السورة: ANNISAI 

الآية : 61

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ وَإِلَى ٱلرَّسُولِ رَأَيۡتَ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ يَصُدُّونَ عَنكَ صُدُودٗا

Na wanapoambiwa: Njooni kwenye yale aliyoyateremsha Allah na (njooni) kwa Mtume, utawaona wanafiki wanakuwekea pingamizi nyingi



السورة: ANNISAI 

الآية : 62

فَكَيۡفَ إِذَآ أَصَٰبَتۡهُم مُّصِيبَةُۢ بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡ ثُمَّ جَآءُوكَ يَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ إِنۡ أَرَدۡنَآ إِلَّآ إِحۡسَٰنٗا وَتَوۡفِيقًا

Basi itakuwaje msiba utakapowafika kwasababu ya yale yaliyotangulia kufanywa na mikono yao, kisha wakakujia huku wakiapa kwa Allah kwamba: Hatukukusudia ila tu kufanya yaliyo mazuri na kupatanisha?



السورة: ANNISAI 

الآية : 63

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ يَعۡلَمُ ٱللَّهُ مَا فِي قُلُوبِهِمۡ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَعِظۡهُمۡ وَقُل لَّهُمۡ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ قَوۡلَۢا بَلِيغٗا

Hao ndio ambao Allah anayajua yaliyomo ndani ya nyoyo zao. Basi wapuuze na wape mawaidha na waambie katika nafsi zao maneno mazito



السورة: ANNISAI 

الآية : 64

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا مِن رَّسُولٍ إِلَّا لِيُطَاعَ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَلَوۡ أَنَّهُمۡ إِذ ظَّلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ جَآءُوكَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ ٱللَّهَ وَٱسۡتَغۡفَرَ لَهُمُ ٱلرَّسُولُ لَوَجَدُواْ ٱللَّهَ تَوَّابٗا رَّحِيمٗا

Na hatukumtuma Mtume yeyote ila tu atiiwe kwa idhini ya Allah. Na lau kama walipozidhulumu nafsi zao (kwa kutenda dhambi) wangelikujia wakamuomba msamaha Allah, na Mtume (naye) akawaombea msamaha, kwa yakini kabisa, wangemkuta Allah ni Mwenye kupokea toba na Mwenye kurehemu



السورة: ANNISAI 

الآية : 65

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤۡمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيۡنَهُمۡ ثُمَّ لَا يَجِدُواْ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ حَرَجٗا مِّمَّا قَضَيۡتَ وَيُسَلِّمُواْ تَسۡلِيمٗا

Hapana; nina apa kwa Mola wako kwamba, (watu) hawawi waumini mpaka wakufanye wewe kuwa muamuzi katika migogoro inayotokea baina yao, kisha wasihisi uzito wowote (au mashaka) katika nafsi zao kutokana na hukumu uliyoitoa na waonyeshe utiifu kamili



السورة: ANNISAI 

الآية : 66

وَلَوۡ أَنَّا كَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ أَنِ ٱقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ أَوِ ٱخۡرُجُواْ مِن دِيَٰرِكُم مَّا فَعَلُوهُ إِلَّا قَلِيلٞ مِّنۡهُمۡۖ وَلَوۡ أَنَّهُمۡ فَعَلُواْ مَا يُوعَظُونَ بِهِۦ لَكَانَ خَيۡرٗا لَّهُمۡ وَأَشَدَّ تَثۡبِيتٗا

Na lau tungewaandikia (tungewawajibishia) kuwa: Jiueni au tokeni majumbani mwenu, wasingefanya hivyo ila wachache tu miongoni mwao. Na lau kama wangefanya wanayo waidhiwa kwa yakini kabisa ingekuwa bora kwao na madhubuti sana



السورة: ANNISAI 

الآية : 67

وَإِذٗا لَّأٓتَيۡنَٰهُم مِّن لَّدُنَّآ أَجۡرًا عَظِيمٗا

Na pia tungewapa malipo makubwa sana kutoka kwetu



السورة: ANNISAI 

الآية : 68

وَلَهَدَيۡنَٰهُمۡ صِرَٰطٗا مُّسۡتَقِيمٗا

Na tungewaongoza njia iliyo nyooka



السورة: ANNISAI 

الآية : 69

وَمَن يُطِعِ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَعَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلصِّدِّيقِينَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَٱلصَّـٰلِحِينَۚ وَحَسُنَ أُوْلَـٰٓئِكَ رَفِيقٗا

Na wenye kumtii Allah na Mtume, basi hao watakuwa pamoja na wale ambao Allah amewaneemesha ikiwa ni pamoja na Manabii na Wenye kusadikisha (Maswahaba) na Mashahidi na Watu Wema.[1] Na ni uzuri ulioje kuwa pamoja na watu hao!


1- - Aya hapa inawabainisha walioneemeshwa na ambao katika Aya ya 6 na ya 7 ya Sura Alfaatiha (1) Waislamu wametakiwa kuwaiga na kufuata njia, muongozo na sera zao. Swahaba, wakiongozwa na Abubakar, Umar, Uthman na Ali (Allah awawie radhi) wanahusika katika Aya hii kwa sababu kuna Hadithi kadhaa za Mtume (Allah amshushie rehema na amani, zinazowataja kuwa wamo Mashahidi na Wasadikishaji.


السورة: ANNISAI 

الآية : 70

ذَٰلِكَ ٱلۡفَضۡلُ مِنَ ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ عَلِيمٗا

Fadhila hizo[1] zinatoka kwa Allah. Na inatosha kwamba Allah ni Mjuzi (wa kila jambo)


1- - Ngawira, ukombozi na ushindi.


السورة: ANNISAI 

الآية : 71

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ خُذُواْ حِذۡرَكُمۡ فَٱنفِرُواْ ثُبَاتٍ أَوِ ٱنفِرُواْ جَمِيعٗا

Enyi mbao mmeamini, chukueni tahadhari yenu. Kwa hiyo, tokeni (kwenda vitani) kwa vikosi au (tokeni) nyote kwa pamoja



السورة: ANNISAI 

الآية : 72

وَإِنَّ مِنكُمۡ لَمَن لَّيُبَطِّئَنَّ فَإِنۡ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَالَ قَدۡ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيَّ إِذۡ لَمۡ أَكُن مَّعَهُمۡ شَهِيدٗا

Na hakika kabisa, wapo miongoni mwenu wanaosuasua (wanaobaki nyuma kwasababu ya kuona uzito wa kutoka kwenda vitani). Ukikupateni msiba wanasema: Hakika, Allah amenineemesha kwa kuwa sikuwa pamoja nao



السورة: ANNISAI 

الآية : 73

وَلَئِنۡ أَصَٰبَكُمۡ فَضۡلٞ مِّنَ ٱللَّهِ لَيَقُولَنَّ كَأَن لَّمۡ تَكُنۢ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُۥ مَوَدَّةٞ يَٰلَيۡتَنِي كُنتُ مَعَهُمۡ فَأَفُوزَ فَوۡزًا عَظِيمٗا

Na ikikufikieni fadhila itokayo kwa Allah kwa hakika kabisa husema, kama vile hapakuwa na mapenzi yoyote baina yenu na baina yao, kwamba: Laiti nami ningekuwa pamoja nao nikafanikiwa mafanikio makubwa



السورة: ANNISAI 

الآية : 74

۞فَلۡيُقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ يَشۡرُونَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا بِٱلۡأٓخِرَةِۚ وَمَن يُقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ فَيُقۡتَلۡ أَوۡ يَغۡلِبۡ فَسَوۡفَ نُؤۡتِيهِ أَجۡرًا عَظِيمٗا

Basi wapigane katika njia ya Allah wale ambao wanauza uhai (wao) wa duniani kwa Akhera. Na yeyote anayepigana katika njia ya Allah kisha akauliwa au akashinda, basi ni punde tu tutampa malipo makubwa



السورة: ANNISAI 

الآية : 75

وَمَا لَكُمۡ لَا تُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَٱلۡمُسۡتَضۡعَفِينَ مِنَ ٱلرِّجَالِ وَٱلنِّسَآءِ وَٱلۡوِلۡدَٰنِ ٱلَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَآ أَخۡرِجۡنَا مِنۡ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِ ٱلظَّالِمِ أَهۡلُهَا وَٱجۡعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ وَلِيّٗا وَٱجۡعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ نَصِيرًا

Na mna nini nyinyi hampigani katika njia ya Allah na ilhali wapo wanaume na wanawake na watoto wanao onewa (na) ambao wanasema: Ewe Mola wetu, tutoe katika mji huu ambao watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi atokaye kwako na tujaalie kutoka kwako wa kutunusuru



السورة: ANNISAI 

الآية : 76

ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۖ وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِ ٱلطَّـٰغُوتِ فَقَٰتِلُوٓاْ أَوۡلِيَآءَ ٱلشَّيۡطَٰنِۖ إِنَّ كَيۡدَ ٱلشَّيۡطَٰنِ كَانَ ضَعِيفًا

Walioamini wanapigana katika njia ya Allah, na waliokufuru wanapigana katika njia ya Twaghuti. Basi wapigeni marafiki wa shetani. Hakika, hila za shetani zimekuwa dhaifu sana



السورة: ANNISAI 

الآية : 77

أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ قِيلَ لَهُمۡ كُفُّوٓاْ أَيۡدِيَكُمۡ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ فَلَمَّا كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقِتَالُ إِذَا فَرِيقٞ مِّنۡهُمۡ يَخۡشَوۡنَ ٱلنَّاسَ كَخَشۡيَةِ ٱللَّهِ أَوۡ أَشَدَّ خَشۡيَةٗۚ وَقَالُواْ رَبَّنَا لِمَ كَتَبۡتَ عَلَيۡنَا ٱلۡقِتَالَ لَوۡلَآ أَخَّرۡتَنَآ إِلَىٰٓ أَجَلٖ قَرِيبٖۗ قُلۡ مَتَٰعُ ٱلدُّنۡيَا قَلِيلٞ وَٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّمَنِ ٱتَّقَىٰ وَلَا تُظۡلَمُونَ فَتِيلًا

Je, hukuwaona wale ambao wakiambiwa: Zuieni mikono yenu (acheni vita) na simamisheni Swala na toeni Zaka? Basi walipoandikiwa (walipowajibishiwa) vita mara kundi miongoni mwao wanawaogopa watu kama wanavyomuogopa Allah au zaidi (ya kumuogopa Allah). Na wamesema: Kwanini umetufaradhishia kupigana? Ingekuwa bora kutuchelewesha mpaka muda wa karibu (ili tufe kifo cha kawaida). Sema (uwaambie): Raha ya duniani ni ndogo, na Akhera ni bora zaidi kwa mwenye Ucha Mungu, na hamtadhulumiwa (jambo lolote hata kama ni dogo kama) uzi wa kokwa ya tende



السورة: ANNISAI 

الآية : 78

أَيۡنَمَا تَكُونُواْ يُدۡرِككُّمُ ٱلۡمَوۡتُ وَلَوۡ كُنتُمۡ فِي بُرُوجٖ مُّشَيَّدَةٖۗ وَإِن تُصِبۡهُمۡ حَسَنَةٞ يَقُولُواْ هَٰذِهِۦ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ وَإِن تُصِبۡهُمۡ سَيِّئَةٞ يَقُولُواْ هَٰذِهِۦ مِنۡ عِندِكَۚ قُلۡ كُلّٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ فَمَالِ هَـٰٓؤُلَآءِ ٱلۡقَوۡمِ لَا يَكَادُونَ يَفۡقَهُونَ حَدِيثٗا

Popote muwapo mauti yatakufikeni, hata mkiwa katika ngome madhubuti. Na likiwapata (jambo) zuri wanasema: Hili linatoka kwa Allah, na likiwapata (jambo) baya wanasema: Hili limetoka kwako. Sema (uwaambie): Yote yanatoka kwa Allah. Basi wana nini watu hawa hawakaribii kufahamu mazungumzo?



السورة: ANNISAI 

الآية : 79

مَّآ أَصَابَكَ مِنۡ حَسَنَةٖ فَمِنَ ٱللَّهِۖ وَمَآ أَصَابَكَ مِن سَيِّئَةٖ فَمِن نَّفۡسِكَۚ وَأَرۡسَلۡنَٰكَ لِلنَّاسِ رَسُولٗاۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدٗا

(Jambo) Zuri lolote lililokupata limetoka kwa Allah, na (jambo) lolote baya lililokupata limetokana na wewe mwenyewe. Na tumekupeleka kwa watu ukiwa Mtume, na yatosha kwamba Allah ni shahidi



السورة: ANNISAI 

الآية : 80

مَّن يُطِعِ ٱلرَّسُولَ فَقَدۡ أَطَاعَ ٱللَّهَۖ وَمَن تَوَلَّىٰ فَمَآ أَرۡسَلۡنَٰكَ عَلَيۡهِمۡ حَفِيظٗا

Yeyote anayemtii Mtume basi hakika (atakuwa) amemtii Allah, na yeyote atakaye kengeuka basi (ni juu yake, kwa sababu) hatukukupeleka kwao uwe mtunzaji (wa matendo yao)



السورة: ANNISAI 

الآية : 81

وَيَقُولُونَ طَاعَةٞ فَإِذَا بَرَزُواْ مِنۡ عِندِكَ بَيَّتَ طَآئِفَةٞ مِّنۡهُمۡ غَيۡرَ ٱلَّذِي تَقُولُۖ وَٱللَّهُ يَكۡتُبُ مَا يُبَيِّتُونَۖ فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ وَكَفَىٰ بِٱللَّهِ وَكِيلًا

Na wanasema: Tumetii. Lakini wakiondoka kwako kundi miongoni mwao linapanga njama usiku tofauti na yale unayosema, na Allah anayaandika wanayo yapanga usiku. Basi wapuuze, na mtegemee Allah, na inatosha kwamba Allah ni Mwenye kutegemewa



السورة: ANNISAI 

الآية : 82

أَفَلَا يَتَدَبَّرُونَ ٱلۡقُرۡءَانَۚ وَلَوۡ كَانَ مِنۡ عِندِ غَيۡرِ ٱللَّهِ لَوَجَدُواْ فِيهِ ٱخۡتِلَٰفٗا كَثِيرٗا

Hivi hawaizingatii hii Kurani? Na lau kama ingetoka kwa asiyekuwa Allah bila shaka wangekuta ndani yake kasoro nyingi



السورة: ANNISAI 

الآية : 83

وَإِذَا جَآءَهُمۡ أَمۡرٞ مِّنَ ٱلۡأَمۡنِ أَوِ ٱلۡخَوۡفِ أَذَاعُواْ بِهِۦۖ وَلَوۡ رَدُّوهُ إِلَى ٱلرَّسُولِ وَإِلَىٰٓ أُوْلِي ٱلۡأَمۡرِ مِنۡهُمۡ لَعَلِمَهُ ٱلَّذِينَ يَسۡتَنۢبِطُونَهُۥ مِنۡهُمۡۗ وَلَوۡلَا فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَرَحۡمَتُهُۥ لَٱتَّبَعۡتُمُ ٱلشَّيۡطَٰنَ إِلَّا قَلِيلٗا

Na linapowafikia jambo lolote la amani au hofu wanalitangaza. Na lau kama wangelirejesha kwa Mtume na kwa wenye mamlaka miongoni mwao, wangelijua wale walio na uwezo wa kulichambua.[1] Na lau kama sio fadhila za Allah kwenu na rehema zake, mngemfuata shetani ispokuwa wachache sana


1- - Kurani hapa inawakemea wale wenye tabia ya kusambaza habari nyeti zinazoweza kuteteresha amani au `kuleta hofu na taharuki katika jamii. Habari inapohusu amani na utulivu inapaswa kuachiwa wenye mamlaka. Katika Aya hapa ametajwa Mtume kwa sababu yeye alikuwa Mkuu wa Dola. Wenye mamlaka ni wale ambao wamekasimiwa mamlaka na Dola. Aya imeeleza kuwa hawa ndio wenye uwezo na nyenzo za kuchunguza, kutafiti na kupata undani wa habari na usahihi wake au kinyume chake. Pia hawa ndio wenye mamlaka na dhamana ya kulinda amani, utulivu na ustawi wa jamii.


السورة: ANNISAI 

الآية : 84

فَقَٰتِلۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ لَا تُكَلَّفُ إِلَّا نَفۡسَكَۚ وَحَرِّضِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَۖ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَكُفَّ بَأۡسَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ وَٱللَّهُ أَشَدُّ بَأۡسٗا وَأَشَدُّ تَنكِيلٗا

Basi pigana katika njia ya Allah. Hukalifishwi isipokuwa nafsi yako tu, na wahamasishe waumini, huenda Allah akayazuia mashambulizi ya waliokufuru. Na Allah ni Mkali sana wa kushambulia na Mkali wa kuadhibu



السورة: ANNISAI 

الآية : 85

مَّن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةً حَسَنَةٗ يَكُن لَّهُۥ نَصِيبٞ مِّنۡهَاۖ وَمَن يَشۡفَعۡ شَفَٰعَةٗ سَيِّئَةٗ يَكُن لَّهُۥ كِفۡلٞ مِّنۡهَاۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ مُّقِيتٗا

Yeyote atakayeombea maombezi mazuri (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo jema) atapata fungu katika jambo zuri hilo, na yeyote atakayeombea maombezi maovu (atakayeingilia kati katika kufanikisha jambo ovu) atapata fungu katika jambo ovu hilo. Na Allahni Mwenye uweza na ujuzi juu ya kila kitu



السورة: ANNISAI 

الآية : 86

وَإِذَا حُيِّيتُم بِتَحِيَّةٖ فَحَيُّواْ بِأَحۡسَنَ مِنۡهَآ أَوۡ رُدُّوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٍ حَسِيبًا

Na mnapoamkiwa maamkizi yoyote yale, basi nanyi itikieni kwa maamkizi mazuri zaidi kuliko hayo au rejesheni hayo hayo. Hakika, Allah ni Mwenye kuhesabu kila kitu



السورة: ANNISAI 

الآية : 87

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۗ وَمَنۡ أَصۡدَقُ مِنَ ٱللَّهِ حَدِيثٗا

Allah, hakuna mwenye haki ya kuabudiwa ispokuwa yeye tu. Kwa yakini kabisa, atakukusanyeni katika Siku ya Kiyama isiyokuwa na shaka yoyote. Na ni nani mkweli sana wa maneno kuliko Allah?



السورة: ANNISAI 

الآية : 88

۞فَمَا لَكُمۡ فِي ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِئَتَيۡنِ وَٱللَّهُ أَرۡكَسَهُم بِمَا كَسَبُوٓاْۚ أَتُرِيدُونَ أَن تَهۡدُواْ مَنۡ أَضَلَّ ٱللَّهُۖ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَلَن تَجِدَ لَهُۥ سَبِيلٗا

Basi mna nini nyinyi mmegawanyika makundi mawili kuhusu wanafiki, na ilhali Allah amewageuza (na kurudi kwenye ukafiri) kwasababu ya yale waliyo-yachuma? Hivi mnataka kuwaongoa ambao Allah amewapoteza? Na yeyote ambaye Allah amempoteza hutapata njia (ya kumuongoza)



السورة: ANNISAI 

الآية : 89

وَدُّواْ لَوۡ تَكۡفُرُونَ كَمَا كَفَرُواْ فَتَكُونُونَ سَوَآءٗۖ فَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ أَوۡلِيَآءَ حَتَّىٰ يُهَاجِرُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَخُذُوهُمۡ وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ وَجَدتُّمُوهُمۡۖ وَلَا تَتَّخِذُواْ مِنۡهُمۡ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرًا

Wametamani lau mngekufuru kama walivyokufuru wao ili muwe sawa. Basi msiwafanye marafiki wa karibu miongoni mwao mpaka wahame kwa ajili ya dini ya Allah. Basi kama wakikengeuka washikeni (mateka) na waueni popote mtakapowakuta, na msifanye miongoni mwao rafiki wa karibu wala msaidizi



السورة: ANNISAI 

الآية : 90

إِلَّا ٱلَّذِينَ يَصِلُونَ إِلَىٰ قَوۡمِۭ بَيۡنَكُمۡ وَبَيۡنَهُم مِّيثَٰقٌ أَوۡ جَآءُوكُمۡ حَصِرَتۡ صُدُورُهُمۡ أَن يُقَٰتِلُوكُمۡ أَوۡ يُقَٰتِلُواْ قَوۡمَهُمۡۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَسَلَّطَهُمۡ عَلَيۡكُمۡ فَلَقَٰتَلُوكُمۡۚ فَإِنِ ٱعۡتَزَلُوكُمۡ فَلَمۡ يُقَٰتِلُوكُمۡ وَأَلۡقَوۡاْ إِلَيۡكُمُ ٱلسَّلَمَ فَمَا جَعَلَ ٱللَّهُ لَكُمۡ عَلَيۡهِمۡ سَبِيلٗا

Isipokuwa wale ambao wana-husiana na watu ambao kati yenu na wao kuna mkataba au wamekujieni huku nyoyo zao zikiona tabu kupigana nanyi au kupigana na watu wao. Na Allah angetaka angeliwapa nguvu dhidi yenu wakakupigeni. Basi wakiachana nanyi na wasipigane nanyi na wakakuleteeni amani (wakakutangazieni amani), basi Allah hakukupeni njia (ruhusa ya kupiganana nao)