السورة: AL-QAMAR

الآية : 55

فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ

Katika kizazi kilichoridhiwa mbele ya Mfalme aliye Muweza



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 46

وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ

Na kwa mwenye kukhofu kusi-mamishwa mbele ya Mola wake atapata bustani mbili



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema



السورة: AL-QALAM 

الآية : 34

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 23

ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ

Ambao wenye kudumisha Sala zao



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 24

وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ

Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 25

لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ

Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 26

وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ

Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 27

وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 28

إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ

Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 29

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ

Na ambao wanahifadhi tupu zao



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 30

إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ

Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 31

فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ

Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 32

وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ

Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuzichunga (na kuzitimiza)



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 33

وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ

Na ambao wanasimama imara katika kutoa ushahidi wao,



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 34

وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ

Na ambao kwenye Sala zao ni wenye kuzilinda



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 35

أُوْلَـٰٓئِكَ فِي جَنَّـٰتٖ مُّكۡرَمُونَ

Hao ndio watakao heshimiwa Peponi



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 41

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ

Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchem



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 42

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ

Na matunda katika yale wanayoyatamani



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 43

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

(Wataabiwa): Kuleni na kunyweni kwa furaha kwasababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 44

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika sisi ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema



السورة: ANNAAZIAAT 

الآية : 40

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ

Ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi yake na na matamanio



السورة: ANNAAZIAAT 

الآية : 41

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!



السورة: AL-MUTWAFFIFIIN 

الآية : 22

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema



السورة: AL-MUTWAFFIFIIN 

الآية : 23

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia



السورة: AL-MUTWAFFIFIIN 

الآية : 24

تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ

Utatambua katika nyuso zao mng’aro wa neema,



السورة: AL-BURUJI 

الآية : 11

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ

Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa



السورة: AL-FAJRI 

الآية : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!