السورة: AL-HIJRI 

الآية : 73

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ

Basi (ghafla) Ukelele mkali uliwachukua kipindi cha mapam-bazuko



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 74

فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ

Na tukaigeuza nchi (yao) juu chini chini juu, na tukawanyeshea (mvua ya) mawe ya udongo wa Motoni



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 75

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu iliyowapata watu wa Lutwi) zipo ishara kwa wanaozingatia



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 76

وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ

Na (kitongoji cha watu wa Lutwi) kipo kwenye barabara ipitwayo (na watu wanaokwenda Sham)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 77

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu) ipo ishara (na mazingatio) kwa Waumini



السورة: AL-ANBIYAA 

الآية : 74

وَلُوطًا ءَاتَيۡنَٰهُ حُكۡمٗا وَعِلۡمٗا وَنَجَّيۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡقَرۡيَةِ ٱلَّتِي كَانَت تَّعۡمَلُ ٱلۡخَبَـٰٓئِثَۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمَ سَوۡءٖ فَٰسِقِينَ

Na Lutwi tukampa hukumu na elimu na tukamuokoa na ule mji ulio kuwa ukifanya maovu. Hakika hao walikuwa watu wabaya, wachafu



السورة: AL-ANBIYAA 

الآية : 75

وَأَدۡخَلۡنَٰهُ فِي رَحۡمَتِنَآۖ إِنَّهُۥ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tukamuingiza katika rehema yetu. Hakika yeye ni miongoni mwa watenda mema



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 160

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Watu wa Lutwi waliwakanusha Mitume



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 161

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ لُوطٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao, Lutwi: Je! Hamumchi Allah?



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 162

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 163

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah na nitiini mimi



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 164

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala mimi sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 165

أَتَأۡتُونَ ٱلذُّكۡرَانَ مِنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Je! mnawaingilia wanaume katika walimwengu?



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 166

وَتَذَرُونَ مَا خَلَقَ لَكُمۡ رَبُّكُم مِّنۡ أَزۡوَٰجِكُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٌ عَادُونَ

Na mnaacha alicho kuumbieni Mola wenu Mlezi katika wake zenu? Ama kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka!



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 167

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰلُوطُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُخۡرَجِينَ

Wakasema: Ewe Lutwi! Usipo acha, hapana shaka utakuwa miongoni mwa wanao tolewa mji!



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 168

قَالَ إِنِّي لِعَمَلِكُم مِّنَ ٱلۡقَالِينَ

Akasema: Hakika mimi ni katika wanao kichukia hichi kitendo chenu



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 169

رَبِّ نَجِّنِي وَأَهۡلِي مِمَّا يَعۡمَلُونَ

Mola wangu Mlezi! Niokoe mimi na ahali zangu na haya wayatendayo



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 170

فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake wote,



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 171

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipokuwa kikongwe katika waliokaa nyuma



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 172

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengine



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 173

وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Na tukawanyeshea mvua, basi ni mbaya mno mvua ya waliyoonywa



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 174

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo Ishara. Na hawakuwa wengi wao wenye kuamini



السورة: ASH-SHUARAA 

الآية : 175

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu



السورة: ANNAMLI 

الآية : 54

وَلُوطًا إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِۦٓ أَتَأۡتُونَ ٱلۡفَٰحِشَةَ وَأَنتُمۡ تُبۡصِرُونَ

Na Lutwi alipo waambia watu wake: Je! Mnafanya uchafu nanyi mnaona?



السورة: ANNAMLI 

الآية : 55

أَئِنَّكُمۡ لَتَأۡتُونَ ٱلرِّجَالَ شَهۡوَةٗ مِّن دُونِ ٱلنِّسَآءِۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ تَجۡهَلُونَ

Hivyo nyinyi mnawaingilia wanaume kwa matamanio badala ya wanawake? Hakika nyinyi ni watu mnao fanya ujinga kabisa!



السورة: ANNAMLI 

الآية : 56

۞فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُوٓاْ أَخۡرِجُوٓاْ ءَالَ لُوطٖ مِّن قَرۡيَتِكُمۡۖ إِنَّهُمۡ أُنَاسٞ يَتَطَهَّرُونَ

Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Wafukuzeni wafwasi wa Lutwi katika mji wenu. Hao ni watu wanao jitia usafi



السورة: ANNAMLI 

الآية : 57

فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَٰهَا مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Basi tukamwokoa yeye na ahali zake, isipo kuwa mkewe; tukamkadiria katika walio baki nyuma



السورة: ANNAMLI 

الآية : 58

وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِم مَّطَرٗاۖ فَسَآءَ مَطَرُ ٱلۡمُنذَرِينَ

Na tukawanyeshea mvua. Ni mbaya kweli kweli hiyo mvua ya walio kwisha onywa



السورة: AL-ANKABUUT 

الآية : 26

۞فَـَٔامَنَ لَهُۥ لُوطٞۘ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّيٓۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Lutwi akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima



السورة: AL-ANKABUUT 

الآية : 31

وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُوٓاْ إِنَّا مُهۡلِكُوٓاْ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِۖ إِنَّ أَهۡلَهَا كَانُواْ ظَٰلِمِينَ

Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawaangamiza watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu