أَنَّا صَبَبۡنَا ٱلۡمَآءَ صَبّٗا
Hakika Sisi tumemimina maji kwa nguvu
ثُمَّ شَقَقۡنَا ٱلۡأَرۡضَ شَقّٗا
Kisha Tukaipasua ardhi mipasuko
فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا حَبّٗا
Kisha tukaotesha humo nafaka mbali mbali
وَعِنَبٗا وَقَضۡبٗا
Na mizabibu na mimea ya mboga (ikatwayo ikamea tena)
وَزَيۡتُونٗا وَنَخۡلٗا
Na mizaituni na mitende
وَحَدَآئِقَ غُلۡبٗا
Na mabustani yaliyositawi na kusongamana miti yake
وَفَٰكِهَةٗ وَأَبّٗا
Na matunda na majani ya malisho ya wanyama
مَّتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ
Ni manufaa kwenu na kwa wanyama wenu wa mifugo
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ
Hebu na ajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ
Hakika Yeye ana uwezo wa kumrudisha
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa (simamishwa)?
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ
Soma kwa jina la Mola wako Mlezi ambaye ameumba