـٰٓئِكَ عَلَىٰ هُدٗى مِّن رَّبِّهِمۡۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Hao wako juu ya muongozo utokao kwa Mola wao, na hao tu ndio waliofaulu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 6

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡهِمۡ ءَأَنذَرۡتَهُمۡ أَمۡ لَمۡ تُنذِرۡهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hakika, waliokufuru, ni sawa kwao umewahadharisha au hukuwahadharisha; hawaamini



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 7

خَتَمَ ٱللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ وَعَلَىٰ سَمۡعِهِمۡۖ وَعَلَىٰٓ أَبۡصَٰرِهِمۡ غِشَٰوَةٞۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Allah amefunga nyoyo zao na usikivu wao, na katika uonaji wao kuna kifuniko, na watastahiki adhabu kubwa



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 8

وَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَبِٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَمَا هُم بِمُؤۡمِنِينَ

Na miongoni mwa watu wapo wanaosema[1] kuwa: “Tumemuamini Allah na Siku ya Mwisho” na[2] sio waumini (wa kweli)


1- - Kwa maneno tu.


2- - Ukweli ni kwamba…


السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 9

يُخَٰدِعُونَ ٱللَّهَ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَمَا يَخۡدَعُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Wanamhadaa Allah na wale walioamini. Na hawahadai isipokuwa nafsi zao tu na wao hawatambui



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 10

فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ فَزَادَهُمُ ٱللَّهُ مَرَضٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡذِبُونَ

Ndani ya nyoyo zao kuna ugonjwa, na Allah akawaongezea ugonjwa. Na wanastahiki adhabu kali kwa uongo waliokuwa wanaufanya



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 11

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَا تُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ قَالُوٓاْ إِنَّمَا نَحۡنُ مُصۡلِحُونَ

Na wanapoambiwa msifanye uharibifu ardhini wanasema: Hapana, bali sisi niwafanyaji mazuri



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 12

أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلۡمُفۡسِدُونَ وَلَٰكِن لَّا يَشۡعُرُونَ

Elewa! Kwa yakini, wao ndio waharibifu hasa na lakini hawatambui



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 13

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ ءَامِنُواْ كَمَآ ءَامَنَ ٱلنَّاسُ قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ كَمَآ ءَامَنَ ٱلسُّفَهَآءُۗ أَلَآ إِنَّهُمۡ هُمُ ٱلسُّفَهَآءُ وَلَٰكِن لَّا يَعۡلَمُونَ

Na wanapoambiwa: Kuweni wenye kuamini kama walivyoamini watu, wanasema: Ah! Hivi tuamini kama walivyoamini wapumbavu? Elewa! Wao ndio wapumbavu hasa na lakini hawajui



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 14

وَإِذَا لَقُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَإِذَا خَلَوۡاْ إِلَىٰ شَيَٰطِينِهِمۡ قَالُوٓاْ إِنَّا مَعَكُمۡ إِنَّمَا نَحۡنُ مُسۡتَهۡزِءُونَ

Na wanapokutana na walioamini wanasema: Tumeamini. Na wanapokuwa faragha na mashetani wao wanasema: Sisi tuko pamoja nanyi, tunachokifanya sisi tunacheza shere tu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 15

ٱللَّهُ يَسۡتَهۡزِئُ بِهِمۡ وَيَمُدُّهُمۡ فِي طُغۡيَٰنِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

Allah anawacheza shere wao, na anawapa muda zaidi katika kupotoka kwao huku wakiwa wanatangatanga



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 16

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلضَّلَٰلَةَ بِٱلۡهُدَىٰ فَمَا رَبِحَت تِّجَٰرَتُهُمۡ وَمَا كَانُواْ مُهۡتَدِينَ

Hao ndio walioununua upotevu kwa uongofu. Biashara yao haikuleta faida, na hawakuwa waongofu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 17

مَثَلُهُمۡ كَمَثَلِ ٱلَّذِي ٱسۡتَوۡقَدَ نَارٗا فَلَمَّآ أَضَآءَتۡ مَا حَوۡلَهُۥ ذَهَبَ ٱللَّهُ بِنُورِهِمۡ وَتَرَكَهُمۡ فِي ظُلُمَٰتٖ لَّا يُبۡصِرُونَ

Mfano wao ni kama mfano wa mtu aliyewasha moto. Kila moto ulipomuangazia maeneo yanayomzunguka, Allah akaondoa mwanga wao na kuwaacha katika kiza kinene; hawaoni



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 18

صُمُّۢ بُكۡمٌ عُمۡيٞ فَهُمۡ لَا يَرۡجِعُونَ

Ni viziwi, mabubu, vipofu. Kwa sababu hiyo, hawarudi



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 19

أَوۡ كَصَيِّبٖ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فِيهِ ظُلُمَٰتٞ وَرَعۡدٞ وَبَرۡقٞ يَجۡعَلُونَ أَصَٰبِعَهُمۡ فِيٓ ءَاذَانِهِم مِّنَ ٱلصَّوَٰعِقِ حَذَرَ ٱلۡمَوۡتِۚ وَٱللَّهُ مُحِيطُۢ بِٱلۡكَٰفِرِينَ

Au ni kama mvua iteremkayo kwa kasi kutoka mawinguni, ndani yake mna kiza kinene na radi na umeme wanaweka vidole vyao masikioni mwao kutokana na radi kwa kuhadhari kifo. Na Allah amewazunguka makafiri wote



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 20

يَكَادُ ٱلۡبَرۡقُ يَخۡطَفُ أَبۡصَٰرَهُمۡۖ كُلَّمَآ أَضَآءَ لَهُم مَّشَوۡاْ فِيهِ وَإِذَآ أَظۡلَمَ عَلَيۡهِمۡ قَامُواْۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَذَهَبَ بِسَمۡعِهِمۡ وَأَبۡصَٰرِهِمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Umeme unakaribia kupofoa macho yao. Kila unapowaangazia wanatembea katika mwanga huo, na pale unapowazimikia wanasimama. Na kama Allah angelitaka basi, kwa yakini kabisa, angeondoa kusikia kwao na macho yao. Hakika, Allah ni muweza wa kila kitu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 21

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱعۡبُدُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ

Enyi watu, muabuduni Mola wenu ambaye amekuumbeni na (ameumba) waliokuwepo kabla yenu ili muwe Wacha Mungu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 22

ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ فِرَٰشٗا وَٱلسَّمَآءَ بِنَآءٗ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجَ بِهِۦ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ رِزۡقٗا لَّكُمۡۖ فَلَا تَجۡعَلُواْ لِلَّهِ أَندَادٗا وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Ambaye amekuumbieni ardhi ikiwa imetandazwa, na mbingu ikiwa sakafu na ameteremsha kutoka mawinguni maji (mvua), akatoa kwa maji hayo riziki zenu kutoka kwenye matunda. Basi msimfanyie Allah washirika ilihali mnajua (kuwa Allah hana mshirika)



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 23

وَإِن كُنتُمۡ فِي رَيۡبٖ مِّمَّا نَزَّلۡنَا عَلَىٰ عَبۡدِنَا فَأۡتُواْ بِسُورَةٖ مِّن مِّثۡلِهِۦ وَٱدۡعُواْ شُهَدَآءَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na ikiwa mna shaka na kile tulichomteremshia mja wetu, basi leteni Sura (moja tu) iliyo mithili yake, na waleteni mashahidi wenu badala ya Allah ikiwa nyinyi ni wa kweli



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 24

فَإِن لَّمۡ تَفۡعَلُواْ وَلَن تَفۡعَلُواْ فَٱتَّقُواْ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُۖ أُعِدَّتۡ لِلۡكَٰفِرِينَ

Na msipofanya (hivyo) na kamwe hamtaweza kufanya (hivyo), basi uogopeni Moto ambao nishati yake ni watu na mawe, ulioandaliwa kwa ajili ya makafiri



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 25

وَبَشِّرِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أَنَّ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ كُلَّمَا رُزِقُواْ مِنۡهَا مِن ثَمَرَةٖ رِّزۡقٗا قَالُواْ هَٰذَا ٱلَّذِي رُزِقۡنَا مِن قَبۡلُۖ وَأُتُواْ بِهِۦ مُتَشَٰبِهٗاۖ وَلَهُمۡ فِيهَآ أَزۡوَٰجٞ مُّطَهَّرَةٞۖ وَهُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wape bishara wale walioamini na kufanya matendo mema kuwa, watapata bustani zitiririkazo mito chini yake. Kila wanapopewa riziki ya matunda humo wanasema: Hii ndio ile riziki tuliyopewa kabla. Na wamepewa riziki hiyo ikiwa inafanana. Na watapata humo wake waliotwaharishwa, na watabaki humo daima



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 26

۞إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَسۡتَحۡيِۦٓ أَن يَضۡرِبَ مَثَلٗا مَّا بَعُوضَةٗ فَمَا فَوۡقَهَاۚ فَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ فَيَعۡلَمُونَ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّهِمۡۖ وَأَمَّا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَيَقُولُونَ مَاذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِهَٰذَا مَثَلٗاۘ يُضِلُّ بِهِۦ كَثِيرٗا وَيَهۡدِي بِهِۦ كَثِيرٗاۚ وَمَا يُضِلُّ بِهِۦٓ إِلَّا ٱلۡفَٰسِقِينَ

Hakika, Allah haoni aibu kutoa mfano wowote; wa mbu na (mfano) zaidi (ya mbu). Ama walioamini wanajua kuwa mfano huo ni haki kutoka kwa Mola wao. Na ama waliokufuru, wanasema kuwa: Allah amekusudia nini kwa mfano huu? Allah, kwa mfano huu, anawaacha wengi wapotee na anawaongoza wengi. Na (Allah) hawaachi kupotea kwa mfano huu isipokuwa waovu tu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 27

ٱلَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهۡدَ ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مِيثَٰقِهِۦ وَيَقۡطَعُونَ مَآ أَمَرَ ٱللَّهُ بِهِۦٓ أَن يُوصَلَ وَيُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Ambao wana vunja ahadi za Allah baada ya kuwekwa, na wanakataa alichoamuru Allah kiungwe, na wanafanya uharibifu ardhini. Hao tu ndio wenye hasara



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 28

كَيۡفَ تَكۡفُرُونَ بِٱللَّهِ وَكُنتُمۡ أَمۡوَٰتٗا فَأَحۡيَٰكُمۡۖ ثُمَّ يُمِيتُكُمۡ ثُمَّ يُحۡيِيكُمۡ ثُمَّ إِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Vipi mnamkufuru Allah, na ilhali mlikuwa wafu akakupeni uhai? Kisha atakufisheni, kisha atakupeni uhai. Na kisha ni kwake tu ndiko mtakakorejeshwa



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 29

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰٓ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَسَوَّىٰهُنَّ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖۚ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Ni yeye tu aliye kuumbieni vyote vilivyomo ardhini. Kisha akakusudia mbingu na kuziumba zikiwa mbingu saba zilizo sawa. Na yeye ni mjuzi wa kila kitu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 30

وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّي جَاعِلٞ فِي ٱلۡأَرۡضِ خَلِيفَةٗۖ قَالُوٓاْ أَتَجۡعَلُ فِيهَا مَن يُفۡسِدُ فِيهَا وَيَسۡفِكُ ٱلدِّمَآءَ وَنَحۡنُ نُسَبِّحُ بِحَمۡدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَۖ قَالَ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na (kumbuka) Mola wako alipowaambia Malaika kuwa: Kwa yakini, mimi nitamuweka Khalifa ardhini. Wakasema: Hivi unamuweka humo atakayefanya uharibifu humo na kumwaga damu, na wakati sisi tunakutakasa kwa kukusifu? (Allah) Akasema: Mimi ninajua msichokijua