السورة: ATTUR 

الآية : 31

قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ

Sema subirini basi hakika mimi pamoja nanyi ni miongoni mwa wenye kusubiri



السورة: ATTUR 

الآية : 32

أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ

Au zinawaamuru wao ndoto zao kwa hili au wao ni watu waovu



السورة: ATTUR 

الآية : 33

أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ

Au wanasema ameizua hiyo qurani bali hawaamini



السورة: ATTUR 

الآية : 34

فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Basi walete mazungumzo (Quran) mfano wake kama watakua wakweli



السورة: ATTUR 

الآية : 35

أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Au wameumbwa pasipo na kitu chochote (bila ya muumba) au wao ndio waumbaji?



السورة: ATTUR 

الآية : 36

أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ

Au wameumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini



السورة: ATTUR 

الآية : 37

أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ

Au wanazo hazina za Mola wako mlezi, au wao ndio wenye madaraka? (wenye kudhibiti)?



السورة: ATTUR 

الآية : 38

أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Au wanazo ngazi wanasikilizia kwa makini humo? Basi msikilizaji wao alete dalili bayana



السورة: ATTUR 

الآية : 39

أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ

Au (Allah) Ana watoto wa kike, nanyi mna watoto wa kiume?



السورة: ATTUR 

الآية : 40

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au unawaomba ujira kwa hiyo wameelemewa na uzito wa gharama?



السورة: ATTUR 

الآية : 41

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanayo elimu ya ghayb kisha wao wanaandika?



السورة: ATTUR 

الآية : 42

أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ

Au wanakusudia hila (shari)? Basi wale waliokufuru wao ndio watakaopangiwa hila



السورة: ATTUR 

الآية : 43

أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Au wana wao mungu asiye Allah utakasifu ni wake allah na yote wanayomshirikisha nayo



السورة: ATTUR 

الآية : 44

وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ

Na hata wangeliona pande la moto kutoka mbinguni linaanguka wangelisema: Mawingu tu yamerundikana



السورة: ATTUR 

الآية : 45

فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ

Basi waachilie mbali mpaka wakutane na Siku yao ambayo humo wataangamizwa



السورة: ATTUR 

الآية : 46

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo njama zao hazitowafaa kitu chochote, na wala wao hawatonusuriwa



السورة: ATTUR 

الآية : 47

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hiyo, lakini wengi wao hawajui



السورة: ATTUR 

الآية : 48

وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Na subiri hukumu ya mola wako mlezi na hakika wewe uko machoni kwetu (uangalizi wetu) na msabihi Mola wako mlezi pamoja na kusifu wakati unapoamka



السورة: ATTUR 

الآية : 49

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Na katika usiku Msabbih na zinapokuchwa nyota