السورة: QAAF 

الآية : 30

يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٖ

Siku Tutakapoiambia Jahannam: Je, umeshajaa? Nayo itasema: Je, kuna ziada yoyote?



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 43

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ

Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 44

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ

Si cha baridi na wala si cha kunufaisha



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 51

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ

Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 52

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ

Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 53

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ

Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 54

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ

Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 55

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ

Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa



السورة: AL-WAAQIA’H 

الآية : 56

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)



السورة: ATTAHRIIM 

الآية : 6

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ وَأَهۡلِيكُمۡ نَارٗا وَقُودُهَا ٱلنَّاسُ وَٱلۡحِجَارَةُ عَلَيۡهَا مَلَـٰٓئِكَةٌ غِلَاظٞ شِدَادٞ لَّا يَعۡصُونَ ٱللَّهَ مَآ أَمَرَهُمۡ وَيَفۡعَلُونَ مَا يُؤۡمَرُونَ

Enyi walioamini! Jikingeni nafsi zenu na ahli zenu na Moto ambao kuni zake ni watu na mawe; Wanausimamia Malaika wakali, wenye nguvu, hawamuasi Allah kwa yale Anayowaamrisha na wanafanya yale wanayoamrishwa



السورة: AL-MULK 

الآية : 6

وَلِلَّذِينَ كَفَرُواْ بِرَبِّهِمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na kwa walio mkufuru Mola wao Mlezi ipo adhabu ya Jahanamu. Na ni marejeo maovu yalioje hayo!



السورة: AL-MULK 

الآية : 7

إِذَآ أُلۡقُواْ فِيهَا سَمِعُواْ لَهَا شَهِيقٗا وَهِيَ تَفُورُ

Watakapotupwa humo watausikia mngurumo wake na huku inafoka



السورة: AL-MULK 

الآية : 8

تَكَادُ تَمَيَّزُ مِنَ ٱلۡغَيۡظِۖ كُلَّمَآ أُلۡقِيَ فِيهَا فَوۡجٞ سَأَلَهُمۡ خَزَنَتُهَآ أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَذِيرٞ

Unakaribia kupasuka kwa hasira. Kila mara litakapotupwa humo kundi, walinzi wake watawauliza: Je, hakukufikieni muonyaji?



السورة: ALHAAQQA 

الآية : 31

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ

Kisha kwenye moto uwakao vikali mtupeni humo!



السورة: ALHAAQQA 

الآية : 32

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ

Mkamateni Na Mtieni Minyororo Shingoni Mwake,



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 15

كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

Sio hivyo (Hayawezekani hayo). Kwa hakika, huo ni Moto mkali kabisa



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 16

نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unaobabua kwa nguvu ngozi ya kichwani na mwilini



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 17

تَدۡعُواْ مَنۡ أَدۡبَرَ وَتَوَلَّىٰ

Unamwita yule aliyegeuza mgongo (aliyepuuza muongozo wa Allah) na akakengeuka



السورة: ALMA’RIJ 

الآية : 18

وَجَمَعَ فَأَوۡعَىٰٓ

Na akakusanya (mali) kisha akayahifadhi (katika makasha)



السورة: ALMUDDATH-THIR 

الآية : 26

سَأُصۡلِيهِ سَقَرَ

Nitamuingiza (na kumuunguza) kwenye Moto wa saqar



السورة: ALMUDDATH-THIR 

الآية : 27

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سَقَرُ

Na ni nini kitakujuulisha nini huo Moto wa Saqar?



السورة: ALMUDDATH-THIR 

الآية : 28

لَا تُبۡقِي وَلَا تَذَرُ

Haubakishi wala hauachi, (kitu chochote)



السورة: ALMUDDATH-THIR 

الآية : 29

لَوَّاحَةٞ لِّلۡبَشَرِ

Wenye kubabua vikali ngozi, (iwe nyeusi)



السورة: AL-INSAAN

الآية : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 30

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ

Nendeni kwenye kivuli chenye sehemu tatu!



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 31

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ

Hakiwafuniki, na wala hakiwa-kingi na muwako wa moto



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 32

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ

Hakika Moto huo hurusha macheche Kama majumba!



السورة: ALMURSALAAT 

الآية : 33

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ

Kana kwamba ni ngamia waku-bwa wa rangi ya manjano!



السورة: ANNABAI 

الآية : 21

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا

Hakika moto wa Jahannamu utakuwa ni wenye kuvizia