السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 281

وَٱتَّقُواْ يَوۡمٗا تُرۡجَعُونَ فِيهِ إِلَى ٱللَّهِۖ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na iogopeni siku ambayo mtarejeshwa kwa Allah, kisha kila mtu atalipwa kikamilifu aliyoyachuma, nao hawatadhulumiwa



السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 282

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِذَا تَدَايَنتُم بِدَيۡنٍ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى فَٱكۡتُبُوهُۚ وَلۡيَكۡتُب بَّيۡنَكُمۡ كَاتِبُۢ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَلَا يَأۡبَ كَاتِبٌ أَن يَكۡتُبَ كَمَا عَلَّمَهُ ٱللَّهُۚ فَلۡيَكۡتُبۡ وَلۡيُمۡلِلِ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ وَلۡيَتَّقِ ٱللَّهَ رَبَّهُۥ وَلَا يَبۡخَسۡ مِنۡهُ شَيۡـٔٗاۚ فَإِن كَانَ ٱلَّذِي عَلَيۡهِ ٱلۡحَقُّ سَفِيهًا أَوۡ ضَعِيفًا أَوۡ لَا يَسۡتَطِيعُ أَن يُمِلَّ هُوَ فَلۡيُمۡلِلۡ وَلِيُّهُۥ بِٱلۡعَدۡلِۚ وَٱسۡتَشۡهِدُواْ شَهِيدَيۡنِ مِن رِّجَالِكُمۡۖ فَإِن لَّمۡ يَكُونَا رَجُلَيۡنِ فَرَجُلٞ وَٱمۡرَأَتَانِ مِمَّن تَرۡضَوۡنَ مِنَ ٱلشُّهَدَآءِ أَن تَضِلَّ إِحۡدَىٰهُمَا فَتُذَكِّرَ إِحۡدَىٰهُمَا ٱلۡأُخۡرَىٰۚ وَلَا يَأۡبَ ٱلشُّهَدَآءُ إِذَا مَا دُعُواْۚ وَلَا تَسۡـَٔمُوٓاْ أَن تَكۡتُبُوهُ صَغِيرًا أَوۡ كَبِيرًا إِلَىٰٓ أَجَلِهِۦۚ ذَٰلِكُمۡ أَقۡسَطُ عِندَ ٱللَّهِ وَأَقۡوَمُ لِلشَّهَٰدَةِ وَأَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَرۡتَابُوٓاْ إِلَّآ أَن تَكُونَ تِجَٰرَةً حَاضِرَةٗ تُدِيرُونَهَا بَيۡنَكُمۡ فَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَلَّا تَكۡتُبُوهَاۗ وَأَشۡهِدُوٓاْ إِذَا تَبَايَعۡتُمۡۚ وَلَا يُضَآرَّ كَاتِبٞ وَلَا شَهِيدٞۚ وَإِن تَفۡعَلُواْ فَإِنَّهُۥ فُسُوقُۢ بِكُمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ وَيُعَلِّمُكُمُ ٱللَّهُۗ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Enyi mliyoamini, mnapoko-peshana mkopo wowote kwa muda maalum, basi uandikeni. Na mwandishi aandike baina yenu kwa uadilifu. Na mwandishi asikatae kuandika. Aandike kama Allah alivyomfunza. Hivyo basi, aandike na ni juu ya mdaiwa kutoa maneno ya kuandikwa na amwogope Allah, Mola wake Mlezi, na asipunguze chochote ndani yake. Na kama yule anayedaiwa ni alie pumbaa mnyonge, au hawezi kuandikisha mwenyewe, basi msimamizi wake aandikishe kwa uadilifu. Na shuhudisheni mashahidi wawili wanaume waaminifu sana miongoni mwenu. Na iwapo hakuna wanaume wawili, basi (apatikane) mwanaume mmoja na wanawake wawili katika wale mnaowaridhia kuwa mashahidi, ili kama atasahau mmoja wa wanawake wawili, yule mwingine amkumbushe mwenzake. Na mashahidi wasikatae wanapoitwa. Na msikimwe kuliandika deni, likiwa dogo au kubwa, mpaka muda wake. Jambo hilo kwenu ni uadilifu zaidi mbele ya Allah, na sahihi zaidi kwa ushahidi, na pia inakurubisha mno kutokuwa na shaka, isipokuwa kama ni biashara mnayofanya kati yenu papo hapo, basi si dhambi kwenu msipoiandika. Na mnapouziana wekeni mashahidi. Wala asitiwe matatani mwandishi wala shahidi, na kama mkifanya hivyo (kuwatia matatani), basi kwa hakika huo ni uovu mkubwa kwenu. Na mwogopeni Allah, na Allah ndiye ana kuelimisheni; na Allah ni Mjuzi mno wa kila kitu



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 18

شَهِدَ ٱللَّهُ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَأُوْلُواْ ٱلۡعِلۡمِ قَآئِمَۢا بِٱلۡقِسۡطِۚ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Allah Ameshuhudia kwamba, hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu, na Malaika (pia wameshudia hivyo) na wenye elimu, akisimamia uadilifu. Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima nyingi



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 25

فَكَيۡفَ إِذَا جَمَعۡنَٰهُمۡ لِيَوۡمٖ لَّا رَيۡبَ فِيهِ وَوُفِّيَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Basi itakuwaje tutakapo-wakusanya kwa ajili ya siku ambayo haina shaka, na kila nafsi italipwa kwa ukamilifu kutokana na ilichokichuma na wao hawatadhulumiwa?



السورة: AL-IMRAN 

الآية : 64

قُلۡ يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ كَلِمَةٖ سَوَآءِۭ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمۡ أَلَّا نَعۡبُدَ إِلَّا ٱللَّهَ وَلَا نُشۡرِكَ بِهِۦ شَيۡـٔٗا وَلَا يَتَّخِذَ بَعۡضُنَا بَعۡضًا أَرۡبَابٗا مِّن دُونِ ٱللَّهِۚ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَقُولُواْ ٱشۡهَدُواْ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ

Sema: Enyi Watu wa Kitabu: Njooni kwenye neno la sawa kati yetu na kati yenu ya kuwa, tusimuabudu isipokuwa Allah tu, wala tusimshirikishe na chochote, na tusiwafanye baadhi yetu Miungu badala ya Allah. Na kama watapuuza, basi semeni (muwaambie): Shuhudieni kuwa sisi ni Waislamu



السورة: ANNISAI 

الآية : 3

وَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا تُقۡسِطُواْ فِي ٱلۡيَتَٰمَىٰ فَٱنكِحُواْ مَا طَابَ لَكُم مِّنَ ٱلنِّسَآءِ مَثۡنَىٰ وَثُلَٰثَ وَرُبَٰعَۖ فَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا تَعۡدِلُواْ فَوَٰحِدَةً أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُكُمۡۚ ذَٰلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَلَّا تَعُولُواْ

Na kama mtaogopa kutofanya uadilifu kwa Yatima, basi oeni wale mliowaridhia miongoni mwa wanawake, wawili wawili na watatu watatu na wane wane. Na kama mtahofia kutofanya uadilifu, basi oeni mmoja tu au (oeni vijakazi) mnaowamiliki. Kufanya hivyo kutawasogeza karibu zaidi ya kuacha dhuluma



السورة: ANNISAI 

الآية : 58

۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تُؤَدُّواْ ٱلۡأَمَٰنَٰتِ إِلَىٰٓ أَهۡلِهَا وَإِذَا حَكَمۡتُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ أَن تَحۡكُمُواْ بِٱلۡعَدۡلِۚ إِنَّ ٱللَّهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ سَمِيعَۢا بَصِيرٗا

Hakika, Allah anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe, na mnapo hukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika, mazuri mno anayokuwaidhini Allah ni hayo. HakikaAllah ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kuona



السورة: ANNISAI 

الآية : 65

فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤۡمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيۡنَهُمۡ ثُمَّ لَا يَجِدُواْ فِيٓ أَنفُسِهِمۡ حَرَجٗا مِّمَّا قَضَيۡتَ وَيُسَلِّمُواْ تَسۡلِيمٗا

Hapana; nina apa kwa Mola wako kwamba, (watu) hawawi waumini mpaka wakufanye wewe kuwa muamuzi katika migogoro inayotokea baina yao, kisha wasihisi uzito wowote (au mashaka) katika nafsi zao kutokana na hukumu uliyoitoa na waonyeshe utiifu kamili



السورة: ANNISAI 

الآية : 105

إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِتَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ بِمَآ أَرَىٰكَ ٱللَّهُۚ وَلَا تَكُن لِّلۡخَآئِنِينَ خَصِيمٗا

Hakika, sisi tumekuteremshia kitabu kwa haki ili uhukumu baina ya watu kwa kile ambacho Allah amekuonyesha (amekuelimisha). Na usiwe mtetezi wa wanaofanya khiana



السورة: ANNISAI 

الآية : 129

وَلَن تَسۡتَطِيعُوٓاْ أَن تَعۡدِلُواْ بَيۡنَ ٱلنِّسَآءِ وَلَوۡ حَرَصۡتُمۡۖ فَلَا تَمِيلُواْ كُلَّ ٱلۡمَيۡلِ فَتَذَرُوهَا كَٱلۡمُعَلَّقَةِۚ وَإِن تُصۡلِحُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Na hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wanawake (wake zenu) hata kama mtafanya jitihada. Basi (pamoja na hayo) msimili (msielemee) moja kwa moja (kwa mke mmoja), mkamuacha mwingine kama aliyetundikwa (aliyening’inizwa).[1] Na kama mtafanya usuluhishi na mkamcha Allah, hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehem


1- - Waume wanakatazwa kutofanya uadilifu baina ya wake zao kwa kutotoa huduma stahiki kwa usawa au kwa kutelekeza baadhi. Hili halihusu mume mwenye wake zaidi ya mmoja tu, lakini linamhusu hata mume mwenye mke mmoja. Mume mwenye mke mmoja pia haruhusiwi kutomtendea uadilifu mkewe kwa kutompa haki zake au kwa kumtelekeza na kumuweka katika mazingira ya kutojitambua kwamba ni mke au sio mke. Uadilifu unaokusudia na sheria ni uadilifu wa huduma na sio hisia za mvuto, mahaba na mapenzi ya moyoni.


السورة: ANNISAI 

الآية : 135

۞يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُواْ قَوَّـٰمِينَ بِٱلۡقِسۡطِ شُهَدَآءَ لِلَّهِ وَلَوۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِكُمۡ أَوِ ٱلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَۚ إِن يَكُنۡ غَنِيًّا أَوۡ فَقِيرٗا فَٱللَّهُ أَوۡلَىٰ بِهِمَاۖ فَلَا تَتَّبِعُواْ ٱلۡهَوَىٰٓ أَن تَعۡدِلُواْۚ وَإِن تَلۡوُۥٓاْ أَوۡ تُعۡرِضُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٗا

Enyi mlioamini, kuweni wasimamishaji uadilifu, wenye kutoa ushahidi kwa ajili ya Allah hata kama (uadilifu na ushahidi huo) ni dhidi ya nafsi zenu au wazazi na ndugu wa karibu. Ikiwa (anayetakiwa kutolewa ushahidi) ni tajiri au fukara (msipindishe ushahidi kwasababu) Allah ni bora zaidi kwao (kuliko nyinyi[1] Basi msifuate matamanio ya nafsi zenu mkaacha kutenda uadilifu. Na kama mtapotosha (ushahidi) au mtapuuza (kwa kuacha kuutoa) basi ni hakika Allah anayajua yote mnayotenda


1- - . Allah anasisitiza kuwa yeye ndiye Muumba wa Tajiri na maskini na anataka haki itendeke kwa wote. Ushahidi utolewe bila ya kuangalia utajiri wa mtu au umaskini wake.


السورة: AL-MAIDA 

الآية : 8

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُواْ قَوَّـٰمِينَ لِلَّهِ شُهَدَآءَ بِٱلۡقِسۡطِۖ وَلَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شَنَـَٔانُ قَوۡمٍ عَلَىٰٓ أَلَّا تَعۡدِلُواْۚ ٱعۡدِلُواْ هُوَ أَقۡرَبُ لِلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Enyi miloamini, kuweni wasimamizi (wa haki) kwa ajili ya Allah, mtoao ushahidi kwa uadilifu. Na kuwachukia (watu) kusikupelekeeni kutofanya uadilifu. Fanyeni uadilifu (kwa watu wote). Hilo ndilo lililo karibu zaidi (kufikisha) kwenye uchamungu. Na mcheni Allah. Hakika, Allah anayajua mnayoyatenda



السورة: AL-MAIDA 

الآية : 42

سَمَّـٰعُونَ لِلۡكَذِبِ أَكَّـٰلُونَ لِلسُّحۡتِۚ فَإِن جَآءُوكَ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُمۡ أَوۡ أَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡۖ وَإِن تُعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ فَلَن يَضُرُّوكَ شَيۡـٔٗاۖ وَإِنۡ حَكَمۡتَ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُقۡسِطِينَ

(Hao ni) Wasikilizaji sana wa uwongo, walaji sana wa haramu. Basi wakikujia, wahukumu baina yao au wapuuze[1]. Na ukiwapuuza, katu hawatakudhuru kitu chochote. Na ukihukumu, basi hukumu baina yao kwa uadilifu. Hakika, Allah anawapenda waadilifu


1- - Amri hii ya kupuuza imefutwa kwa Aya ya 49 ya Sura hii hii ya Almaida (5) inayolazimisha kutekelezwa kwa hukumu bila ya kuwa na hiari ya kupuuza.


السورة: AL-MAIDA 

الآية : 45

وَكَتَبۡنَا عَلَيۡهِمۡ فِيهَآ أَنَّ ٱلنَّفۡسَ بِٱلنَّفۡسِ وَٱلۡعَيۡنَ بِٱلۡعَيۡنِ وَٱلۡأَنفَ بِٱلۡأَنفِ وَٱلۡأُذُنَ بِٱلۡأُذُنِ وَٱلسِّنَّ بِٱلسِّنِّ وَٱلۡجُرُوحَ قِصَاصٞۚ فَمَن تَصَدَّقَ بِهِۦ فَهُوَ كَفَّارَةٞ لَّهُۥۚ وَمَن لَّمۡ يَحۡكُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Na humo (ndani ya Taurati) tumewaandikia ya kwamba, roho kwa roho na jicho kwa jicho na pua kwa pua na sikio kwa sikio na jino kwa jino na majeraha ni kisasi. Basi atakayetoa sadaka (ya kusamehe haki yake kulipa kisasi) hiyo ni kafara yake (ya madhambi yake). Na wasiohukumu kwa (sheria) aliyoiteremsha Allah, basi hao ndio madhalimu



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 152

وَلَا تَقۡرَبُواْ مَالَ ٱلۡيَتِيمِ إِلَّا بِٱلَّتِي هِيَ أَحۡسَنُ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ أَشُدَّهُۥۚ وَأَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَٱلۡمِيزَانَ بِٱلۡقِسۡطِۖ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۖ وَإِذَا قُلۡتُمۡ فَٱعۡدِلُواْ وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰۖ وَبِعَهۡدِ ٱللَّهِ أَوۡفُواْۚ ذَٰلِكُمۡ وَصَّىٰكُم بِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ

Na msizisogelee mali za Yatima ila kwa njia iliyo nzuri sana hadi afikie utu uzima wake. Na timizeni vipimo na mizani kwa uadilifu. Hatuilazimishi nafsi (jambo lolote) isipokuwa kwa kadiri ya vile iwezavyo. Na msemapo semeni kwa uadilifu hata ikiwa (ni dhidi ya) ndugu. Na ahadi za Allah zitekelezeni. Hayo amekuusieni (Allah) ili mpate kukumbuka



السورة: AL-AN’AAM 

الآية : 161

قُلۡ إِنَّنِي هَدَىٰنِي رَبِّيٓ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ دِينٗا قِيَمٗا مِّلَّةَ إِبۡرَٰهِيمَ حَنِيفٗاۚ وَمَا كَانَ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Sema: Kwa hakika, mimi ameniongoza Mola wangu Mlezi kwenye njia iliyo nyooka; dini iliyo sawa kabisa, mila ya Ibrahimu aliyeacha itikadi zote potofu na hakuwa miongoni mwa washirikina



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 29

قُلۡ أَمَرَ رَبِّي بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَقِيمُواْ وُجُوهَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَٱدۡعُوهُ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَۚ كَمَا بَدَأَكُمۡ تَعُودُونَ

Sema: Mola wangu Mlezi ameamrisha (kufanya) uadilifu. Na elekezeni nyuso zenu kila mnaposwali (mkusudieni Allah kila mfanyapo ibada) na muabuduni yeye tu mkimtakasia dini. Kama (Allah) ambavyo amekuumbeni mwanzo ndivyo mtakavyorudi



السورة: YUNUS 

الآية : 47

وَلِكُلِّ أُمَّةٖ رَّسُولٞۖ فَإِذَا جَآءَ رَسُولُهُمۡ قُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na kila umma una Mtume (wake). Basi anapofika Mtume wao watahukumiwa baina yao kwa uadilifu nao hawatadhulumiwa



السورة: YUNUS 

الآية : 54

وَلَوۡ أَنَّ لِكُلِّ نَفۡسٖ ظَلَمَتۡ مَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لَٱفۡتَدَتۡ بِهِۦۗ وَأَسَرُّواْ ٱلنَّدَامَةَ لَمَّا رَأَوُاْ ٱلۡعَذَابَۖ وَقُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡقِسۡطِ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na lau kama kila nafsi iliyodhu-lumu ingekuwa inamiliki vyote vilivyomo duniani, bila shaka yoyote ingevitoa fidia (ili kujikomboa isiadhibiwe). Na watakapoiona adhabu wataficha majuto na patahu-kumiwa baina yao kwa uadilifu, nao hawatadhulumiwa



السورة: ANNAHLI 

الآية : 90

۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُ بِٱلۡعَدۡلِ وَٱلۡإِحۡسَٰنِ وَإِيتَآيِٕ ذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَيَنۡهَىٰ عَنِ ٱلۡفَحۡشَآءِ وَٱلۡمُنكَرِ وَٱلۡبَغۡيِۚ يَعِظُكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ

Kwa hakika Allah anaamuru uadilifu, na ihsani, na kuwapa (sadaka) ndugu wa karibu na anakataza uchafu, na uovu, na uasi. Anawanasihini ili mpate kukumbuka



السورة: ANNAHLI 

الآية : 111

۞يَوۡمَ تَأۡتِي كُلُّ نَفۡسٖ تُجَٰدِلُ عَن نَّفۡسِهَا وَتُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا عَمِلَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Siku ambayo kila nafsi itakuja kujitetea yenyewe, na kila nafsi itapewa sawa na iliyoyafanya, nao hawatadhulumiwa



السورة: AL-ISRAA 

الآية : 71

يَوۡمَ نَدۡعُواْ كُلَّ أُنَاسِۭ بِإِمَٰمِهِمۡۖ فَمَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَأُوْلَـٰٓئِكَ يَقۡرَءُونَ كِتَٰبَهُمۡ وَلَا يُظۡلَمُونَ فَتِيلٗا

Siku tutakapo waita kila kikundi cha watu kwa mujibu wa wakifuatacho - basi atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, basi hao watasoma kitabu chao wala hawatadhulumiwa hata chembe



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 62

وَلَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَاۚ وَلَدَيۡنَا كِتَٰبٞ يَنطِقُ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na hatuilazimishi nafsi ila kwa kadri ya uwezo wake. Na tunacho kitabu kisemacho kweli. Nao hawatadhulumiwa



السورة: AL-AHZAAB 

الآية : 5

ٱدۡعُوهُمۡ لِأٓبَآئِهِمۡ هُوَ أَقۡسَطُ عِندَ ٱللَّهِۚ فَإِن لَّمۡ تَعۡلَمُوٓاْ ءَابَآءَهُمۡ فَإِخۡوَٰنُكُمۡ فِي ٱلدِّينِ وَمَوَٰلِيكُمۡۚ وَلَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٞ فِيمَآ أَخۡطَأۡتُم بِهِۦ وَلَٰكِن مَّا تَعَمَّدَتۡ قُلُوبُكُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمًا

Waiteni kwa baba zao, maana huo ndio uadilifu zaidi mbele ya Allah. Na ikiwa hamwajui baba zao, basi ni ndugu zenu katika Dini, na rafiki zenu. Wala si lawama juu yenu kwa mlivyo kosea. Lakini ipo lawama katika yale ziliyofanya nyoyo zenu kwa makusudi. Na Allah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu



السورة: AZZUMAR 

الآية : 69

وَأَشۡرَقَتِ ٱلۡأَرۡضُ بِنُورِ رَبِّهَا وَوُضِعَ ٱلۡكِتَٰبُ وَجِاْيٓءَ بِٱلنَّبِيِّـۧنَ وَٱلشُّهَدَآءِ وَقُضِيَ بَيۡنَهُم بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na ardhi itang’ara kwa Nuru ya Mola wake Mlezi, na Kitabu kitawekwa, na wataletwa Manabii na mashahidi, na patahukumiwa baina yao kwa haki, wala hawata-dhulumiwa



السورة: AZZUMAR 

الآية : 70

وَوُفِّيَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا عَمِلَتۡ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَا يَفۡعَلُونَ

Na kila nafsi italipwa kwa yale iliyo yafanya, na Yeye anayajua sana wanayo yatenda



السورة: GHAAFIR 

الآية : 20

وَٱللَّهُ يَقۡضِي بِٱلۡحَقِّۖ وَٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِهِۦ لَا يَقۡضُونَ بِشَيۡءٍۗ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ

Na Allah huhukumu kwa haki; lakini hao wanao waomba badala yake hawahukumu chochote. Hakika Allah ndiye Mwenye kusikia Mwenye kuona



السورة: ASH-SHUURAA 

الآية : 15

فَلِذَٰلِكَ فَٱدۡعُۖ وَٱسۡتَقِمۡ كَمَآ أُمِرۡتَۖ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡۖ وَقُلۡ ءَامَنتُ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ مِن كِتَٰبٖۖ وَأُمِرۡتُ لِأَعۡدِلَ بَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ رَبُّنَا وَرَبُّكُمۡۖ لَنَآ أَعۡمَٰلُنَا وَلَكُمۡ أَعۡمَٰلُكُمۡۖ لَا حُجَّةَ بَيۡنَنَا وَبَيۡنَكُمُۖ ٱللَّهُ يَجۡمَعُ بَيۡنَنَاۖ وَإِلَيۡهِ ٱلۡمَصِيرُ

Basi kwa haya waite! Nawe simama sawa sawa kama ulivyo amrishwa, wala usiyafuate matamanio yao. Na sema: Naamini aliyo teremsha Allah katika Vitabu. Na nimeamrishwa nifanye uadilifu baina yenu. Allah ni Mola wetu Mlezi, na Mola wenu Mlezi. Sisi tuna jukumu kwa vitendo vyetu, na nyinyi mna jukumu kwa vitendo vyenu. Hapana kuhojiana baina yetu na nyinyi. Na Allah atatukusanya pamoja, na marejeo ni kwake



السورة: AL-JAATHIYA 

الآية : 22

وَخَلَقَ ٱللَّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّ وَلِتُجۡزَىٰ كُلُّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na Allah ameziumba mbingu na ardhi kwa haki, na ili kila nafsi ilipwe yale iliyo yachuma. Nao hawatadhulumiwa



السورة: AL-AHQAAF 

الآية : 19

وَلِكُلّٖ دَرَجَٰتٞ مِّمَّا عَمِلُواْۖ وَلِيُوَفِّيَهُمۡ أَعۡمَٰلَهُمۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na wote watakuwa na daraja zao mbali mbali kwa waliyo yatenda, na ili awalipe kwa vitendo vyao, na wala hawatadhulumiwa