السورة: AL-BAQARAH 

الآية : 24

فَإِن لَّمۡ تَفۡعَلُواْ وَلَن تَفۡعَلُواْ فَٱتَّقُواْ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُۖ أُعِدَّتۡ لِلۡكَٰفِرِينَ

Na msipofanya (hivyo) na kamwe hamtaweza kufanya (hivyo), basi uogopeni Moto ambao nishati yake ni watu na mawe, ulioandaliwa kwa ajili ya makafiri



السورة: ANNISAI 

الآية : 56

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا سَوۡفَ نُصۡلِيهِمۡ نَارٗا كُلَّمَا نَضِجَتۡ جُلُودُهُم بَدَّلۡنَٰهُمۡ جُلُودًا غَيۡرَهَا لِيَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَزِيزًا حَكِيمٗا

Hakika, wale waliozipinga Aya zetu, tutawaingiza Motoni. Kila zinapoiva ngozi zao tutawabadilishia ngozi nyingine, ili waonje adhabu. Hakika, Allah amekuwa Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima



السورة: AL-AARAAF 

الآية : 41

لَهُم مِّن جَهَنَّمَ مِهَادٞ وَمِن فَوۡقِهِمۡ غَوَاشٖۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلظَّـٰلِمِينَ

(Waovu) Jahanamu itakua kitanda chao na juu yao nguo za moto za kujifunika. Na hivyo ndivyo tunavowalipa madhalimu



السورة: YUNUS 

الآية : 27

وَٱلَّذِينَ كَسَبُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ جَزَآءُ سَيِّئَةِۭ بِمِثۡلِهَا وَتَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ مَّا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِنۡ عَاصِمٖۖ كَأَنَّمَآ أُغۡشِيَتۡ وُجُوهُهُمۡ قِطَعٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِ مُظۡلِمًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wale waliochuma maovu, malipo ya maovu ni uovu kama huo, na yatawafika madhila, hawatakuwa na yeyote wa kuwakinga (dhidi ya) Allah (asiwaadhibu). (Hali yao itakuwa), kana kwamba nyuso zao zimefunikizwa na kipande cha usiku wa giza nene. Hao ndio watu wa motoni, watakaahumo milele



السورة: HUUD 

الآية : 106

فَأَمَّا ٱلَّذِينَ شَقُواْ فَفِي ٱلنَّارِ لَهُمۡ فِيهَا زَفِيرٞ وَشَهِيقٌ

Ama wale waovu basi hao Motoni ndio makazi yao humo watasikia sauti za Moto ukivuta pumzi ndani na kutoa nje



السورة: HUUD 

الآية : 107

خَٰلِدِينَ فِيهَا مَا دَامَتِ ٱلسَّمَٰوَٰتُ وَٱلۡأَرۡضُ إِلَّا مَا شَآءَ رَبُّكَۚ إِنَّ رَبَّكَ فَعَّالٞ لِّمَا يُرِيدُ

Watadumu humo muda wa kuwepo mbingu na ardhi, isipokuwa vile apendavyo Mola wako mlezi. Hakika Mola wako mlezi anatenda apendavyo



السورة: IBRAHIM 

الآية : 16

مِّن وَرَآئِهِۦ جَهَنَّمُ وَيُسۡقَىٰ مِن مَّآءٖ صَدِيدٖ

(Kila mkaidi ajue) Usoni (mbele) yake ipo Jahanamu (inamngoja), na atanyweshwa maji ya usaha (na damu itiririkayo kutoka kwenye mili ya watu wa Motoni)



السورة: IBRAHIM 

الآية : 17

يَتَجَرَّعُهُۥ وَلَا يَكَادُ يُسِيغُهُۥ وَيَأۡتِيهِ ٱلۡمَوۡتُ مِن كُلِّ مَكَانٖ وَمَا هُوَ بِمَيِّتٖۖ وَمِن وَرَآئِهِۦ عَذَابٌ غَلِيظٞ

Ataugugumia usaha (na damu ili akate kiu), wala hawezi kuumeza (kutokana na kinyaa na kuunguza kwake). Na (sababu za) mauti zitamjia kutoka kila upande (wa kiungo, lakini), wala hafi. Na zaidi ya hayo ipo adhabu nyingine kali zaidi



السورة: IBRAHIM 

الآية : 49

وَتَرَى ٱلۡمُجۡرِمِينَ يَوۡمَئِذٖ مُّقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ

Na utawaona wahalifu siku hiyo wamefungwa katika minyororo



السورة: IBRAHIM 

الآية : 50

سَرَابِيلُهُم مِّن قَطِرَانٖ وَتَغۡشَىٰ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ

Mavazi yao yatakuwa ya lami (nyeusi tii na yananuka), na nyuso zao zitagubikwa na Moto



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 43

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na bila shaka Jahanamu ndipo mahali pao walipoahidiwa wote (wanaokufuata)



السورة: AL-HIJRI 

الآية : 44

لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ

(Moto wa Jahanamu) una milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu waliyotengewa



السورة: AL-ISRAA 

الآية : 97

وَمَن يَهۡدِ ٱللَّهُ فَهُوَ ٱلۡمُهۡتَدِۖ وَمَن يُضۡلِلۡ فَلَن تَجِدَ لَهُمۡ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِهِۦۖ وَنَحۡشُرُهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ عُمۡيٗا وَبُكۡمٗا وَصُمّٗاۖ مَّأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ كُلَّمَا خَبَتۡ زِدۡنَٰهُمۡ سَعِيرٗا

Na anae ongozwa na Allah ndiye mwenye kuongoka kwenye haki. Na wanao potezwa na Allah hauta wapatia mtu rafiki ataae waongoa kinyume na Allah, tutawafufuwa Siku ya Kiyama ilihali ni vipofu na mabubu na viziwi. Na makaazi yao ni Jahannamu. Kila Moto ukifanya kusinzia tutazidi kuuchochea uwake kwa nguvu



السورة: AL-KAHF 

الآية : 29

وَقُلِ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَن شَآءَ فَلۡيُؤۡمِن وَمَن شَآءَ فَلۡيَكۡفُرۡۚ إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلظَّـٰلِمِينَ نَارًا أَحَاطَ بِهِمۡ سُرَادِقُهَاۚ وَإِن يَسۡتَغِيثُواْ يُغَاثُواْ بِمَآءٖ كَٱلۡمُهۡلِ يَشۡوِي ٱلۡوُجُوهَۚ بِئۡسَ ٱلشَّرَابُ وَسَآءَتۡ مُرۡتَفَقًا

Na sema: Hii ni kweli itokayo kwa Mola wako Mlezi. Basi atakaye, aamini. Na atakaye, akatae. Hakika Sisi tumewaandalia wenye kudhulumu Moto ambao utawazunguka kama khema. Na wakiomba msaada watasaidiwa kwa kupewa maji kama mafuta yaliyo tibuka. Yatakayo wababua nyuso zao. Kinywaji hicho ni kiovu mno! Na matandiko hayo ya kupumzikia ni maovu mno



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 19

۞هَٰذَانِ خَصۡمَانِ ٱخۡتَصَمُواْ فِي رَبِّهِمۡۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ قُطِّعَتۡ لَهُمۡ ثِيَابٞ مِّن نَّارٖ يُصَبُّ مِن فَوۡقِ رُءُوسِهِمُ ٱلۡحَمِيمُ

Hawa wagomvi wawili walio gombana kwa ajili ya Mola wao Mlezi. Basi walio kufuru watakatiwa nguo za moto, na yatamiminwa juu ya vichwa vyao maji yanayo chemka



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 20

يُصۡهَرُ بِهِۦ مَا فِي بُطُونِهِمۡ وَٱلۡجُلُودُ

Kwa maji hayo vitayayushwa viliomo matumboni mwao, na ngozi zao pia



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 21

وَلَهُم مَّقَٰمِعُ مِنۡ حَدِيدٖ

Na kwa ajili yao yatakuwapo marungu ya chuma



السورة: AL-HAJJ 

الآية : 22

كُلَّمَآ أَرَادُوٓاْ أَن يَخۡرُجُواْ مِنۡهَا مِنۡ غَمٍّ أُعِيدُواْ فِيهَا وَذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ

Kila wakitaka kutoka humo kwasababu ya uchungu watarudishwa humo humo, na wataambiwa: Onjeni adhabu ya kuungua!



السورة: ALMUUMINUUN 

الآية : 104

تَلۡفَحُ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ وَهُمۡ فِيهَا كَٰلِحُونَ

Moto utababua nyuso zao, nao watakuwa na nyuso zilizo kunjana



السورة: ALFURQAAN 

الآية : 12

إِذَا رَأَتۡهُم مِّن مَّكَانِۭ بَعِيدٖ سَمِعُواْ لَهَا تَغَيُّظٗا وَزَفِيرٗا

Ule Moto ukiwaona tangu mahali mbali wao watasikia hasira yake na mngurumo wake



السورة: ALFURQAAN 

الآية : 13

وَإِذَآ أُلۡقُواْ مِنۡهَا مَكَانٗا ضَيِّقٗا مُّقَرَّنِينَ دَعَوۡاْ هُنَالِكَ ثُبُورٗا

Na watakapo tupwa humo mahali dhiki, hali wamefungwa, wataomba wafe



السورة: AL-AHZAAB 

الآية : 66

يَوۡمَ تُقَلَّبُ وُجُوهُهُمۡ فِي ٱلنَّارِ يَقُولُونَ يَٰلَيۡتَنَآ أَطَعۡنَا ٱللَّهَ وَأَطَعۡنَا ٱلرَّسُولَا۠

Siku ambayo nyuso zao zitapinduliwa pinduliwa katika Moto. Watasema: Laiti tungeli mt’ii Allah, na tungeli mt’ii Mtume!



السورة: SWAAD 

الآية : 56

جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَا فَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia



السورة: SWAAD 

الآية : 57

هَٰذَا فَلۡيَذُوقُوهُ حَمِيمٞ وَغَسَّاقٞ

Ndio hivi! Basi na wayaonje maji ya moto na ya usaha!



السورة: SWAAD 

الآية : 58

وَءَاخَرُ مِن شَكۡلِهِۦٓ أَزۡوَٰجٌ

Na adhabu nyenginezo za namna hii



السورة: AZZUMAR 

الآية : 16

لَهُم مِّن فَوۡقِهِمۡ ظُلَلٞ مِّنَ ٱلنَّارِ وَمِن تَحۡتِهِمۡ ظُلَلٞۚ ذَٰلِكَ يُخَوِّفُ ٱللَّهُ بِهِۦ عِبَادَهُۥۚ يَٰعِبَادِ فَٱتَّقُونِ

Yatawekwa juu yao matabaka ya Moto, na chini yao matabaka. Kwa hayo Allah anawakhofisha waja wake. Enyi waja wangu! Nicheni Mimi!



السورة: AZZUMAR 

الآية : 72

قِيلَ ٱدۡخُلُوٓاْ أَبۡوَٰبَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۖ فَبِئۡسَ مَثۡوَى ٱلۡمُتَكَبِّرِينَ

Itasemwa: Ingieni milango ya Jahannamu mdumu humo. Basi nayo ni ubaya ulioje wa makaazi ya wenye kiburi!



السورة: GHAAFIR 

الآية : 70

ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِٱلۡكِتَٰبِ وَبِمَآ أَرۡسَلۡنَا بِهِۦ رُسُلَنَاۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Ambao wamekanusha Kitabu na yale tuliyo watuma Mitume wetu. Basi watakuja jua



السورة: GHAAFIR 

الآية : 71

إِذِ ٱلۡأَغۡلَٰلُ فِيٓ أَعۡنَٰقِهِمۡ وَٱلسَّلَٰسِلُ يُسۡحَبُونَ

Pingu Zitakapo kuwa shingoni mwao na minyororo, huku wanabu-ruzwa



السورة: GHAAFIR 

الآية : 72

فِي ٱلۡحَمِيمِ ثُمَّ فِي ٱلنَّارِ يُسۡجَرُونَ

Katika maji ya moto, kisha wanaunguzwa Motoni,