السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 114

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن مَّنَعَ مَسَٰجِدَ ٱللَّهِ أَن يُذۡكَرَ فِيهَا ٱسۡمُهُۥ وَسَعَىٰ فِي خَرَابِهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ مَا كَانَ لَهُمۡ أَن يَدۡخُلُوهَآ إِلَّا خَآئِفِينَۚ لَهُمۡ فِي ٱلدُّنۡيَا خِزۡيٞ وَلَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ عَذَابٌ عَظِيمٞ

Na ninani dhalimu zaidi kuliko yule azuiaye Misikitiya Allah kutajwa humo jina lake na kujitahidi kuiharibu? Hao haitawawia kuingia humo ila kwa kuogopa. Watapata fedheha katika dunia, na akhera watapata adhabu kubwa



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 140

أَمۡ تَقُولُونَ إِنَّ إِبۡرَٰهِـۧمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ وَإِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَٱلۡأَسۡبَاطَ كَانُواْ هُودًا أَوۡ نَصَٰرَىٰۗ قُلۡ ءَأَنتُمۡ أَعۡلَمُ أَمِ ٱللَّهُۗ وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن كَتَمَ شَهَٰدَةً عِندَهُۥ مِنَ ٱللَّهِۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Au mnasema kuwa, Ibrahimu na Ismaili na Isihaka na Yakubu na watoto wake walikuwa Wayahudi au Wanaswara? Sema: Hivi nyinyi ndio wajuzi zaidi au Allah? Na ni nani aliyedhalimu mno kuliko yule aliyeuficha ushahidi alionao kutoka kwa Allah? Na Allah si mwenye kughafilika na yote mnayoyafanya



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 57

وَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَيُوَفِّيهِمۡ أُجُورَهُمۡۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ama walioamini na wakatenda mema, basi (Allah) atawalipa malipo yao kamili, na Allah hawapendi madhalimu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 86

كَيۡفَ يَهۡدِي ٱللَّهُ قَوۡمٗا كَفَرُواْ بَعۡدَ إِيمَٰنِهِمۡ وَشَهِدُوٓاْ أَنَّ ٱلرَّسُولَ حَقّٞ وَجَآءَهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Vipi Allah atawaongoa watu waliokufuru baada ya kuamini, na wameshuhudia pasipo shaka kwamba Mtume (Muhammad) ni hakina wamejiwa na ubainifu mbalimbali? Na Allah hawaongoi watu madhalimu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 94

فَمَنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ مِنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Basi watakaomzulia Allah uongo baada ya haya basi hao ndio madhalimu hasa



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 117

مَثَلُ مَا يُنفِقُونَ فِي هَٰذِهِ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا كَمَثَلِ رِيحٖ فِيهَا صِرٌّ أَصَابَتۡ حَرۡثَ قَوۡمٖ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَأَهۡلَكَتۡهُۚ وَمَا ظَلَمَهُمُ ٱللَّهُ وَلَٰكِنۡ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Mfano wawavitoavyo katika maisha haya ya duniani (na kutaraji kupata malipo mema Akhera) ni kama upepo wenye baridi kali uliolikumba shamba la watu waliodhulumu nafsi zao (kwa kumuasi Allah) ukaliangamiza shamba hilo (na wakakosa kufaidika na mazao waliyoyapanda kwa kuwa yameteketea). Na Allah hakuwadhulumu lakini wanajidhulumu wenyewe



السورة: ANNISAI 

الآية : 18

وَلَيۡسَتِ ٱلتَّوۡبَةُ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ حَتَّىٰٓ إِذَا حَضَرَ أَحَدَهُمُ ٱلۡمَوۡتُ قَالَ إِنِّي تُبۡتُ ٱلۡـَٰٔنَ وَلَا ٱلَّذِينَ يَمُوتُونَ وَهُمۡ كُفَّارٌۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَعۡتَدۡنَا لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمٗا

Na haikubaliwi toba kwa wale ambao wanafanya mabaya hadi mmoja wao umauti umfike (ndipo) anasema: Mimi sasa nimetubu, na wala wale wanaokufa wakiwa makafiri. Hao tumewaandalia adhabu yenye maumivu makali mno



السورة: AL-MAIDA 

الآية : 45

وَكَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيهَآ أَنَّ ٱلنَّفۡسَ بِٱلنَّفۡسِ وَٱلۡعَيۡنَ بِٱلۡعَيۡنِ وَٱلۡأَنفَ بِٱلۡأَنفِ وَٱلۡأُذُنَ بِٱلۡأُذُنِ وَٱلسِّنَّ بِٱلسِّنِّ وَٱلۡجُرُوحَ قِصَاصٞۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِۦ فَهُوَ كَفَّارَةٞ لَّهُۥۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Na humo (ndani ya Taurati) tumewaandikia ya kwamba, roho kwa roho na jicho kwa jicho na pua kwa pua na sikio kwa sikio na jino kwa jino na majeraha ni kisasi. Basi atakayetoa sadaka (ya kusamehe haki yake kulipa kisasi) hiyo ni kafara yake (ya madhambi yake). Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, basi hao ndio madhalimu



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 21

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِهِۦٓۚ إِنَّهُۥ لَا يُفۡلِحُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzulia uongo Allah au aliyezipinga Aya zake? Hakika ni kuwa, madhalimu hawafaulu



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 58

قُل لَّوۡ أَنَّ عِندِي مَا تَسۡتَعۡجِلُونَ بِهِۦ لَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۗ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِٱلظَّـٰلِمِينَ

Sema: Lau kama ningekuwa na kile mnachokiharakisha, basi lingekwishahukumiwa jambo kati yangu na kati yenu. Na Allah anawajua zaidi madhalimu



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 93

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ قَالَ أُوحِيَ إِلَيَّ وَلَمۡ يُوحَ إِلَيۡهِ شَيۡءٞ وَمَن قَالَ سَأُنزِلُ مِثۡلَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۗ وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلظَّـٰلِمُونَ فِي غَمَرَٰتِ ٱلۡمَوۡتِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ بَاسِطُوٓاْ أَيۡدِيهِمۡ أَخۡرِجُوٓاْ أَنفُسَكُمُۖ ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ عَذَابَ ٱلۡهُونِ بِمَا كُنتُمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَكُنتُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهِۦ تَسۡتَكۡبِرُونَ

Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia Allah uongo (kuwa amempa Utume) au aliyesema kuwa: Nimeletewa Wahyi na ilhali hakuletewa Wahyi wowote? Na (ni nani dhalimu zaidi kuliko) yule aliyesema kuwa: Nitateremsha mfano wa aliyoteremsha Allah? Na lau ungeona wakati madhalimu wamo katika mahangaiko ya mauti na Malaika wamenyoosha mikono yao (wakiwa tayari kuchukua roho zao wakiwaambia): Zitoeni (ziokoeni) roho zenu (kutoka mikononi mwetu kama mnaweza kwa sababu) leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya yale yasiyokuwa ya haki mliyomsingizia Allah, na mlikuwa mnazifanyia kiburi Aya zake



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 144

وَمِنَ ٱلۡإِبِلِ ٱثۡنَيۡنِ وَمِنَ ٱلۡبَقَرِ ٱثۡنَيۡنِۗ قُلۡ ءَآلذَّكَرَيۡنِ حَرَّمَ أَمِ ٱلۡأُنثَيَيۡنِ أَمَّا ٱشۡتَمَلَتۡ عَلَيۡهِ أَرۡحَامُ ٱلۡأُنثَيَيۡنِۖ أَمۡ كُنتُمۡ شُهَدَآءَ إِذۡ وَصَّىٰكُمُ ٱللَّهُ بِهَٰذَاۚ فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبٗا لِّيُضِلَّ ٱلنَّاسَ بِغَيۡرِ عِلۡمٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na katika ngamia (kaumba) wawili (dume na jike) na katika ng’ombe wawili. Sema: Je, ni madume mawili (Allah) alioharamisha au majike mawili au kilichobebwa katika matumbo ya majike mawili? Au nyinyi mlikuwepo wakati Allah amekuusieni haya? Basi ni nani aliye dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia Allah uongo ili awapoteze watu bila ya elimu yoyote. Hakika, Allah hawaongoi watu madhalimu



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 157

أَوۡ تَقُولُواْ لَوۡ أَنَّآ أُنزِلَ عَلَيۡنَا ٱلۡكِتَٰبُ لَكُنَّآ أَهۡدَىٰ مِنۡهُمۡۚ فَقَدۡ جَآءَكُم بَيِّنَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَهُدٗى وَرَحۡمَةٞۚ فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّن كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَصَدَفَ عَنۡهَاۗ سَنَجۡزِي ٱلَّذِينَ يَصۡدِفُونَ عَنۡ ءَايَٰتِنَا سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِ بِمَا كَانُواْ يَصۡدِفُونَ

Au (msije) mkasema: Lau kama tungeteremshiwa sisi kitabu tungekuwa waongofu zaidi kuliko wao. Basi kwa hakika kabisa, umekujieni ubainifu kutoka kwa Mola wenu Mlezi na muongozo na rehema. Sasa ni nani dhalimu zaidi (katika suala zima la itikadi) kuliko yule aliyepinga Aya za Allah na akajitenga nazo? Tutawalipa wale wanaojitenga na Aya zetu adhabu mbaya kwa sababu ya yale waliyokuwa wakijitenga nayo



السورة: AN-FAL 

الآية : 55

إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hakika viumbe waovu mno mbele ya Allah ni wale waliokufuru, kwasababu hawaamini (upekee wa Allah na uweza wake)



السورة: ATTAUBA 

الآية : 23

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَتَّخِذُوٓاْ ءَابَآءَكُمۡ وَإِخۡوَٰنَكُمۡ أَوۡلِيَآءَ إِنِ ٱسۡتَحَبُّواْ ٱلۡكُفۡرَ عَلَى ٱلۡإِيمَٰنِۚ وَمَن يَتَوَلَّهُم مِّنكُمۡ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Enyi mlioamini, msiwafanye baba zenu na ndugu zenu kuwa marafiki (wa ndani wa kuwategemea) ikiwa watapenda kuchagua ukafiri kuliko Imani (Uislamu). Na yeyote katika nyinyi atakayewafanya marafiki (na kuwaibia siri za Waislamu), basi hao ndio madhalimu hasa



السورة: ATTAUBA 

الآية : 70

أَلَمۡ يَأۡتِهِمۡ نَبَأُ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ قَوۡمِ نُوحٖ وَعَادٖ وَثَمُودَ وَقَوۡمِ إِبۡرَٰهِيمَ وَأَصۡحَٰبِ مَدۡيَنَ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتِۚ أَتَتۡهُمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِۖ فَمَا كَانَ ٱللَّهُ لِيَظۡلِمَهُمۡ وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Je, hazikuwafikia habari za wale waliokuwepo kabla yao; kaumu ya Nuhu na Adi na Thamudi na kaumu ya Ibrahimu na watu wa Madiyana na miji iliyopinduliwa chini juu, juu chini? Mitume wao waliwafikia kwa hoja zilizo wazi (na waliwapinga). Basi Allah hakuwa mwenye kuwadhulumu, lakini walikuwa wakijidhulumu wao wenyewe



السورة: ATTAUBA 

الآية : 98

وَمِنَ ٱلۡأَعۡرَابِ مَن يَتَّخِذُ مَا يُنفِقُ مَغۡرَمٗا وَيَتَرَبَّصُ بِكُمُ ٱلدَّوَآئِرَۚ عَلَيۡهِمۡ دَآئِرَةُ ٱلسَّوۡءِۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٞ

Na miongoni mwa Mabedui wapo wanaochukulia (wanadhani) vile wanavyovitoa (katika njia ya Allah) ni kazi bure (hasara), na wanakuvizieni mpate majanga. Majanga mabaya yawashukie wao. Na Allah ni Mwenye kusikia sana, Mwenye kujua mno



السورة: YUNUS 

الآية : 44

إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَظۡلِمُ ٱلنَّاسَ شَيۡـٔٗا وَلَٰكِنَّ ٱلنَّاسَ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Hakika, Allah hawadhulumu watu chochote na lakini watu wanazidhulumu nafsi zao



السورة: IBRAHIM 

الآية : 42

وَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱللَّهَ غَٰفِلًا عَمَّا يَعۡمَلُ ٱلظَّـٰلِمُونَۚ إِنَّمَا يُؤَخِّرُهُمۡ لِيَوۡمٖ تَشۡخَصُ فِيهِ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

(Ewe Mtume) Wala usidhani kwamba Allah ameghafilika na wanayo yafanya madhalimu. Hakika Yeye anachelewesha tu (kuwaadhibu papo hapo) mpaka siku yatapo kodoka macho yao



السورة: ANNAHLI 

الآية : 45

أَفَأَمِنَ ٱلَّذِينَ مَكَرُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَخۡسِفَ ٱللَّهُ بِهِمُ ٱلۡأَرۡضَ أَوۡ يَأۡتِيَهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Hivi, wanajiona wako salama wale waliofanya vitimbi vibaya kwamba Allah hataweza kuwa-didimiza ardhini, au (wanaona kuwa) haitawafika adhabu ghafla bila ya kuhisi kuja kwake?



السورة: ANNAHLI 

الآية : 46

أَوۡ يَأۡخُذَهُمۡ فِي تَقَلُّبِهِمۡ فَمَا هُم بِمُعۡجِزِينَ

Au iwachukuwe wakiwa katika mihangaiko yao? Na hawatoweza wao kuponyoka



السورة: ANNAHLI 

الآية : 47

أَوۡ يَأۡخُذَهُمۡ عَلَىٰ تَخَوُّفٖ فَإِنَّ رَبَّكُمۡ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٌ

Au awachukuwe (kwa kuwa-punguzia mali matunda na nafsi) au kwa adhabu yake? Hakika Mola wenu ni mlezi mpole mno, mwenye rehema



السورة: AL-ISRAA 

الآية : 82

وَنُنَزِّلُ مِنَ ٱلۡقُرۡءَانِ مَا هُوَ شِفَآءٞ وَرَحۡمَةٞ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ وَلَا يَزِيدُ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا خَسَارٗا

Na tunateremsha katika Qur’ani yaliyo matibabu na rehema kwa Waumini. Wala hayawazidishii madhaalimu ila khasara



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 53

لِّيَجۡعَلَ مَا يُلۡقِي ٱلشَّيۡطَٰنُ فِتۡنَةٗ لِّلَّذِينَ فِي قُلُوبِهِم مَّرَضٞ وَٱلۡقَاسِيَةِ قُلُوبُهُمۡۗ وَإِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ لَفِي شِقَاقِۭ بَعِيدٖ

Hayo ni ili alifanye lile analo litia Shetani liwe ni fitna kwa wale wenye maradhi ndani ya nyoyo zao, na wale ambao nyoyo zao ni ngumu. Na hakika madhalimu wamo katika mfarakano wa mbali



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 71

وَيَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ سُلۡطَٰنٗا وَمَا لَيۡسَ لَهُم بِهِۦ عِلۡمٞۗ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِن نَّصِيرٖ

Na wanaabudu badala ya Allah ambavyo hakuviteremshia ushahidi, na ambavyo hawana ujuzi navyo. Na madhalimu hawatakuwa na wa kuwasaidia



السورة: ANNUUR 

الآية : 48

وَإِذَا دُعُوٓاْ إِلَى ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَهُمۡ إِذَا فَرِيقٞ مِّنۡهُم مُّعۡرِضُونَ

Na wanapoitwa kumuendea Allah na Mtume wake ili ahukumu baina yao, kipo kikundi katika wao kinakataa



السورة: ANNUUR 

الآية : 49

وَإِن يَكُن لَّهُمُ ٱلۡحَقُّ يَأۡتُوٓاْ إِلَيۡهِ مُذۡعِنِينَ

Na ikiwa haki ni yao, wanamjia kwa kutii



السورة: ANNUUR 

الآية : 50

أَفِي قُلُوبِهِم مَّرَضٌ أَمِ ٱرۡتَابُوٓاْ أَمۡ يَخَافُونَ أَن يَحِيفَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَرَسُولُهُۥۚ بَلۡ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Je! Wana maradhi katika nyoyo zao, au wanaona shaka, au wanao-gopa ya kuwa Allah na Mtume wake watawadhulumu? Bali hao ndio madhaalimu



السورة: AL-QASWAS 

الآية : 50

فَإِن لَّمۡ يَسۡتَجِيبُواْ لَكَ فَٱعۡلَمۡ أَنَّمَا يَتَّبِعُونَ أَهۡوَآءَهُمۡۚ وَمَنۡ أَضَلُّ مِمَّنِ ٱتَّبَعَ هَوَىٰهُ بِغَيۡرِ هُدٗى مِّنَ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ikiwa hawakuitikii, basi jua kuwa wanafuata pumbao lao tu. Na nani aliye potea zaidi kumshinda anaye fuata pumbao lake bila ya uwongofu utokao kwa Mwenyezi Mungu. Hakika Mwenyezi Mungu hawaongoi watu wenye kudhulumu



السورة: AL-ANKABUUT 

الآية : 4

أَمۡ حَسِبَ ٱلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسَّيِّـَٔاتِ أَن يَسۡبِقُونَاۚ سَآءَ مَا يَحۡكُمُونَ

Au wamedhani ambao wanatenda maovu kwamba watatushinda? Ni hukumu mbaya sana hiyo wanayohukumu