السورة: AL-HIJRI 

الآية : 31

إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

Isipokuwa Ibilisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na waliosujudu



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 32

قَالَ يَـٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

(Allah) alisema: Ewe Ibilisi! Umepatwa na nini hata hukuwa pamoja na waliosujudu?



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 33

قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

(Ibilisi) Alisema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliyemuumba kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope meusi yaliyovunda[1]


1- - Ibilisi aliyasema hayo kwa kiburi na kujiona kuwa, Yeye aliyeumbwa kwa miale ya moto ni bora
zaidi kuliko Yule aliyeumbwa kwa udongo mweusi, unaotoa sauti na uliovunda.


السورة: AL-HIJRI 

الآية : 34

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ

(Allah) alisema: Basi toka humo (Peponi), kwa hakika wewe ni umelaaniwa



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 35

وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na hakika laana itakuwa juu yako mpaka Siku ya Malipo



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 36

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

(Iblisi) Alisema: (Ewe) Mola wangu Mlezi, Nipe muhula (nibakishe) mpaka siku watakapofufuliwa (watu)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 37

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

(Allah) alisema: Kwa hakika wewe ni katika waliopewa muhula (wa kutoangamizwa mpaka siku hiyo)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 38

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ

(Wewe utaendelea kuwepo) Mpaka siku ya wakati maalumu



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 39

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Ibilisi) Alisema: (Ewe) Mola wangu Mlezi, kwa ulivyonipotoa, basi ninakuapia nitawapambia (upotovu) hapa duniani na nitawapoteza wote



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 40

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipokuwa waja wako walio-safishwa



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 41

قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ

(Allah) Alisema: Hii Njia ya kuja kwangu Iliyo nyooka (kuwalinda waja wangu na upotovu hilo ni jukumu langu)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 42

إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipokuwa (ataathirika nawe) yule mpotofu aliyekufuata



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 43

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na bila shaka Jahanamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote (wanaokufuata)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 44

لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ

(Moto wa Jahanamu) una milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu waliyotengewa



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 45

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ

Hakika wanaomuogopa Mola wao watakuwa katika Pepo na chemchem



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 46

ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ

(Wamchao Allah wataambiwa:) Ingieni (Peponi) kwa salama na amani



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 47

وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Na tutaondoa (kwa watu wa Peponi) chuki iliyokuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya fahari wakiwa wameelekeana



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 48

لَا يَمَسُّهُمۡ فِيهَا نَصَبٞ وَمَا هُم مِّنۡهَا بِمُخۡرَجِينَ

Hautawagusa humo uchovu, wala humo hawatatolewa



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 49

۞نَبِّئۡ عِبَادِيٓ أَنِّيٓ أَنَا ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ

Wape habari waja wangu ya kwamba, Mimi ndiye Mwenye kusamehe sana, Mwenye kurehemu



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 50

وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ ٱلۡعَذَابُ ٱلۡأَلِيمُ

Na kwamba adhabu yangu ndiyo adhabu iliyo chungu mno



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 51

وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ

(Ewe Mtume) Na wape (waja wangu) habari za wageni wa Ibrahim



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 52

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ

Walipoingia kwake na walisema: Salama! Yeye alisema (kwa kuingia kwenu bila kubisha hodi): Hakika sisi tunakuogopeni



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 53

قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ

Walisema (kumwambia): Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi mno (Naye ni Is-haka)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 54

قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ

(Ibrahimu) Alisema: Mnanibashiria (mwana) nami uzee umenishika![1] Basi mnanibashiria kwa kigezo gani?


1- - Ibrahimu hapa alileta mshangao unaotokana na muktadha wa ada na desturi za kibinadamu
kwamba, mtu kikongwe kama yeye ni nadra kupata mwana katika umri huo na si kupinga Qadari na
uweza wa Allah.


السورة: AL-HIJRI 

الآية : 55

قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ

(Wale Malaika) Walisema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanaokata tamaa (ya kupata mtoto uzeeni)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 56

قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ

(Ibrahimu) Alisema: Na hakuna anayekata tamaa na rehema za Mola wake Mlezi isipokuwa wale (watu) waliopotea?



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 57

قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

(Ibrahimu) Alisema (zaidi ya bishara hii): Mna jambo gani lingine, enyi wajumbe?



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 58

قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ

Walisema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu (watu) waovu



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 59

إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Isipokuwa waliomfuata Lutwi (na kumuamini). Bila ya shaka sisi tutawaokoa wote



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 60

إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Ispokuwa mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni (mwa) watakaobakia nyuma