السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 31

ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ

Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 32

فَأَرۡسَلۡنَا فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ

Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Allah! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamuogopi?



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 33

وَقَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱلۡأٓخِرَةِ وَأَتۡرَفۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا مَا هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُكُمۡ يَأۡكُلُ مِمَّا تَأۡكُلُونَ مِنۡهُ وَيَشۡرَبُ مِمَّا تَشۡرَبُونَ

Na wakasema wakubwa katika watu wake waliokufuru na kukadhibisha mkutano wa Akhera na tuliwatajirisha katika maisha ya dunia, huyu siye ila ni mtu kama nyinyi anakula katika vile mnavyokula na anakunywa katika vile mnavyokunywa



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 34

وَلَئِنۡ أَطَعۡتُم بَشَرٗا مِّثۡلَكُمۡ إِنَّكُمۡ إِذٗا لَّخَٰسِرُونَ

Na lau mtamtii binadamu kama nyinyi, basi nyinyi mtakuwa ni wenye kupata hasara (kwa kuwaacha waungu wenu na kumfuata yeye)



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 35

أَيَعِدُكُمۡ أَنَّكُمۡ إِذَا مِتُّمۡ وَكُنتُمۡ تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَنَّكُم مُّخۡرَجُونَ

Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 36

۞هَيۡهَاتَ هَيۡهَاتَ لِمَا تُوعَدُونَ

Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 37

إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا نَمُوتُ وَنَحۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ

Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 38

إِنۡ هُوَ إِلَّا رَجُلٌ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبٗا وَمَا نَحۡنُ لَهُۥ بِمُؤۡمِنِينَ

Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Allah uongo, wala sisi sio wa kumuamini



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 39

قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي بِمَا كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwasababu wananikanusha



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 40

قَالَ عَمَّا قَلِيلٖ لَّيُصۡبِحُنَّ نَٰدِمِينَ

(Allah) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 41

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ بِٱلۡحَقِّ فَجَعَلۡنَٰهُمۡ غُثَآءٗۚ فَبُعۡدٗا لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhalimu!



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 42

ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قُرُونًا ءَاخَرِينَ

Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 43

مَا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ

Hapana umma uwezao kutan-guliza ajali yake wala kuikawiza



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 44

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا تَتۡرَاۖ كُلَّ مَا جَآءَ أُمَّةٗ رَّسُولُهَا كَذَّبُوهُۖ فَأَتۡبَعۡنَا بَعۡضَهُم بَعۡضٗا وَجَعَلۡنَٰهُمۡ أَحَادِيثَۚ فَبُعۡدٗا لِّقَوۡمٖ لَّا يُؤۡمِنُونَ

Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafua-tanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 45

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ وَأَخَاهُ هَٰرُونَ بِـَٔايَٰتِنَا وَسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Kisha tukamtuma Mussa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 46

إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ وَكَانُواْ قَوۡمًا عَالِينَ

Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 47

فَقَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لِبَشَرَيۡنِ مِثۡلِنَا وَقَوۡمُهُمَا لَنَا عَٰبِدُونَ

Wakasema: Je, tuwaamini wawili hawa wanaadamu kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 48

فَكَذَّبُوهُمَا فَكَانُواْ مِنَ ٱلۡمُهۡلَكِينَ

Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 49

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ لَعَلَّهُمۡ يَهۡتَدُونَ

Na hakika tulimpa Mussa Kitabu ili wapate kuongoka



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 50

وَجَعَلۡنَا ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَأُمَّهُۥٓ ءَايَةٗ وَءَاوَيۡنَٰهُمَآ إِلَىٰ رَبۡوَةٖ ذَاتِ قَرَارٖ وَمَعِينٖ

Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 51

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلرُّسُلُ كُلُواْ مِنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَٱعۡمَلُواْ صَٰلِحًاۖ إِنِّي بِمَا تَعۡمَلُونَ عَلِيمٞ

Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 52

وَإِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱتَّقُونِ

Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 53

فَتَقَطَّعُوٓاْ أَمۡرَهُم بَيۡنَهُمۡ زُبُرٗاۖ كُلُّ حِزۡبِۭ بِمَا لَدَيۡهِمۡ فَرِحُونَ

Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 54

فَذَرۡهُمۡ فِي غَمۡرَتِهِمۡ حَتَّىٰ حِينٍ

Basi waache katika ghafla yao kwa muda



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 55

أَيَحۡسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُم بِهِۦ مِن مَّالٖ وَبَنِينَ

Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 56

نُسَارِعُ لَهُمۡ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ بَل لَّا يَشۡعُرُونَ

Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 57

إِنَّ ٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ خَشۡيَةِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 58

وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ يُؤۡمِنُونَ

Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 59

وَٱلَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمۡ لَا يُشۡرِكُونَ

Na wale ambao hawa mshirikishi Mola wao Mlezi



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 60

وَٱلَّذِينَ يُؤۡتُونَ مَآ ءَاتَواْ وَّقُلُوبُهُمۡ وَجِلَةٌ أَنَّهُمۡ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ رَٰجِعُونَ

Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinaogopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,