السورة: GHAAFIR 

الآية : 44

فَسَتَذۡكُرُونَ مَآ أَقُولُ لَكُمۡۚ وَأُفَوِّضُ أَمۡرِيٓ إِلَى ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Basi mtayakumbuka ninayo kuambieni. Nami namkabidhi Allah mambo yangu. Hakika Allah anawaona waja wake



السورة: GHAAFIR 

الآية : 45

فَوَقَىٰهُ ٱللَّهُ سَيِّـَٔاتِ مَا مَكَرُواْۖ وَحَاقَ بِـَٔالِ فِرۡعَوۡنَ سُوٓءُ ٱلۡعَذَابِ

Basi Allah akamlinda na ubaya wa hila walizo zifanya. Na adhabu mbaya itawazunguka watu wa Firaun



السورة: GHAAFIR 

الآية : 46

ٱلنَّارُ يُعۡرَضُونَ عَلَيۡهَا غُدُوّٗا وَعَشِيّٗاۚ وَيَوۡمَ تَقُومُ ٱلسَّاعَةُ أَدۡخِلُوٓاْ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ أَشَدَّ ٱلۡعَذَابِ

Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itakapofika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 46

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ بِـَٔايَٰتِنَآ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَقَالَ إِنِّي رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na bila ya shaka tulimtuma Mussa kwa Ishara zetu aende kwa Firauni na waheshimiwa wake, na akasema: Hakika mimi ni Mtume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote!



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 47

فَلَمَّا جَآءَهُم بِـَٔايَٰتِنَآ إِذَا هُم مِّنۡهَا يَضۡحَكُونَ

Lakini alipo wajia na Ishara zetu wakaanza kuzicheka



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 48

وَمَا نُرِيهِم مِّنۡ ءَايَةٍ إِلَّا هِيَ أَكۡبَرُ مِنۡ أُخۡتِهَاۖ وَأَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡعَذَابِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na hatukuwaonyesha Ishara yoyote ila hiyo ilikuwa kubwa zaidi kuliko nyingine. Na tukawakamata kwa adhabu ili warejee



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 49

وَقَالُواْ يَـٰٓأَيُّهَ ٱلسَّاحِرُ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ بِمَا عَهِدَ عِندَكَ إِنَّنَا لَمُهۡتَدُونَ

Na wakasema: Ewe mchawi! Tuombee kwa Mola wako Mlezi kwa ile ahadi aliyokuahidi; hakika sisi tutakuwa wenye kuongoka



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 50

فَلَمَّا كَشَفۡنَا عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابَ إِذَا هُمۡ يَنكُثُونَ

Basi tulipo waondolea adhabu hiyo, mara wakaingia kuvunja ahadi



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 51

وَنَادَىٰ فِرۡعَوۡنُ فِي قَوۡمِهِۦ قَالَ يَٰقَوۡمِ أَلَيۡسَ لِي مُلۡكُ مِصۡرَ وَهَٰذِهِ ٱلۡأَنۡهَٰرُ تَجۡرِي مِن تَحۡتِيٓۚ أَفَلَا تُبۡصِرُونَ

Na Firauni alitangaza kwa watu wake, akisema: Enyi watu wangu! Kwani mimi sinao huu ufalme wa Misri, na hii mito inapita chini yangu? Je! Hamuoni?



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 52

أَمۡ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡ هَٰذَا ٱلَّذِي هُوَ مَهِينٞ وَلَا يَكَادُ يُبِينُ

Au mimi si bora kuliko huyu aliye mnyonge, wala hawezi kusema waziwazi?



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 53

فَلَوۡلَآ أُلۡقِيَ عَلَيۡهِ أَسۡوِرَةٞ مِّن ذَهَبٍ أَوۡ جَآءَ مَعَهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ مُقۡتَرِنِينَ

Basi mbona hakuvikwa vikuku vya dhahabu, au hawakuja Malaika pamoja naye wakamwandama?



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 54

فَٱسۡتَخَفَّ قَوۡمَهُۥ فَأَطَاعُوهُۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمٗا فَٰسِقِينَ

Basi aliwachezea watu wake, na wakamtii. Kwa hakika hao walikuwa watu wapotovu



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 55

فَلَمَّآ ءَاسَفُونَا ٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ فَأَغۡرَقۡنَٰهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Walipotukasirisha tuliwapatiliza tukawazamisha wote!



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 56

فَجَعَلۡنَٰهُمۡ سَلَفٗا وَمَثَلٗا لِّلۡأٓخِرِينَ

Kisha tukawafanya kuwa watan-gulizi na mfano kwa watakaokuja baadae



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 17

۞وَلَقَدۡ فَتَنَّا قَبۡلَهُمۡ قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَ وَجَآءَهُمۡ رَسُولٞ كَرِيمٌ

Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 18

أَنۡ أَدُّوٓاْ إِلَيَّ عِبَادَ ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Akasema: Nipeni waja wa Allah; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 19

وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Na msimfanyie kiburi Allah; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 20

وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ

Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 21

وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ

Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 22

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ مُّجۡرِمُونَ

Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 23

فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Allah akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 24

وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٞ مُّغۡرَقُونَ

Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 25

كَمۡ تَرَكُواْ مِن جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 26

وَزُرُوعٖ وَمَقَامٖ كَرِيمٖ

Na mimea na vyeo vitukufu!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 27

وَنَعۡمَةٖ كَانُواْ فِيهَا فَٰكِهِينَ

Na neema walizokuwa wakiji-stareheshea!



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 28

كَذَٰلِكَۖ وَأَوۡرَثۡنَٰهَا قَوۡمًا ءَاخَرِينَ

Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 29

فَمَا بَكَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّمَآءُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَا كَانُواْ مُنظَرِينَ

Hazikuwalilia mbingu wala ardhi, wala hawakupewa muhula



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 30

وَلَقَدۡ نَجَّيۡنَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ مِنَ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡمُهِينِ

Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 31

مِن فِرۡعَوۡنَۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَالِيٗا مِّنَ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka



السورة: ADH-DHAARIYAAT 

الآية : 38

وَفِي مُوسَىٰٓ إِذۡ أَرۡسَلۡنَٰهُ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Na katika khabari za mussa pale tulipompeleka kwa Firauni kwa hoja za wazi