السورة: AL-AARAAF 

الآية : 91

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلرَّجۡفَةُ فَأَصۡبَحُواْ فِي دَارِهِمۡ جَٰثِمِينَ

Basi likawachukua tetemeko (la ardhi) wakawa wameangamia majumbani mwao huku wamepiga magoti



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 92

ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ شُعَيۡبٗا كَأَن لَّمۡ يَغۡنَوۡاْ فِيهَاۚ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ شُعَيۡبٗا كَانُواْ هُمُ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Ambao wamemkadhibisha (wamempinga) Shuaibu (waliangamia na kutoweka majumbani mwao) kama vile hawakuwemo kabisa humo. Ambao walimkadhibisha Shuaibu walikuwa hasa ndio wenye hasara



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 93

فَتَوَلَّىٰ عَنۡهُمۡ وَقَالَ يَٰقَوۡمِ لَقَدۡ أَبۡلَغۡتُكُمۡ رِسَٰلَٰتِ رَبِّي وَنَصَحۡتُ لَكُمۡۖ فَكَيۡفَ ءَاسَىٰ عَلَىٰ قَوۡمٖ كَٰفِرِينَ

Basi (Shuaibu) aliachana nao (aliwapuuza) na kuwaambia: Enyi watu wangu, kwa hakika kabisa, nimewafikishieni ujumbe wa Mola wangu na nimekupeni nasaha. Basi inakuwaje niwasikitikie watu makafiri?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 94

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا فِي قَرۡيَةٖ مِّن نَّبِيٍّ إِلَّآ أَخَذۡنَآ أَهۡلَهَا بِٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ لَعَلَّهُمۡ يَضَّرَّعُونَ

Na hatukumpeleka Mtume yeyote katika mji wowote isipokuwa kwamba tuliwashikisha adabu watu wake kwa mateso na shida ili wapate kunyenyekea



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 95

ثُمَّ بَدَّلۡنَا مَكَانَ ٱلسَّيِّئَةِ ٱلۡحَسَنَةَ حَتَّىٰ عَفَواْ وَّقَالُواْ قَدۡ مَسَّ ءَابَآءَنَا ٱلضَّرَّآءُ وَٱلسَّرَّآءُ فَأَخَذۡنَٰهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ

Kisha tulibadilisha sehemu ya baya tukaweka zuri mpaka wakaneemeka (na neema zilipowazidi) na wakasema: Ziliwapata baba zetu shida na raha, kwa sababu hiyo, tuliwashika (tuliwaadhibu) ghafla na ilhali hawatambui



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 96

وَلَوۡ أَنَّ أَهۡلَ ٱلۡقُرَىٰٓ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَفَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَرَكَٰتٖ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلَٰكِن كَذَّبُواْ فَأَخَذۡنَٰهُم بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Na lau kama watu wa miji wangeamini na kumcha Allah tungewafungulia baraka nyingi kutoka mbinguni na ardhini na lakini wamekadhibisha kwa sababu hiyo tumewashikisha adabu kwa sababu ya yale waliyokuwa wanayachuma (wanayafanya)



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 97

أَفَأَمِنَ أَهۡلُ ٱلۡقُرَىٰٓ أَن يَأۡتِيَهُم بَأۡسُنَا بَيَٰتٗا وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Hivi watu wa miji wamejia-minisha kwamba haitawajia adhabu yetu usiku na ilhali wamelala?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 98

أَوَأَمِنَ أَهۡلُ ٱلۡقُرَىٰٓ أَن يَأۡتِيَهُم بَأۡسُنَا ضُحٗى وَهُمۡ يَلۡعَبُونَ

Au watu wa miji wamejiaminisha kwamba haitawajia adhabu yetu mchana na ilhali wanacheza?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 99

أَفَأَمِنُواْ مَكۡرَ ٱللَّهِۚ فَلَا يَأۡمَنُ مَكۡرَ ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Hivi wamejiaminisha vitimbi vya Allah? Basi hawajiaminishi vitimbi vya Allah isipokuwa tu watu wenye hasara



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 100

أَوَلَمۡ يَهۡدِ لِلَّذِينَ يَرِثُونَ ٱلۡأَرۡضَ مِنۢ بَعۡدِ أَهۡلِهَآ أَن لَّوۡ نَشَآءُ أَصَبۡنَٰهُم بِذُنُوبِهِمۡۚ وَنَطۡبَعُ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَهُمۡ لَا يَسۡمَعُونَ

Hivi haijawa muongozo kwa wale wanaoirithi ardhi baada ya watu wake (walioangamizwa) kwamba lau tungetaka tungewapa msiba (mitihani na matatizo) kwa sababu ya madhambi yao, na tungepiga lakiri katika nyoyo zao wakawa hawasikii?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 101

تِلۡكَ ٱلۡقُرَىٰ نَقُصُّ عَلَيۡكَ مِنۡ أَنۢبَآئِهَاۚ وَلَقَدۡ جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَمَا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُواْ بِمَا كَذَّبُواْ مِن قَبۡلُۚ كَذَٰلِكَ يَطۡبَعُ ٱللَّهُ عَلَىٰ قُلُوبِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Hiyo ni miji tunakusimulia miongoni mwa habari zake. Na kwa hakika kabisa, Mitume wao waliwajia na hoja za wazi wazi. Basi hawakuyaamini yale waliyoyakadhibisha hapo kabla. Kama hivyo Allah anazipiga lakini nyoyo za makafiri



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 102

وَمَا وَجَدۡنَا لِأَكۡثَرِهِم مِّنۡ عَهۡدٖۖ وَإِن وَجَدۡنَآ أَكۡثَرَهُمۡ لَفَٰسِقِينَ

Na hatukupata kwa wengi wao (utekelezaji wa) ahadi yoyote na hakika kabisa, tumekuta wengi wao ni waovu



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 103

ثُمَّ بَعَثۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِم مُّوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَظَلَمُواْ بِهَاۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Kisha tulimtuma Musa kwa Aya zetu baada yao, aende kwa Firauni na kundi lake la mamwinyi, basi wakazidhulumu (wakazipinga) Aya hizo. Basi ona namna ulivyokuwa mwisho wa waharibifu



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 104

وَقَالَ مُوسَىٰ يَٰفِرۡعَوۡنُ إِنِّي رَسُولٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na Musa akasema: Ewe Firauni, hakika mimi ni Mtume kutoka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 105

حَقِيقٌ عَلَىٰٓ أَن لَّآ أَقُولَ عَلَى ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡحَقَّۚ قَدۡ جِئۡتُكُم بِبَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ فَأَرۡسِلۡ مَعِيَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Ni haki kwangu kutomsemea Allah ila lile la haki tu. Hakika, nimekujieni na hoja za wazi kutoka kwa Mola wenu Mlezi (zinazothibitisha ukweli wangu). Basi waachie Wana wa Israili (wawe huru) wawe pamoja na mimi (kwenda kwenye mji wa baba zao)



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 106

قَالَ إِن كُنتَ جِئۡتَ بِـَٔايَةٖ فَأۡتِ بِهَآ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

(Firauni) Akasema: Kama umekuja na hoja basi ilete kama wewe ni miongoni mwa wasemao kweli



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 107

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi (Musa) akaitupa chini fimbo yake na ghafla ikawa nyoka wa dhahiri



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 108

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa kwa nguvu mkono wake (kutoka katika nguo yake) na ghafla ukawa mweupe kwa wanaotazama



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 109

قَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِ فِرۡعَوۡنَ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

Mamwinyi katika watu wa Firauni wakasema: Hakika, huyu ni mchawi mjuzi sana



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 110

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُمۡۖ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika ardhi (nchi) yenu (kwa uchawi wake). Basi mnaniamuru (mnanishauri nifanye) nini?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 111

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَأَرۡسِلۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye (Musa) na ndugu yake na tuma katika miji yote (watu) watakaofanya kazi ya kukusanya (wachawi)



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 112

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَٰحِرٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi mahiri sana



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 113

وَجَآءَ ٱلسَّحَرَةُ فِرۡعَوۡنَ قَالُوٓاْ إِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Na wachawi walikuja kwa Firauni wakasema: Hivi sisi tutalipwa endapo tutashinda?



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 114

قَالَ نَعَمۡ وَإِنَّكُمۡ لَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

(Firauni) Akasema: Ndio, na kwa hakika kabisa, nyinyi mtakuwa miongoni mwa watu wangu wa karibu sana



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 115

قَالُواْ يَٰمُوسَىٰٓ إِمَّآ أَن تُلۡقِيَ وَإِمَّآ أَن نَّكُونَ نَحۡنُ ٱلۡمُلۡقِينَ

(Wachawi) Wakasema: Ewe Musa, ama tupa (toa wewe uchawi wako) au sisi tuwe wa mwanzo kutupa (kutoa)



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 116

قَالَ أَلۡقُواْۖ فَلَمَّآ أَلۡقَوۡاْ سَحَرُوٓاْ أَعۡيُنَ ٱلنَّاسِ وَٱسۡتَرۡهَبُوهُمۡ وَجَآءُو بِسِحۡرٍ عَظِيمٖ

(Musa) Akasema: Tupeni (Toeni). (Wachawi) Walipotupa (walipotoa uchawi wao) waliyaroga macho ya watu na waliwatisha na walikuja na uchawi mkubwa sana!



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 117

۞وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنۡ أَلۡقِ عَصَاكَۖ فَإِذَا هِيَ تَلۡقَفُ مَا يَأۡفِكُونَ

Na tulimfunulia Musa Wahyi kwamba: Tupa fimbo yako, na ghafla ikawa inameza vyote wanavyovizusha



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 118

فَوَقَعَ ٱلۡحَقُّ وَبَطَلَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Basi haki ikathibiti na vikabatilika vyote walivyokuwa wanafanya



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 119

فَغُلِبُواْ هُنَالِكَ وَٱنقَلَبُواْ صَٰغِرِينَ

Basi (wachawi) hapo wakashindwa na wakabadilika wakawa wanyonge!



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 120

وَأُلۡقِيَ ٱلسَّحَرَةُ سَٰجِدِينَ

Na wachawi wakaporomoka chini kumsujudia (Allah)