ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ
Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Bwana wako ni Mwingi wa msamaha. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ
Amemuumba mwanadamu kutokana na udongo utowao sauti kama vyombo vya udongo vilivyochomwa
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?
وَٱللَّهُ أَنۢبَتَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ نَبَاتٗا
Na Allah amekuotesheni (Amekuanzisheni vizuri katika udongo) wa ardhi kama mimea
أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ
Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?
فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke
هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا
Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa
إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا
Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ
Kwani hatukukuumbeni kwa maji dhalili (manii)?
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ
Kisha Tukayaweka katika mahali pa kutulia, madhubuti?
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ
Mpaka muda maalumu?
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ
Tukakadiria na Sisi ni wazuri walioje wa kukadiria
مِنۡ أَيِّ شَيۡءٍ خَلَقَهُۥ
Hivi hakumbuki! Kwa kitu gani amemuumba?
مِن نُّطۡفَةٍ خَلَقَهُۥ فَقَدَّرَهُۥ
Kutokana na tone la manii, Amemuumba, Akamkadiria, [Akamuwezesha]
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu