السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 21

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱعۡبُدُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ

Enyi watu, muabuduni Mola wenu ambaye amekuumbeni na (ameumba) waliokuwepo kabla yenu ili muwe Wacha Mungu



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 168

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ كُلُواْ مِمَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ حَلَٰلٗا طَيِّبٗا وَلَا تَتَّبِعُواْ خُطُوَٰتِ ٱلشَّيۡطَٰنِۚ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٌ

Enyi watu, kuleni vilivyomo katika ardhi vikiwa halali na vizuri. Na msifuate nyendo za shetani kwa sababu, bila ya shaka, yeye kwenu ni adui aliye wazi



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 281

وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا تُرۡجَعُونَ فِيهِ إِلَى ٱللَّهِۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na iogopeni siku ambayo mtarejeshwa kwa Allah, kisha kila mtu atalipwa kikamilifu aliyoyachuma, nao hawatadhulumiwa



السورة: ANNISAI 

الآية : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمُ ٱلَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفۡسٖ وَٰحِدَةٖ وَخَلَقَ مِنۡهَا زَوۡجَهَا وَبَثَّ مِنۡهُمَا رِجَالٗا كَثِيرٗا وَنِسَآءٗۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِي تَسَآءَلُونَ بِهِۦ وَٱلۡأَرۡحَامَۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلَيۡكُمۡ رَقِيبٗا

Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi Ambaye amekuumbeni kutokana na nafsi moja tu na ameumba kutoka kwenye nafsi hiyo mke wake (Hawaa), na akaeneza kutokana na wawili hao wanaume wengi na wanawake (wengi), na mcheni Allah Ambaye mnaombana kupitia yeye, na (ogopeni kukata) udugu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye kukufuatilieni kwa karibu sana



السورة: ANNISAI 

الآية : 58

۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تُؤَدُّواْ ٱلۡأَمَٰنَٰتِ إِلَىٰٓ أَهۡلِهَا وَإِذَا حَكَمۡتُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ أَن تَحۡكُمُواْ بِٱلۡعَدۡلِۚ إِنَّ ٱللَّهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ سَمِيعَۢا بَصِيرٗا

Hakika, Allah anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe, na mnapo hukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika, mazuri mno anayokuwaidhini Allah ni hayo. HakikaAllah ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kuona



السورة: ANNISAI 

الآية : 170

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلرَّسُولُ بِٱلۡحَقِّ مِن رَّبِّكُمۡ فَـَٔامِنُواْ خَيۡرٗا لَّكُمۡۚ وَإِن تَكۡفُرُواْ فَإِنَّ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Enyi watu, hakika amekujieni Mtume kwa haki kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi aminini, iwe kheri kwenu. Na mkikufuru basi hakika ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Na Allah ni Mjuzi sana, Mwenye hekima



السورة: IBRAHIM 

الآية : 52

هَٰذَا بَلَٰغٞ لِّلنَّاسِ وَلِيُنذَرُواْ بِهِۦ وَلِيَعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَلِيَذَّكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hii (Qur’ani) ni ufikisho (wa ujumbe) kwa watu, na ili waonywe na ili wapate kujua kuwa, uhakika ni kwamba Yeye (Allah) ni Muabudiwa mmoja tu, na ili wenye akili wapate kuonyeka



السورة: AL-ISRAA 

الآية : 89

وَلَقَدۡ صَرَّفۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ فَأَبَىٰٓ أَكۡثَرُ ٱلنَّاسِ إِلَّا كُفُورٗا

Na hakika tumewaeleza watu katika hii Qur’ani kwa kila mfano. Lakini watu wengi wanakataa isipo kuwa kukanusha tu



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمۡۚ إِنَّ زَلۡزَلَةَ ٱلسَّاعَةِ شَيۡءٌ عَظِيمٞ

Enyi watu, mcheni Mola wenu Mlezi. Hakika tetemeko la Kiyama ni jambo kubwa mno



السورة: LUQMAAN 

الآية : 33

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱتَّقُواْ رَبَّكُمۡ وَٱخۡشَوۡاْ يَوۡمٗا لَّا يَجۡزِي وَالِدٌ عَن وَلَدِهِۦ وَلَا مَوۡلُودٌ هُوَ جَازٍ عَن وَالِدِهِۦ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِٱللَّهِ ٱلۡغَرُورُ

Enyi watu! Mcheni Mola wenu Mlezi, na iogopeni siku ambayo mzazi hatamfaa mwana, wala mwana hatamfaa mzazi kwa lolote. Hakika ahadi ya Allah ni ya kweli. Basi yasikudanganyeni maisha ya dunia, wala asikudanganyeni juu ya Allah mdanganyifu



السورة: FAATWIR 

الآية : 3

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ ٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡۚ هَلۡ مِنۡ خَٰلِقٍ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَرۡزُقُكُم مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِۚ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ

Enyi watu, kumbukeni neema za Allah kwenu. Ati yupo Muumba mwingine asiyekuwa Allah anayekupeni riziki kutoka mbinguni na ardhini? Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa ila Yeye tu. Basi vipi mnageuzwa (mnapotoshwa)?



السورة: FAATWIR 

الآية : 5

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞۖ فَلَا تَغُرَّنَّكُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَلَا يَغُرَّنَّكُم بِٱللَّهِ ٱلۡغَرُورُ

Enyi watu! Hakika ahadi ya Allah ni ya kweli. Basi yasiku-danganyeni maisha ya dunia, wala mdanganyifu asikudanganyeni juu ya Allah



السورة: FAATWIR 

الآية : 6

إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمۡ عَدُوّٞ فَٱتَّخِذُوهُ عَدُوًّاۚ إِنَّمَا يَدۡعُواْ حِزۡبَهُۥ لِيَكُونُواْ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلسَّعِيرِ

Hakika Shetani ni adui yenu, basi mfanyeni kuwa ni adui. Kwani yeye analiita kundi lake liwe katika watu wa Motoni