السورة: YUNUS 

الآية : 61

وَمَا تَكُونُ فِي شَأۡنٖ وَمَا تَتۡلُواْ مِنۡهُ مِن قُرۡءَانٖ وَلَا تَعۡمَلُونَ مِنۡ عَمَلٍ إِلَّا كُنَّا عَلَيۡكُمۡ شُهُودًا إِذۡ تُفِيضُونَ فِيهِۚ وَمَا يَعۡزُبُ عَن رَّبِّكَ مِن مِّثۡقَالِ ذَرَّةٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا فِي ٱلسَّمَآءِ وَلَآ أَصۡغَرَ مِن ذَٰلِكَ وَلَآ أَكۡبَرَ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٍ

Na huwi katika jambo lolote na husomi chochote katika Qur’ani na hamtendi kitendo chochote isipokuwa kwamba tumekuwa mashahidi kwenu mnapokiendea (mnapofanya). Na haujifichi kwa Mola wako Mlezi uzito wa chembe ndogo ardhini wala mbinguni na hata kidogo zaidi ya hicho au kikubwa isipokuwa kipo katika kitabu chenye kuweka wazi (kila kitu)



السورة: YUNUS 

الآية : 62

أَلَآ إِنَّ أَوۡلِيَآءَ ٱللَّهِ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Zindukeni: Hakika, Mawalii (wapenzi) wa Allah hawana hofu (yoyote) na hawahuzuniki



السورة: YUNUS 

الآية : 63

ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَكَانُواْ يَتَّقُونَ

(Mawalii wa Allah ni) Ambao wameamini na wakawa wacha Mungu



السورة: YUNUS 

الآية : 64

لَهُمُ ٱلۡبُشۡرَىٰ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِۚ لَا تَبۡدِيلَ لِكَلِمَٰتِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ هُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Wana bishara (habari njema) katika maisha ya duniani (kwa kupata wanachokipenda) na Akhera (kwa kuingia Peponi). Hakuna kubadilishwa kwa maneno ya Allah. Hayo ndio mafanikio makubwa



السورة: YUNUS 

الآية : 65

وَلَا يَحۡزُنكَ قَوۡلُهُمۡۘ إِنَّ ٱلۡعِزَّةَ لِلَّهِ جَمِيعًاۚ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na zisikuhuzunishe kauli zao[1]. Hakika, utukufu wote ni wa Allah tu. Yeye tu ndiye Mwenye kusikia, Mjuzi sana


1- - Makafiri walikuwa wakimwambia Mtume kauli nyingi za kejeli na kumkatisha tamaa. Miongoni mwa kauli hizo walizokuwa wakimwambia ni pamoja na hii: Wewe sio Mtume n.k.


السورة: YUNUS 

الآية : 66

أَلَآ إِنَّ لِلَّهِ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَمَا يَتَّبِعُ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ شُرَكَآءَۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ

Zindukeni kuwa, wote waliomo mbinguni na ardhini ni wa Allah tu. Na wale wanaowaomba (Miungu) wengine kinyume na Allah hawawafuati washirika. Hawafuati isipokuwa dhana tu na hawana chochote isipokuwa wanasema uongo tu



السورة: YUNUS 

الآية : 67

هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلَّيۡلَ لِتَسۡكُنُواْ فِيهِ وَٱلنَّهَارَ مُبۡصِرًاۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَسۡمَعُونَ

Yeye (Allah) ndiye ambaye amekuwekeeni usiku ili muweze kutulia humo na (amekuwekeeni) mchana ukiangaza (ili mpate kuona na kufanya shughuli zenu mbali mbali). Hakika, katika haya zipo ishara (za kuzingatia) kwa watu wanaosikia (na kuzingatia)



السورة: YUNUS 

الآية : 68

قَالُواْ ٱتَّخَذَ ٱللَّهُ وَلَدٗاۗ سُبۡحَٰنَهُۥۖ هُوَ ٱلۡغَنِيُّۖ لَهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ إِنۡ عِندَكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭ بِهَٰذَآۚ أَتَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

(Wayahudi na Wakristo na wanaoiga itikadi zao) Wamesema: Allah ana mtoto. Utakasifu ni wake! Yeye tu ndiye Mkwasi. Ni vyake yeye tu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Nyinyi hamna hoja yoyote juu ya haya! Hivi mnamsingizia Allah msiyoyajua?



السورة: YUNUS 

الآية : 69

قُلۡ إِنَّ ٱلَّذِينَ يَفۡتَرُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ لَا يُفۡلِحُونَ

Sema: Hakika, wale wanaomzushia Allah uwongo, hawafaulu



السورة: YUNUS 

الآية : 70

مَتَٰعٞ فِي ٱلدُّنۡيَا ثُمَّ إِلَيۡنَا مَرۡجِعُهُمۡ ثُمَّ نُذِيقُهُمُ ٱلۡعَذَابَ ٱلشَّدِيدَ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ

Ni starehe (ndogo) tu duniani, kisha marejeo yao ni kwetu tu, kisha tutawaonjesha adhabu kali, kwa sababu ya ukafiri waliokuwa wakiufanya



السورة: YUNUS 

الآية : 71

۞وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ نُوحٍ إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ إِن كَانَ كَبُرَ عَلَيۡكُم مَّقَامِي وَتَذۡكِيرِي بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ فَعَلَى ٱللَّهِ تَوَكَّلۡتُ فَأَجۡمِعُوٓاْ أَمۡرَكُمۡ وَشُرَكَآءَكُمۡ ثُمَّ لَا يَكُنۡ أَمۡرُكُمۡ عَلَيۡكُمۡ غُمَّةٗ ثُمَّ ٱقۡضُوٓاْ إِلَيَّ وَلَا تُنظِرُونِ

Na wasomee habari za (Mtume) Nuhu wakati alipowaambia watu wake kuwa: “Enyi watu wangu, ikiwa mnachukizwa na kuishi kwangu (na nyinyi) na kukumbusha kwangu Aya za Allah, basi mimi nimemtegemea Allah tu. Basi amueni jambo lenu nyinyi na washirika (Miungu) wenu, kisha jambo lenu lisiwe la kificho, kisha pitisheni hukumu kwangu na msinicheleweshe



السورة: YUNUS 

الآية : 72

فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَمَا سَأَلۡتُكُم مِّنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِۖ وَأُمِرۡتُ أَنۡ أَكُونَ مِنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ

Basi mkikengeuka, mimi sikukuombeni ujira wowote. Ujira wangu haupo (popote) isipokuwa kwa Allah tu, na nimeamrishwa niwe miongoni mwa Waislamu”



السورة: YUNUS 

الآية : 73

فَكَذَّبُوهُ فَنَجَّيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ وَجَعَلۡنَٰهُمۡ خَلَـٰٓئِفَ وَأَغۡرَقۡنَا ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَاۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Basi (watu wake) wakamka-dhibisha (wakampinga Mtume Nuhu), tukamuokoa yeye na waliokuwepo pamoja naye katika mashua, na tukawafanya warithi (wa nafasi za walioangamizwa) na tukawazamisha baharini wale waliozikadhibisha Aya zetu. Basi angalia namna ulivyokuwa mwisho wa walio onywa



السورة: YUNUS 

الآية : 74

ثُمَّ بَعَثۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِۦ رُسُلًا إِلَىٰ قَوۡمِهِمۡ فَجَآءُوهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَمَا كَانُواْ لِيُؤۡمِنُواْ بِمَا كَذَّبُواْ بِهِۦ مِن قَبۡلُۚ كَذَٰلِكَ نَطۡبَعُ عَلَىٰ قُلُوبِ ٱلۡمُعۡتَدِينَ

Kisha baada yake tuliwatuma Mitume (mbali mbali) kwa watu wao, na (Mitume hao) waliwaendea kwa hoja za waziwazi. Hawakuweza kuyaamini yale waliyoyapinga hapo kabla. Kama hivyo, tunazipiga chapa nyoyo za watu wavukao mipaka (ya sheria za Allah)



السورة: YUNUS 

الآية : 75

ثُمَّ بَعَثۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِم مُّوسَىٰ وَهَٰرُونَ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ بِـَٔايَٰتِنَا فَٱسۡتَكۡبَرُواْ وَكَانُواْ قَوۡمٗا مُّجۡرِمِينَ

Kisha tukamtuma Musa na Haruna baada ya hao kwenda kwa Firauni na mamwinyi wake (wakiwa na) Aya zetu. Basi wakafanya kiburi na wakawa watu wakosefu



السورة: YUNUS 

الآية : 76

فَلَمَّا جَآءَهُمُ ٱلۡحَقُّ مِنۡ عِندِنَا قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰذَا لَسِحۡرٞ مُّبِينٞ

Basi ilipowajia haki kutoka kwetu walisema: “Bila shaka, huu hasa ni uchawi ulio dhahiri sana”



السورة: YUNUS 

الآية : 77

قَالَ مُوسَىٰٓ أَتَقُولُونَ لِلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَكُمۡۖ أَسِحۡرٌ هَٰذَا وَلَا يُفۡلِحُ ٱلسَّـٰحِرُونَ

Akasema Musa: Hivi, mnasema kuhusu haki ilipokujieni kwamba, huu ni uchawi? Na wachawi hawafaulu



السورة: YUNUS 

الآية : 78

قَالُوٓاْ أَجِئۡتَنَا لِتَلۡفِتَنَا عَمَّا وَجَدۡنَا عَلَيۡهِ ءَابَآءَنَا وَتَكُونَ لَكُمَا ٱلۡكِبۡرِيَآءُ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا نَحۡنُ لَكُمَا بِمُؤۡمِنِينَ

Wakasema: “Hivi, umetujia ili utuondoe katika yale tuliyowakuta nayo baba zetu, na ukubwa uwe wenu wawili nyie katika ardhi? Na sisi kamwe hatutakuaminini”



السورة: YUNUS 

الآية : 79

وَقَالَ فِرۡعَوۡنُ ٱئۡتُونِي بِكُلِّ سَٰحِرٍ عَلِيمٖ

Na Firauni akasema: Nileteeni kila mchawi mahiri sana



السورة: YUNUS 

الآية : 80

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالَ لَهُم مُّوسَىٰٓ أَلۡقُواْ مَآ أَنتُم مُّلۡقُونَ

Basi wachawi walipofika, Musa aliwaambia: Tupeni (chini) mnavyotaka kuvitupa (chini)



السورة: YUNUS 

الآية : 81

فَلَمَّآ أَلۡقَوۡاْ قَالَ مُوسَىٰ مَا جِئۡتُم بِهِ ٱلسِّحۡرُۖ إِنَّ ٱللَّهَ سَيُبۡطِلُهُۥٓ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُصۡلِحُ عَمَلَ ٱلۡمُفۡسِدِينَ

Basi (wachawi) walipotupa, Musa akasema: “Hiki mlicholeta ni uchawi. Hakika, Allah ataubatilisha. Hakika, Allah hastawishi vitendo vya waharibifu”



السورة: YUNUS 

الآية : 82

وَيُحِقُّ ٱللَّهُ ٱلۡحَقَّ بِكَلِمَٰتِهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُجۡرِمُونَ

Na Allah anahakikisha haki inashinda kwa maneno yake, na hata kama waovu watachukia



السورة: YUNUS 

الآية : 83

فَمَآ ءَامَنَ لِمُوسَىٰٓ إِلَّا ذُرِّيَّةٞ مِّن قَوۡمِهِۦ عَلَىٰ خَوۡفٖ مِّن فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِمۡ أَن يَفۡتِنَهُمۡۚ وَإِنَّ فِرۡعَوۡنَ لَعَالٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَإِنَّهُۥ لَمِنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Basi hakuna aliyemuamini Musa (pamoja na dalili na hoja zote alizowaonesha) isipokuwa vijana wachache katika kaumu yake huku wakiwa na hofu (ya kumuogopa) Firauni na mamwinyi wao wasiwatese. Na hakika kabisa, Firauni alikuwa mwenye kujikweza ardhini, na kwa yakini kabisa yeye (Firauni) alikuwa miongoni mwa waliokiuka mipaka (katika kufanya uovu)



السورة: YUNUS 

الآية : 84

وَقَالَ مُوسَىٰ يَٰقَوۡمِ إِن كُنتُمۡ ءَامَنتُم بِٱللَّهِ فَعَلَيۡهِ تَوَكَّلُوٓاْ إِن كُنتُم مُّسۡلِمِينَ

Na Musa alisema: Enyi watu wangu, kama kweli nyinyi mmemuamini Allah, basi mtegemeeni yeye tu, kama nyinyi mkiwa Waislamu (kweli)



السورة: YUNUS 

الآية : 85

فَقَالُواْ عَلَى ٱللَّهِ تَوَكَّلۡنَا رَبَّنَا لَا تَجۡعَلۡنَا فِتۡنَةٗ لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Basi wakasema: “Allah tu tunamtegemea. Ewe Mola wetu Mlezi, usitufanye mtihani kwa watu madhalimu”



السورة: YUNUS 

الآية : 86

وَنَجِّنَا بِرَحۡمَتِكَ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na utuokoe kwa rehema zako dhidi ya watu makafiri



السورة: YUNUS 

الآية : 87

وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰ وَأَخِيهِ أَن تَبَوَّءَا لِقَوۡمِكُمَا بِمِصۡرَ بُيُوتٗا وَٱجۡعَلُواْ بُيُوتَكُمۡ قِبۡلَةٗ وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na tulimpa Wahyi Musa na ndugu yake (Haruna) ya kuwa: Wawekeeni makazi (wajengeeni nyumba) watu wenu (katika mji wa) Misri na zifanyeni nyumba zenu ziwe na mahala pa ibada na simamisheni Swala na wape bishara Waumini



السورة: YUNUS 

الآية : 88

وَقَالَ مُوسَىٰ رَبَّنَآ إِنَّكَ ءَاتَيۡتَ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَأَهُۥ زِينَةٗ وَأَمۡوَٰلٗا فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا رَبَّنَا لِيُضِلُّواْ عَن سَبِيلِكَۖ رَبَّنَا ٱطۡمِسۡ عَلَىٰٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ وَٱشۡدُدۡ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَلَا يُؤۡمِنُواْ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Na Musa alisema: “(Ewe) Mola wetu Mlezi, bila shaka umempa Firauni na mamwinyi wake mapambo na mali nyingi katika maisha ya duniani (na hawakukushukuru). (Ewe) Mola wetu Mlezi, (umewapa hivyo vyote na wanavitumia) ili kuwapoteza (watu) wasiifuate njia yako. (Ewe) Mola wetu Mlezi, zifute Mali zao na mioyo yao ifanye kuwa migumu ili wasiamini hadi waione adhabu iumizayo mno”



السورة: YUNUS 

الآية : 89

قَالَ قَدۡ أُجِيبَت دَّعۡوَتُكُمَا فَٱسۡتَقِيمَا وَلَا تَتَّبِعَآنِّ سَبِيلَ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَ

(Allah) Akasema: Hakika maombi yenu yamekubaliwa. Basi simameni imara na katu msifuate njia ya wale wasiojua (wasiokuwa na elimu)



السورة: YUNUS 

الآية : 90

۞وَجَٰوَزۡنَا بِبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱلۡبَحۡرَ فَأَتۡبَعَهُمۡ فِرۡعَوۡنُ وَجُنُودُهُۥ بَغۡيٗا وَعَدۡوًاۖ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَدۡرَكَهُ ٱلۡغَرَقُ قَالَ ءَامَنتُ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱلَّذِيٓ ءَامَنَتۡ بِهِۦ بَنُوٓاْ إِسۡرَـٰٓءِيلَ وَأَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُسۡلِمِينَ

Na tuliwavusha Wana wa Israeli baharini. Basi Firauni na majeshi yake waliwafuata kwa nia ovu na uadui hadi (Firauni) ilipomfikia gharika, alisema: Nimeamini kwamba, hakuna Mola apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa tu yule ambaye Wana wa Israili wamemuamini, na mimi ni miongoni mwa Waislamu