السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 46

بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّـٰرِبِينَ

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 47

لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 48

وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri



السورة: ASSWAAFFAAT 

الآية : 49

كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 71

يُطَافُ عَلَيۡهِم بِصِحَافٖ مِّن ذَهَبٖ وَأَكۡوَابٖۖ وَفِيهَا مَا تَشۡتَهِيهِ ٱلۡأَنفُسُ وَتَلَذُّ ٱلۡأَعۡيُنُۖ وَأَنتُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Watakuwa wanapitishiwa sahani za dhahabu na vikombe; na vitakuwamo ambavyo nafsi zinavipenda na macho yanavifurahia, na nyinyi mtakaa humo milele



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 72

وَتِلۡكَ ٱلۡجَنَّةُ ٱلَّتِيٓ أُورِثۡتُمُوهَا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na hiyo ni Pepo mliyo rithishwa kwa hayo mliyo kuwa mkiyafanya



السورة: AZZUKHRUF 

الآية : 73

لَكُمۡ فِيهَا فَٰكِهَةٞ كَثِيرَةٞ مِّنۡهَا تَأۡكُلُونَ

Mnayo humo matunda mengi mtakayo yala



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 51

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٖ

Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 52

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani na chemchem



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 53

يَلۡبَسُونَ مِن سُندُسٖ وَإِسۡتَبۡرَقٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 54

كَذَٰلِكَ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurulaini



السورة: ADDUKHAAN 

الآية : 55

يَدۡعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَٰكِهَةٍ ءَامِنِينَ

Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani



السورة: MUHAMMAD 

الآية : 15

مَّثَلُ ٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِي وُعِدَ ٱلۡمُتَّقُونَۖ فِيهَآ أَنۡهَٰرٞ مِّن مَّآءٍ غَيۡرِ ءَاسِنٖ وَأَنۡهَٰرٞ مِّن لَّبَنٖ لَّمۡ يَتَغَيَّرۡ طَعۡمُهُۥ وَأَنۡهَٰرٞ مِّنۡ خَمۡرٖ لَّذَّةٖ لِّلشَّـٰرِبِينَ وَأَنۡهَٰرٞ مِّنۡ عَسَلٖ مُّصَفّٗىۖ وَلَهُمۡ فِيهَا مِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِ وَمَغۡفِرَةٞ مِّن رَّبِّهِمۡۖ كَمَنۡ هُوَ خَٰلِدٞ فِي ٱلنَّارِ وَسُقُواْ مَآءً حَمِيمٗا فَقَطَّعَ أَمۡعَآءَهُمۡ

Mfano wa Pepo walio ahidiwa wachamungu ina mito ya maji yasiyo vunda, na mito ya maziwa yasiyo haribika ladha yake, na mito ya mvinyo yenye ladha kwa wanywao, na mito ya asali iliyo safishwa. Na wao humo watakuwa na kila namna ya matunda, na msamaha kutoka kwa Mola wao Mlezi. Basi hao ni kama watakao dumu Motoni na wakinyweshwa maji yanayo chemka ya kuwakata matumbo yao?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 46

وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ

Na kwa mwenye kukhofu kusi-mamishwa mbele ya Mola wake atapata bustani mbili



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 47

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 48

ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ

Zenye miti yenye matawi



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 49

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 50

فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ

Mna humo chemchemu mbili zinazopita



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 51

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 52

فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ

Mna humo kila matunda ya aina mbili mbili



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 53

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 54

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ

Hali yakuwa wakiegemea kwenye matandiko mazito yaliyotengenezwa ndani yake kwa hariri nyepesi na matunda ya bustani hizo yapo karibu



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 55

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 56

فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ

Mna humo wanawake wenye staha wanaoinamisha macho, hawajaguswa na Mtu kabla yao wala Jini



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 57

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 58

كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ

Kana kwamba hao wanawake ni yakuti na marijani



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 59

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 60

هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ

Haikua malipo ya wema ispokua wema



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 61

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



السورة: ARRAHMAAN 

الآية : 62

وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ

Na zaidi ya hizo mbili, ziko bustani mbili zingine