السورة: ANNISAI 

الآية : 145

إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِي ٱلدَّرۡكِ ٱلۡأَسۡفَلِ مِنَ ٱلنَّارِ وَلَن تَجِدَ لَهُمۡ نَصِيرًا

Hakika, wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa la Moto, na hutampata yeyote wa kuwanusuru



السورة: ATTAUBA 

الآية : 64

يَحۡذَرُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ أَن تُنَزَّلَ عَلَيۡهِمۡ سُورَةٞ تُنَبِّئُهُم بِمَا فِي قُلُوبِهِمۡۚ قُلِ ٱسۡتَهۡزِءُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ مُخۡرِجٞ مَّا تَحۡذَرُونَ

Wanafiki wanaogopa kute-remshiwa Sura itakayowafichulia yaliyomo katika nyoyo zao. Sema (uwaambie na kwa kuwaonya kwamba): Fanyeni mzaha, hakika Allah atayadhidirisha hayo mnayoogopa (yasijulikane)



السورة: ATTAUBA 

الآية : 65

وَلَئِن سَأَلۡتَهُمۡ لَيَقُولُنَّ إِنَّمَا كُنَّا نَخُوضُ وَنَلۡعَبُۚ قُلۡ أَبِٱللَّهِ وَءَايَٰتِهِۦ وَرَسُولِهِۦ كُنتُمۡ تَسۡتَهۡزِءُونَ

Na kwa yakini kabisa, ukiwauliza (wanafiki kuhusu unafiki na dhihaka zao) watasema: Sisi tulikuwa tukipiga porojo na kucheza tu. Sema: Je, mlikuwa mkimfanyia masihara Allah na Aya zake (Qur’an) na Mtume wake?



السورة: ATTAUBA 

الآية : 66

لَا تَعۡتَذِرُواْ قَدۡ كَفَرۡتُم بَعۡدَ إِيمَٰنِكُمۡۚ إِن نَّعۡفُ عَن طَآئِفَةٖ مِّنكُمۡ نُعَذِّبۡ طَآئِفَةَۢ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ مُجۡرِمِينَ

(Enyi wanafiki) Msitoe udhuru; hakika mmekwisha kufuru baada ya kuamini kwenu. Ikiwa tutalisamehe kundi katika nyinyi, tunaliadhibu kundi jingine kwa sababu walikuwa wakosefu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 67

ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتُ بَعۡضُهُم مِّنۢ بَعۡضٖۚ يَأۡمُرُونَ بِٱلۡمُنكَرِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَقۡبِضُونَ أَيۡدِيَهُمۡۚ نَسُواْ ٱللَّهَ فَنَسِيَهُمۡۚ إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ هُمُ ٱلۡفَٰسِقُونَ

Wanafiki wanaume na wanafiki wanawake; wote ni hali moja (wanafanana katika unafiki na kutoamini). Wanaamrisha maovu na wanakataza mema na wanakunja mikono yao (kwa kukataa kutoa katika njia za heri). Wamemsahau Allah, basi naye amejifanya amewasahau (amewaacha na unafiki wao). Hakika, wanafiki ndio waovu hasa



السورة: ATTAUBA 

الآية : 68

وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ هِيَ حَسۡبُهُمۡۚ وَلَعَنَهُمُ ٱللَّهُۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّقِيمٞ

Allah amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri Moto wa Jahanamu wakidumu humo milele. Hilo ndilo linalowatosha, na Allah amewalaani na watapata adhabu ya kudumu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 69

كَٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ كَانُوٓاْ أَشَدَّ مِنكُمۡ قُوَّةٗ وَأَكۡثَرَ أَمۡوَٰلٗا وَأَوۡلَٰدٗا فَٱسۡتَمۡتَعُواْ بِخَلَٰقِهِمۡ فَٱسۡتَمۡتَعۡتُم بِخَلَٰقِكُمۡ كَمَا ٱسۡتَمۡتَعَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُم بِخَلَٰقِهِمۡ وَخُضۡتُمۡ كَٱلَّذِي خَاضُوٓاْۚ أُوْلَـٰٓئِكَ حَبِطَتۡ أَعۡمَٰلُهُمۡ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

(Enyi wanafiki vitendo vyenu vya dhihaka) Ni kama (vya) wale (wanafiki) waliokuwepo kabla yenu. Walikuwa na nguvu mno na mali na watoto zaidi kuliko nyinyi. Basi walistarehe na fungu lao, na nyinyi mstarehe na fungu lenu, kama waliokuwepo kabla yenu walivyostarehe na fungu lao. Na nyinyi mmezama (katika maovu) kama wao walivyozama. Hao ndio ambao vitendo vyao vimeharibika katika dunia na Akhera; na hao ndio waliokula hasara hasa



السورة: ATTAUBA 

الآية : 73

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ جَٰهِدِ ٱلۡكُفَّارَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱغۡلُظۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Ewe Nabii, pambana na makafiri na wanafiki (kwa mbinu za aina zote) na uwe mkali kwao. Na makazi yao ni Jahanamu, na huo ni mwisho mbaya sana



السورة: ATTAUBA 

الآية : 74

يَحۡلِفُونَ بِٱللَّهِ مَا قَالُواْ وَلَقَدۡ قَالُواْ كَلِمَةَ ٱلۡكُفۡرِ وَكَفَرُواْ بَعۡدَ إِسۡلَٰمِهِمۡ وَهَمُّواْ بِمَا لَمۡ يَنَالُواْۚ وَمَا نَقَمُوٓاْ إِلَّآ أَنۡ أَغۡنَىٰهُمُ ٱللَّهُ وَرَسُولُهُۥ مِن فَضۡلِهِۦۚ فَإِن يَتُوبُواْ يَكُ خَيۡرٗا لَّهُمۡۖ وَإِن يَتَوَلَّوۡاْ يُعَذِّبۡهُمُ ٱللَّهُ عَذَابًا أَلِيمٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۚ وَمَا لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٖ

(Wanafiki) Wanaapa kwa (jina la) Allah kuwa hawakusema (hayo maneno yaliyokufikia). Na kwa hakika kabisa, walisema neno la ukafiri na wamekufuru baada ya kusilimu kwao na walikusudia kufanya ambayo hawakuyapata (ya kutaka kumuua Mtume na kuwafukuza Waislamu) na hawakuchukia ila tu kwa sababu Allah na Mtume wake wamewatajirisha (Waislamu kwa kuwapa neema mbali mbali) kutokana na fadhila zake. Basi iwapo watatubu itakuwa heri kwao na wakikengeuka, Allah atawaadhibu adhabu inayoumiza mno (hapa) duniani na (kesho) Akhera, na hawana katika ardhi yeyote wa kuwalinda wala wa kuwanusuru



السورة: ATTAUBA 

الآية : 75

۞وَمِنۡهُم مَّنۡ عَٰهَدَ ٱللَّهَ لَئِنۡ ءَاتَىٰنَا مِن فَضۡلِهِۦ لَنَصَّدَّقَنَّ وَلَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na miongoni mwao (hao wanafiki) wapo waliomuahidi Allah kwamba: Iwapo (Allah) atatupa katika fadhila zake basi kwa yakini kabisa tutatoa sadaka sana na tutakuwa katika watendao mema



السورة: ATTAUBA 

الآية : 76

فَلَمَّآ ءَاتَىٰهُم مِّن فَضۡلِهِۦ بَخِلُواْ بِهِۦ وَتَوَلَّواْ وَّهُم مُّعۡرِضُونَ

Basi (Allah) alipowapa katika fadhila zake walizifanyia ubahili na wakakengeuka na huku wakipuuza (walichokiahidi)



السورة: ATTAUBA 

الآية : 77

فَأَعۡقَبَهُمۡ نِفَاقٗا فِي قُلُوبِهِمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ يَلۡقَوۡنَهُۥ بِمَآ أَخۡلَفُواْ ٱللَّهَ مَا وَعَدُوهُ وَبِمَا كَانُواْ يَكۡذِبُونَ

Basi (Allah) akawapa hatima ya unafiki nyoyoni mwao mpaka Siku watapokutana naye, kwa sababu ya kuwa walimhalifu Allah katika yale waliyomuahidi, na kwa sababu ya kusema kwao uwongo



السورة: ATTAUBA 

الآية : 78

أَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ سِرَّهُمۡ وَنَجۡوَىٰهُمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Hivi, (wanafiki) hawakujua kwamba Allah anajua siri zao na minong’ono yao na kwamba Allah ni Mwenye kuyajua mno (mambo) ya Ghaibu?



السورة: ATTAUBA 

الآية : 79

ٱلَّذِينَ يَلۡمِزُونَ ٱلۡمُطَّوِّعِينَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ فِي ٱلصَّدَقَٰتِ وَٱلَّذِينَ لَا يَجِدُونَ إِلَّا جُهۡدَهُمۡ فَيَسۡخَرُونَ مِنۡهُمۡ سَخِرَ ٱللَّهُ مِنۡهُمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ

Wale wanaowabeua (wanaowabeza) Waumini wanaotoa sadaka (wanapotoa kidogo huwalaumu kwamba hakitoshi, na wanapotoa kingi huwasema wanajionesha), na wasio na cha kutoa ila kadiri ya uwezo wao (wanapotoa), basi wanawakejeli (kwamba Allah hahitaji sadaka za aina hii). Allah atawalipa kwa kejeli zao, na watapata adhabu inayoumiza sana



السورة: ATTAUBA 

الآية : 80

ٱسۡتَغۡفِرۡ لَهُمۡ أَوۡ لَا تَسۡتَغۡفِرۡ لَهُمۡ إِن تَسۡتَغۡفِرۡ لَهُمۡ سَبۡعِينَ مَرَّةٗ فَلَن يَغۡفِرَ ٱللَّهُ لَهُمۡۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَفَرُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Waombee msamaha au usiwaombee (yote ni sawa). Hata ukiwaombea msamaha mara sabini (au zaidi), katu Allah hatawasamehe. Hayo ni kwa sababu wamemkufuru Allah na Mtume wake. Na Allah hawaongoi watu waovu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 81

فَرِحَ ٱلۡمُخَلَّفُونَ بِمَقۡعَدِهِمۡ خِلَٰفَ رَسُولِ ٱللَّهِ وَكَرِهُوٓاْ أَن يُجَٰهِدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَقَالُواْ لَا تَنفِرُواْ فِي ٱلۡحَرِّۗ قُلۡ نَارُ جَهَنَّمَ أَشَدُّ حَرّٗاۚ لَّوۡ كَانُواْ يَفۡقَهُونَ

Walioachwa nyuma walifurahia kwa kule kubakia kwao nyuma na kumuacha Mtume wa Allah na walichukia (kwenda) kupigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao katika Njia ya Allah na wakasema: Msiende katika (Jihadi kipindi) cha joto. Sema: Moto wa Jahanamu una joto kali zaidi, laiti kama wangekuwa wanafahamu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 82

فَلۡيَضۡحَكُواْ قَلِيلٗا وَلۡيَبۡكُواْ كَثِيرٗا جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Basi wacheke kidogo (hapa duniani) na walie sana (huko Akhera) ikiwa ni malipo ya yale waliyokuwa wakiyachuma



السورة: ATTAUBA 

الآية : 83

فَإِن رَّجَعَكَ ٱللَّهُ إِلَىٰ طَآئِفَةٖ مِّنۡهُمۡ فَٱسۡتَـٔۡذَنُوكَ لِلۡخُرُوجِ فَقُل لَّن تَخۡرُجُواْ مَعِيَ أَبَدٗا وَلَن تُقَٰتِلُواْ مَعِيَ عَدُوًّاۖ إِنَّكُمۡ رَضِيتُم بِٱلۡقُعُودِ أَوَّلَ مَرَّةٖ فَٱقۡعُدُواْ مَعَ ٱلۡخَٰلِفِينَ

Basi (Ewe Mtume Muhammad) Allah akikurudisha (salama) kwenye kundi moja miongoni mwao (hao wanafiki) na wakakuomba idhini ya kutoka (nawe kwenda vitani) sema: Nyinyi katu hamuwezi kutoka pamoja nami, na asilani hamuwezi kupigana na adui pamoja nami. Hakika, nyinyi mmeridhia kukaa nyuma mara ya kwanza, basi kaeni pamoja na hao wabakiao nyuma (wanawake, watoto na wasiojiweza)



السورة: ATTAUBA 

الآية : 84

وَلَا تُصَلِّ عَلَىٰٓ أَحَدٖ مِّنۡهُم مَّاتَ أَبَدٗا وَلَا تَقُمۡ عَلَىٰ قَبۡرِهِۦٓۖ إِنَّهُمۡ كَفَرُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَمَاتُواْ وَهُمۡ فَٰسِقُونَ

Na kamwe usimswalie yeyote katika wao (wanafiki) akifa wala usisimame kaburini kwake (na kumuombea dua). Hakika, hao wamemkufuru Allah na Mtume wake na wamekufa ilhali ni waovu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 85

وَلَا تُعۡجِبۡكَ أَمۡوَٰلُهُمۡ وَأَوۡلَٰدُهُمۡۚ إِنَّمَا يُرِيدُ ٱللَّهُ أَن يُعَذِّبَهُم بِهَا فِي ٱلدُّنۡيَا وَتَزۡهَقَ أَنفُسُهُمۡ وَهُمۡ كَٰفِرُونَ

Na zisikushangaze mali zao na watoto wao (hapa duniani). Ilivyo ni kwamba, Allah anataka kuwaadhibu kwazo duniani[1] na zitoke kwa nguvu roho zao na ilhali wao ni makafiri


1- - Rejea dokezo katika Aya ya 55 ya Sura hii.


السورة: ATTAUBA 

الآية : 86

وَإِذَآ أُنزِلَتۡ سُورَةٌ أَنۡ ءَامِنُواْ بِٱللَّهِ وَجَٰهِدُواْ مَعَ رَسُولِهِ ٱسۡتَـٔۡذَنَكَ أُوْلُواْ ٱلطَّوۡلِ مِنۡهُمۡ وَقَالُواْ ذَرۡنَا نَكُن مَّعَ ٱلۡقَٰعِدِينَ

Na inapoteremshwa Sura (inayowaamrisha) kwamba: Muaminini Allah na piganeni Jihadi pamoja na Mtume wake, wale wenye uwezo (wa mali na nguvu) miongoni mwao wanakuomba ruhusa na kusema: Tuache tuwe pamoja na wanaokaa nyuma



السورة: ATTAUBA 

الآية : 87

رَضُواْ بِأَن يَكُونُواْ مَعَ ٱلۡخَوَالِفِ وَطُبِعَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَهُمۡ لَا يَفۡقَهُونَ

Wameridhia kuwa pamoja na wabakiao nyuma (wenye nyudhuru), na nyoyo zao zikapigwa chapa kwa hivyo hawafahamu



السورة: ATTAUBA 

الآية : 101

وَمِمَّنۡ حَوۡلَكُم مِّنَ ٱلۡأَعۡرَابِ مُنَٰفِقُونَۖ وَمِنۡ أَهۡلِ ٱلۡمَدِينَةِ مَرَدُواْ عَلَى ٱلنِّفَاقِ لَا تَعۡلَمُهُمۡۖ نَحۡنُ نَعۡلَمُهُمۡۚ سَنُعَذِّبُهُم مَّرَّتَيۡنِ ثُمَّ يُرَدُّونَ إِلَىٰ عَذَابٍ عَظِيمٖ

Na miongoni mwa Mabedui waliopo pembezoni mwenu (pembezoni mwa mji wa Madina) ni wanafiki. Na katika wenyeji wa Madina pia wapo (watu) waliobobea katika unafiki. Wewe huwajui, (lakini) sisi tunawajua. Tutawaadhibu mara mbili, kisha watarudishwa kwenye adhabu kubwa mno



السورة: AL-AHZAAB 

الآية : 73

لِّيُعَذِّبَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ وَٱلۡمُشۡرِكَٰتِ وَيَتُوبَ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۗ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمَۢا

Kwa hivyo Allah anawaadhibu wanafiki wanaume, na wanafiki wanawake, na washirikina wanaume, na washirikina wanawake; na anawapokelea toba Waumini wanaume, na Waumini wanawake. Na Allah ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu



السورة: AL-FAT-HI 

الآية : 6

وَيُعَذِّبَ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ وَٱلۡمُشۡرِكَٰتِ ٱلظَّآنِّينَ بِٱللَّهِ ظَنَّ ٱلسَّوۡءِۚ عَلَيۡهِمۡ دَآئِرَةُ ٱلسَّوۡءِۖ وَغَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَلَعَنَهُمۡ وَأَعَدَّ لَهُمۡ جَهَنَّمَۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرٗا

Na awape adhabu wanafiki wanaume na wanaafiki wanawake, na washirikina wanaume na washirikina wanawake, wanao mdhania Allah dhana mbaya. Utawafikia mgeuko mbaya, na Allah awakasirikie, na awalaani, na awaandalie Jahannamu. Na hayo ni marudio maovu kabisa



السورة: AL-HADIID

الآية : 13

يَوۡمَ يَقُولُ ٱلۡمُنَٰفِقُونَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتُ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ ٱنظُرُونَا نَقۡتَبِسۡ مِن نُّورِكُمۡ قِيلَ ٱرۡجِعُواْ وَرَآءَكُمۡ فَٱلۡتَمِسُواْ نُورٗاۖ فَضُرِبَ بَيۡنَهُم بِسُورٖ لَّهُۥ بَابُۢ بَاطِنُهُۥ فِيهِ ٱلرَّحۡمَةُ وَظَٰهِرُهُۥ مِن قِبَلِهِ ٱلۡعَذَابُ

Siku wanafiki wa kiume na wanafiki wa kike watakapowaambia wale walioamini: Tungojeeni, tupate mwangaza kutokana na nuru yenu! (Wataambiwa): Rudini nyuma yenu, na mtafute huko nuru (yenu)! Kisha utawekwa ukuta baina yao wenye mlango, ndani mna rahma na nje kwa upande wake wa mbele mna adhabu



السورة: AL-HADIID

الآية : 14

يُنَادُونَهُمۡ أَلَمۡ نَكُن مَّعَكُمۡۖ قَالُواْ بَلَىٰ وَلَٰكِنَّكُمۡ فَتَنتُمۡ أَنفُسَكُمۡ وَتَرَبَّصۡتُمۡ وَٱرۡتَبۡتُمۡ وَغَرَّتۡكُمُ ٱلۡأَمَانِيُّ حَتَّىٰ جَآءَ أَمۡرُ ٱللَّهِ وَغَرَّكُم بِٱللَّهِ ٱلۡغَرُورُ

(Wanafiki) Watawaita Waumini wawambie: Je, kwani hatukuwa pamoja nanyi? Watasema: Ndio! Lakini nyinyi mmezifitini nafsi zenu, na mkasitasita; na mkatia shaka, na yakakudanganyeni matamanio ya nafsi zenu, mpaka ikawajieni amri ya Allah (umauti) na akawadanganya kwa Allah mdanganyifu.(msimfuate Allah)



السورة: AL-HADIID

الآية : 15

فَٱلۡيَوۡمَ لَا يُؤۡخَذُ مِنكُمۡ فِدۡيَةٞ وَلَا مِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ مَأۡوَىٰكُمُ ٱلنَّارُۖ هِيَ مَوۡلَىٰكُمۡۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Basi leo haitochukuliwa kutoka kwenu fidia na wala kutoka kwa waliokufuru. Makazi yenu ni moto, hayo ndio yanayostahiki kwenu, na ni marejeo mabaya yalioje



السورة: AL-MUJAADILA 

الآية : 14

۞أَلَمۡ تَرَ إِلَى ٱلَّذِينَ تَوَلَّوۡاْ قَوۡمًا غَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مَّا هُم مِّنكُمۡ وَلَا مِنۡهُمۡ وَيَحۡلِفُونَ عَلَى ٱلۡكَذِبِ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Je, hukuona wale waliofanya urafiki na watu ambao Allah Amewakasirikia?, wao si katika nyinyi, na wala si katika wao, na wanaapia uongo hali yakuwa wanajua



السورة: AL-MUJAADILA 

الآية : 15

أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدًاۖ إِنَّهُمۡ سَآءَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Allah Amewaandalia adhabu kali, hakika ni uovu ulioje waliokuwa wakiutenda